Kwanini samaki wa baharini hawafiki mikoani?

Kwanini samaki wa baharini hawafiki mikoani?

Wandugu kwanini hao samaki wa baharini hawafiki huku mikoani. Huku sijawahi ona bucha linauza samaki wa baharini. Labda vibua kidogo. Ingekuwa poa sana na sisi tupate dagaa mchele tupige na ugali.
Mabucha yote ni sangara na sato. Kwani pweza na hao samaki wengine wa baharini hawakai kwenye mafriza?

Nini kinakwamisha uduvi wasifike mikoani?
Hahaha...mDASLAM anapohamia mkoan lazima kiumane...mjomba anataka mchuz wa pweza mkoan.hahahhaha.nmecheka sana...hao samak wa bahar wenyew wanashindwa kidhi soko la dar pekeee..so mkoan sahauni
 
Mkuu tatizo ni hawa wavuvi wa kienyeji wanavua samaki wachache kuweza kutosheleza hata soko la dar. Ukitaka kujua hii nchi yetu ina uongozi wa hovyo wewe fikiria eneo kubwa la bahari tulilo nalo, miaka zaidi ya 60 bado hatuna makampuni ya uvuvi yanayomilikiwa either na wakala wa serikali au watu binafsi. Miaka yote serikali ina wakala wa uvuvi, lakini hawana meli za kwenda kuvua bahari kuu, hivi unaweza kusema nchi kama hiyo haijalaaniwa kweli? zingatia asilimia kubwa ya watoto wana matatizo ya utapiamlo, lakini tuna kila aina ya vyakula kuanzia samaki, nyama, nk. ambavyo vina protini nyingi sana, nafikiri aliyeturoga alikwisha kufa.................
Mkuu umemaliza kila kitu, ndio maana Kagame amewahi kutudhihaki kuhusu kuwa na bahari na bandari. Saizi serikali imeagiza meli mbili za uvuvi haziwezi kuvuna hata theluthi ya samaki tulionao kwenye pwani yetu.

Wakala wa serikali wa uvuvi na kituo Cha uwekezaji wangewaruhusu watu wakate vibali na kukodi meli za uvuvi au kuingia ubia na kampuni za uvuvi ili wavue deep sea hii ingesaidia kupata samaki wengi, ambao wangeuzwa soko la ndani na nje. Hao samaki wangepelekea Viwanda vya kuchakata na kutengeneza by product kama sahani, rim paper na madawa.

Bahari yetu bado bikra kabisa, lakini nguvu inawekezwa kukata pesa za mitandao wakati bahari ni mgodi usioacha shimo.
 
Utamu ni relative. Watu wa pwani nao wanaona vibua ni watamu kuliko sato. Wala siyo demand. Kuna sehemu huko Kilimanjaro na Arusha hao wa Nyumba ya Mungu hawafiki. Vilevile kanda ya Ziwa kuna sehemu sato hawafiki. Kote huko nimeishi.
Demand and Supply ndugu yangu. Mimi nikiwa Moshi niache kula samaki wa Nyumba ya mungu walivyo watamu nikimbilie ya baharini ambao possibly watakuwa ghali zaidi?
 
Wandugu kwanini hao samaki wa baharini hawafiki huku mikoani. Huku sijawahi ona bucha linauza samaki wa baharini. Labda vibua kidogo. Ingekuwa poa sana na sisi tupate dagaa mchele tupige na ugali.

Mabucha yote ni sangara na sato. Kwani pweza na hao samaki wengine wa baharini hawakai kwenye mafriza?

Nini kinakwamisha uduvi wasifike mikoani?
uko mkoa gani mi nimekula sana dagaa mchele moshi kilimanjaro
 
Utamu ni relative. Watu wa pwani nao wanaona vibua ni watamu kuliko sato. Wala siyo demand. Kuna sehemu huko Kilimanjaro na Arusha hao wa Nyumba ya Mungu hawafiki. Vilevile kanda ya Ziwa kuna sehemu sato hawafiki. Kote huko nimeishi.
Yes. Utamu ni relative. Na ndiyo maana mtu wa Kilimanjaro kwa mfano anaona hana haja ya samaki wa baharini. Kama huamini kuwa demand and supply ndiyo factor basi watu wachukue hii fursa kupeleka samaki huko.
 
Wanawajua lakini? Miaka yangu mingi ya kukaa Bara mpaka 1992 nilipokuja Dar, sikuwahi kumwona pweza, kaa, kibua, kamba, nk. zaidi ya kuwaona kwenye TV. Sasa utapenda vipi chakula ambacho haujapata kukiona? Kwanza wakione...
Yes. Utamu ni relative. Na ndiyo maana mtu wa Kilimanjaro kwa mfano anaona hana haja ya samaki wa baharini. Kama huamini kuwa demand and supply ndiyo factor basi watu wachukue hii fursa kupeleka samaki huko.
 
