Kwanini Serikali inawambia watu ambao haiwezi kuwaajiri waombe nafasi za ajira?

Kwanini Serikali inawambia watu ambao haiwezi kuwaajiri waombe nafasi za ajira?

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Kwenye tangazo la ajira kada ya afya na ualimu kigezo ni wahitimu waliomaliza kati ya 2012-2019.

Lakini leo bungeni waziri Ummy anasema wataajiri waliomaliza kati ya 2012 na 2015. Sasa kulikuwa na maana gani ya kuwambia waliomaliza kati ya 2016 hadi 2019 kuomba hizi ajira ikiwa kipaumbele ni wahitimu wa 2012?

Jambo lingine la kujiuliza, kipindi cha nyuma mh. Jakaya alikuwa akiajiri wahitimu kwa maelfu, sasa hawa wa 2012 wanatoka wapi au ni wale waliotumbuliwa kwa vyeti feki wanataka kurudishwa kivingine?

Mbona toka serikali ya awamu ya tano ianze kuajiri wahitimu wa miaka ya nyuma wamekuwa wakipewa kipaumbele . Je , wapo wengi kiasi gani kwamba wao hawaishi?
 
Ummy kachanganyikiwa.

Tatizo siasa zimekuwa nyingi sana.

Siku ile Wizara ya Afya wanafangaza viajira vyao 400 jamaa alikuwa anapiga siasa utafikiri wanaajiri watu laki 2.

Sasa hapo kigezo ni waliojitolea au waliohitimu mapema?
 
Kuanzia hiyo 2012 watu walipangiwa vituo kabla hata matokeo ya mwisho hayajatoka, ukiona hivyo wengi waliukimbia ualimu na kwenda private, Sasa huko mazingira sio rafiki tena wanaamua kurejesha majeshi.

Wazir ameweka wazi kabisa kuna watu waliripoti na wakala na mishahara kabisa na mpaka kukopa kwenye mabenki na wakakimbia, sasa hapa ndio anatakiwa kuwa makini kwenye hizo ajira kinyume chake anaenda kuajiri majambazi na wahujumu uchumi.
 
Ukiingia kwenye website ya baraza la mitihani ukajua idadi ya wahitimu utapata jibu sahihi. Idadi ya wahitimu ni kubwa sana, ajira za serikali haziwezi kuchukua hata nusu ya idadi kwa mwaka ndio maana wanachukua miaka ya nyuma maana ikiwa kama msoto hao ndio wameshasota sana kulilo hawa wa miaka miwili mitatu iliyopita
 
Ili kuondoa mikanganyiko mingi, na kwa kuwa wataalamu kwenye kada ya afya na ualimu wote wanakuwa wamehitimu mafunzo yao na wamepewa vyeti, kwa nini ajira kwenye halmashauri zisirudi kwa mkurugenzi?

Yaani mkurugenzi anatangaza ajira kulingana na mahitaji yake, anakuwa na kamati yake ambao ni wakuu wa idara au wawakilishi wao, pamoja na kamati ya madiwani wanapitia maombi na kupitisha wale watakaoitwa kwenye usaili. Huu utaratibu ukifanywa na kila halmashauri utaondoa mikanganyiko na malalamiko mengi....
 
Tatizo alilitengeneza jiwe , best solution hapo ni kuajir Kwa mwaka waanzie 2015 onward na watangaze kabisa ualimu na Afya sio vipaumbele tena watu wasome for their own risk .....
Kwanini unataka waanzie 2015 na sio chini ya hapo?
 
Kwanini unataka waanzie 2015 na sio chini ya hapo?
Chini ya hapo kikwete alikuwa anaajiri wote , ni upumbavu Tu kumpa nafas ya pili mjinga wakat kuna watu kibao wanatamani hata hyo first chance.....!! Kama alidharau nafas ya kwanza hakuna haja ya kumpa nafas ya pili katika mazingira ambayo maelf ya vijana wanalilia ajira
 
Ukiingia kwenye website ya baraza la mitihani ukajua idadi ya wahitimu utapata jibu sahihi. Idadi ya wahitimu ni kubwa sana, ajira za serikali haziwezi kuchukua hata nusu ya idadi kwa mwaka ndio maana wanachukua miaka ya nyuma maana ikiwa kama msoto hao ndio wameshasota sana kulilo hawa wa miaka miwili mitatu iliyopita
Baraza la mitihani na wahitimu wapi na wapi mkuu mbona unataka kuchanganya mafuta na maji. Yani unachukulia kwamba kila aliye maliza form 4/6 amehitimu elimu ya chuo kumbe wapo ambao huwa hawafanikiwi kuendelea kwa sababu ya ugonjwa, ukosefu wa pesa za kuwasomesha na wengine huwa hawamalizi chuo kwa sababu mbali mbali kama kudisco au kufukuzwa??
 
Ili kuondoa mikanganyiko mingi, na kwa kuwa wataalamu kwenye kada ya afya na ualimu wote wanakuwa wamehitimu mafunzo yao na wamepewa vyeti, kwa nini ajira kwenye halmashauri zisirudi kwa mkurugenzi? yaani mkurugenzi anatangaza ajira kulingana na mahitaji yake, anakuwa na kamati yake ambao ni wakuu wa idara au wawakilishi wao, pamoja na kamati ya madiwani wanapitia maombi na kupitisha wale watakaoitwa kwenye usaili. Huu utaratibu ukifanywa na kila halmashauri utaondoa mikanganyiko na malalamiko mengi....
Ajira zikirudishwa halmashauri ndio majanga zaidi maana ili upate utategemea kuwa na kimojawapo kati ya hivi vitatu
1. Rushwa
2. Kujuana
3. Undugu

Ukikosa kimoja wapo kati ya hivyo utasota milele
 
Hawa wa 2012 ni wale walianza private ili badae waingie serikalini sasa baada ya kuona upepo hautabiliki nao wanaomba waajiliwe na serikali
 
Chini ya hapo kikwete alikuwa anaajiri wote , ni upumbavu Tu kumpa nafas ya pili mjinga wakat kuna watu kibao wanatamani hata hyo first chance.....!! Kama alidharau nafas ya kwanza hakuna haja ya kumpa nafas ya pili katika mazingira ambayo maelf ya vijana wanalilia ajira
Nami hili swala nimekuwa nikijiuliza mda mrefu yaani mpaka 2014 hamna mwalimu aliachwa mtaani inamaana hao waliukataa ualimu sasa baada ya kusoma upepo wanarud,ni sawa na watu wa engneering wanahoji et mwaka huu hawajatakiwa kuomba nafasi za ualimu wakati haohao ukiwakuta vyuoni ndo wanadai hawawezi kuwa walimu
 
Wanasiasa wa nchi hii ni wapumbavu na malofa, hawana hata huruma na vijana wanaosota mtaani tangu kumaliza vyuo. I repeat ni wapumbavu!!!

20210422_183858.jpg
 
Chini ya hapo kikwete alikuwa anaajiri wote , ni upumbavu Tu kumpa nafas ya pili mjinga wakat kuna watu kibao wanatamani hata hyo first chance.....!! Kama alidharau nafas ya kwanza hakuna haja ya kumpa nafas ya pili katika mazingira ambayo maelf ya vijana wanalilia ajira
Wazir anawataka hawa mbona wengi wao ni above 30 na muda wao kustaafu unakaribia(utani) Pia wapo walioenda shule zaid mfano yule wa diploma na cheti walioenda kusoma degree ni kwamba walimaliza degree zao kati ya mwaka 2015 mpaka 2017 kwahiyo wana haki pia na uzoefu wao pia utasaidia.
 
Back
Top Bottom