Kwanini samaki wa baharini hawafiki mikoani?

Kwanini samaki wa baharini hawafiki mikoani?

Kanda ya Ziwa pia kuna aina nyng za samak kuna ningu, nembe ila wanaishia huko huko kwann sangara na sato?
Mm nafikir kwasababu ya ladha na kuwa na kuwa na nyama nyngi

Nimeelewa hoja yako, sio samaki wote wa ziwani husambaa nchi nzima.

Ningu, gogogo, nembe, mbete hawaendi mjini.
 
Hata hapa Dar mtaani bado kuna Sato na Sangara tu..
 
Mkuu tatizo ni hawa wavuvi wa kienyeji wanavua samaki wachache kuweza kutosheleza hata soko la dar. Ukitaka kujua hii nchi yetu ina uongozi wa hovyo wewe fikiria eneo kubwa la bahari tulilo nalo, miaka zaidi ya 60 bado hatuna makampuni ya uvuvi yanayomilikiwa either na wakala wa serikali au watu binafsi. Miaka yote serikali ina wakala wa uvuvi, lakini hawana meli za kwenda kuvua bahari kuu, hivi unaweza kusema nchi kama hiyo haijalaaniwa kweli? zingatia asilimia kubwa ya watoto wana matatizo ya utapiamlo, lakini tuna kila aina ya vyakula kuanzia samaki, nyama, nk. ambavyo vina protini nyingi sana, nafikiri aliyeturoga alikwisha kufa.................
 
Ukweli ni kwamba watu wa bara wengi ni antagonistic kutumia bidhaa za bahari. Msukuma ale papa, nguru, taa, tasi? Wao watakwambia wamezoea sato na kidogo sangara.

Kuna msukuma mmoja tulikua tunafanya naye kazi tulikaa pale hotel ya Peacock nikamzoesha kula changu ndio akaanza kuwaelewa samaki wa baharini.

Na hata huko kwao Mwanza utasikia sato....sangara hawawapendi. Ila kimsingi sangara ana mnofu sana. Napenda sangara kuliko sato
Sangara siyo origin mwanza maana walipandikizwa
 
Wandugu kwanini hao samaki wa baharini hawafiki huku mikoani. Huku sijawahi ona bucha linauza samaki wa baharini. Labda vibua kidogo. Ingekuwa poa sana na sisi tupate dagaa mchele tupige na ugali.
Mabucha yote ni sangara na sato. Kwani pweza na hao samaki wengine wa baharini hawakai kwenye mafriza?

Nini kinakwamisha uduvi wasifike mikoani?
Upo mkoa gani? Dodoma tunazo na tunanunua kilo 9000 inategemea na Aina ya samaki ushindwe wewe.
 
Back
Top Bottom