Kwanini show nyingi za wasanii wa muziki hufanyika sana Mwanza na Kahama?

Kwanini show nyingi za wasanii wa muziki hufanyika sana Mwanza na Kahama?

Aman iwe juu yenu

Naomba kuuliza ni kwanini wasanii wengi hupenda sana kwenda kufanya show zao kahama na mwanza ambayo ni mikoa masikin kwa majubi wa takwimu za taifa

Je kahama kwa masikin kuna nini mbona show nyingi hufanyika sana pale na tena show za bei kubwa kubwa

Tena show nyingi hufanyika za one man show

Alianza alikiba akajaza uwanja kaja diamond kajaza uwanja nandy naye alijaza uwnja chege na wasanii wengi pia hujaza uwaja

Tukija kwa jiji kubwa na la pili kwa ukubwa nchi nzima ambalo kwa mujibu wa takwimu za taifa ni jiji masikin sana. Napo show hufanyika za kibabe sana tena za kila mwaka

Mwanza kunaweza fanyika show hata tano kwa siku na kila show ikajaza watu

Moja inaweza kuwa isamilo ikajaza na nyingine inaweza kuwa jembe ikajaza na nyingine inaweza kuwa villa ikajaza na nyingine inaweza gold crest ikajaza pia

Je sasa kwanini sehemu hizi masikin hutema sana pesa kushinda sehemu tajili nchini

Nawasilisha

Mayala B


Mkuu pengine huijui vizuri Kahama! Kwanza tambua kuwa Kahama ni wilaya ya pili nchini katika kuchangia pato la taifa baada ya Ilala. Kahama inamiliki migodi miwili mikubwa nchini ambayo huwalipi basic nzuri wafanyakazi wake, Acacia-Buzwagi na Acacia-Bulyanhulu ambao ndiyo mgodi mkubwa wa underground kuliko yote East and Central Africa, kuna migodi mingi sana midogo midogo ambayo inachangia kuwepo kwa mzunguko mkubwa wa pesa, kuna posho mills za kutosha ambazo huwauzia mchele wapemba, Kahama ina ardhi nzuri kwa kilimo kwahiyo watu wengi wanajipatia fedha lukuki kupitia kilimo pia kahama ni sehemu ambayo ina muingiliano mkubwa wa watu wa east africa, mfano mtu anayeenda kongo ya bukavu, Rwanda, Burundi na Uganda lazima alale Kahama.
 
Vp mkuu mzunguko wa pesa uko vzr au umekaaje kaaje mkuu(yaani kwa ujumla)?
Mwanza hali ya pesa/fedha iko vizuri, na mzunguko uko vizuri pia mahitaji muhimu sio ya gharama labda mwenyewe tu upende kujiinua!!!
Karibu Mwanza
 
Kahama ni wilaya, ila inashindana na.mkoa wa dar es salaam kuingiza.mapato ya nchi.

Niliwah enda kufanya mishe fulan pale kwa wiki tatu


Nikagundua wana Gest/Lodge na mahotel kibao na kina aina ya starehe.

Kuna Pesa kuna pesa kuna pesa kama wee ni mjanja na mwenye akili.


KUNA UKIMWI KULIKO WILAYA YOYOTE TZ KWA SASA



Kuna UKIMWI kuzidi njombe na makete?
 
Mwanza hali ya pesa/fedha iko vizuri, na mzunguko uko vizuri pia mahitaji muhimu sio ya gharama labda mwenyewe tu upende kujiinua!!!
Karibu Mwanza
Asante sana mkuu, nilishawahi kuishi kipindi flani hivi,niliona gharama za maisha zilikua za kawaida na pia wenyeji wa Mwz hawana noma na mtu kabisaa.

Ila kipindi hiki cha mzee baba ndo nilikua sina uhakika na mzunguko wa pesa kwa upande wa biashara mkuu.
 
Asante sana mkuu, nilishawahi kuishi kipindi flani hivi,niliona gharama za maisha zilikua za kawaida na pia wenyeji wa Mwz hawana noma na mtu kabisaa.

Ila kipindi hiki cha mzee baba ndo nilikua sina uhakika na mzunguko wa pesa kwa upande wa biashara mkuu.
Pako vizuri kabisa,karibu sana
 
Mwanza wasukuma bado washamba sana kuna wasanii wao huku wanaimba kisukuma yani wanapiga hela mbaya
 
Me nimezaliwa mwanza Mabatin,Ila kinacho fanya mwanza ijaze kwenye show za wasanii ni kutokana na uwepo wa vijana weng wanao toka vijiji vya mikoa ya jiran,kigoma,shinyanga,tabora n,k,Hawa vijana weng huja na ushamba flan, Na kutokana na upataji wa pesa ulivo rahis hapa mwanza vijana hawa hujikuta wana shobokea vitu kama hivyo,hata kahama ni hivo hvo.
 
Back
Top Bottom