Metacha ni mchezaji na mgunda ni kocha. Mchezaji anaingia katika timu (anasajiliwa) katika vipindi viwili tu katika msimu, lakini kocha anaingia muda wowote, hata timu kumi anaweza akabadili kwa msimu mmoja. So, ni rahisi kumuacha na kumuajiri kocha maana mapengo yanazibika na hayana kanuni ngumu, lakini mchezaji haachwi au kusajiliwa kirahisi muda wowote (mfano Feisal, Yanga hawawezi kumuacha kirahisi, ni heri kwao wamuache Nabi kuliko Feisal katikati ya msimu).
Singida walimtoa kwa Yanga kipa wao namba moja halafu wakabaki wanamtegemea kipa namba mbili na tatu, hicho ndicho kilichowashangaza wachambuzi. Yaani ni sawa na Yanga kuipa Mbeya City imchukue Djigui Diara katikati ya msimu, halafu ibaki na Johora