Wanawajua lakini? Miaka yangu mingi ya kukaa Bara mpaka 1992 nilipokuja Dar, sikuwahi kumwona pweza, kaa, kibua, kamba, nk. zaidi ya kuwaona kwenye TV. Sasa utapenda vipi chakula ambacho haujapata kukiona? Kwanza wakione...
Hapo sasa. Ndiyo maana nikasema ni demand and supply. Bara hawajui kina pweza hivyo wakipelekwa kule ni hasara tupu kwa muuzaji.
 
Ni issue ya hali ya biashara (including usafirishaji) kuwa chini. Mbona Marekani pamoja na ukubwa wake ule, chakula cha kusini mwa nchi unakipata kasikazini pia? Siyo demand tu. Ni kwamba hali ya biashara iko chini. Kwa kadiri nchi inavyoendelea, ndivyo bidhaa zinazozalishwa sehemu moja ya nchi zinavyopatikana sehemu nyingine za nchi hiyo ama hata nje yake. Na sisi tutafika huko siku moja, Mungu akipenda.
Hapo sasa. Ndiyo maana nikasema ni demand and supply. Bara hawajui kina pweza hivyo wakipelekwa kule ni hasara tupu kwa muuzaji.
 
Ni issue ya hali ya biashara (including usafirishaji) kuwa chini. Mbona Marekani pamoja na ukubwa wake ule, chakula cha kusini mwa nchi unakipata kasikazini pia? Siyo demand tu. Ni kwamba hali ya biashara iko chini. Kwa kadiri nchi inavyoendelea, ndivyo bidhaa zinazozalishwa sehemu moja ya nchi zinavyopatikana sehemu nyingine za nchi hiyo ama hata nje yake. Na sisi tutafika huko siku moja, Mungu akipenda.
Sir/Madam. We are talking about our present time! My opinion was based on ''now'' and in Tanzania and not in the future or in America. Currrently, the issue is demand and supply. Wether things will change next year or ten years to come that is another story. Thanks anyway!
 
Mkuu umemaliza kila kitu, ndio maana Kagame amewahi kutudhihaki kuhusu kuwa na bahari na bandari. Saizi serikali imeagiza meli mbili za uvuvi haziwezi kuvuna hata theluthi ya samaki tulionao kwenye pwani yetu.

Wakala wa serikali wa uvuvi na kituo Cha uwekezaji wangewaruhusu watu wakate vibali na kukodi meli za uvuvi au kuingia ubia na kampuni za uvuvi ili wavue deep sea hii ingesaidia kupata samaki wengi, ambao wangeuzwa soko la ndani na nje. Hao samaki wangepelekea Viwanda vya kuchakata na kutengeneza by product kama sahani, rim paper na madawa.

Bahari yetu bado bikra kabisa, lakini nguvu inawekezwa kukata pesa za mitandao wakati bahari ni mgodi usioacha shimo.
Mkuu kwani kama mtu ana mtaji kwa hapa Tanzania kupata kibali cha kuvua deep sea inakua ni ngumu sana maana umesema wangewaruhusu watu kwa kumaanisha ni kitu kigumu sana?
 
Wandugu kwanini hao samaki wa baharini hawafiki huku mikoani. Huku sijawahi ona bucha linauza samaki wa baharini. Labda vibua kidogo. Ingekuwa poa sana na sisi tupate dagaa mchele tupige na ugali.

Mabucha yote ni sangara na sato. Kwani pweza na hao samaki wengine wa baharini hawakai kwenye mafriza?

Nini kinakwamisha uduvi wasifike mikoani?
Kwa mtu aliyekulia mkoani, samaki wa baharini kumla ni changamoto sana!!ndio maana hata watu hawana habari nao!!mi mwenyewe wamenishinda kabisa!!hata ukiwapeleka huko hawana soko!!ila samaki wa ziwani ni rahisi kwa mtu yoyote yule kumla!!baharini kuna samaki wa ajabu mno!!mfano huko usukumani nani utakayemuuzia pweza?
 
Wee Mzungu eh? There is no business in this world which is not determined by demand and supply (at least after the collapse of socialist economies). So, you can vaguely say "demand and supply" to explain any business situation even when your explanation does not apply. And that is what you are precisely doing. And I am talking about now, not tomorrow. Now, the country (Tanzania) is still backward business-wise. Transportation, and associated infrastructure, which are key to perishable goods business like fish, are not well developed. Or do not exist at all in some parts of the country. And this is NOW and tomorrow. How do you expect someone in Moshi to consume octopus when they have never seen it in the first place? They have to see it, taste it and then like it or not like it.
Sir/Madam. We are talking about our present time! My opinion was based on ''now'' and in Tanzania and not in the future or in America. Currrently, the issue is demand and supply. Wether things will change next year or ten years to come that is another story. Thanks anyway!
 
Mkuu kwani kama mtu ana mtaji kwa hapa Tanzania kupata kibali cha kuvua deep sea inakua ni ngumu sana maana umesema wangewaruhusu watu kwa kumaanisha ni kitu kigumu sana?
Ndio, kila samaki ili avuliwe lazima uwe na kibali na ulipie. Pia kama unasafirisha kwenda nje Kuna vigezo vyake.
 
Back
Top Bottom