Kwanini siponi Amoeba? Je, kuna uhusiano gani kati ya Amoeba na Minyoo ya Ascaris?

Kwanini siponi Amoeba? Je, kuna uhusiano gani kati ya Amoeba na Minyoo ya Ascaris?

Dumelambegu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
1,052
Reaction score
257
Wakuu,

Yamenikuta mwenzenu tafadhali naomba msaada wa kitabibu.

Ni miezi miwili mfululizo sasa nakunywa dawa za amoeba lakini tatizo lipo palepale. Naendelea kuteseka na maumivu ya tumbo yanayoambatana na gas nyingi na homa na miguu kupata moto nyakati za usiku. Nimekuwa nikijisikia kama nahitaji kwenda haja lakini nikienda naishia kujikamua sana na kupata choo chenye makamasi. Kila nikipima kwenye maabara za hospitali mbalimbali na maabara zinazotoa huduma za vipimo tu, naambiwa aidha nina amoeba au nina ascaris. Baada ya vipimo, hutumia dawa na wakati mwingine dozi mbili kabisa lakini mwisho wa siku, nakaa siku kama moja tu maumivu yanarudi palepale.

Kwa upande wa amoeba, nimetumia dawa karibu zote zinazotajwa na madaktari kuwa ni nzuri including tinidazol, senitidazol, furazol, flagile, (sina uhakika na spelling), n.k. na kwa upande wa minyoo, nimetumia sana dawa aina za albendazol, zentel, combustin, n.k. Ajabu ni kwamba wakati natumia maumivu yanapungua almost yote isipokuwa tu kinachoumiza ni kichefuchefu na mwili kuchoka kutokana na kunywa dawa kali.

Nimejaribu kutumia hata alternative medication ikiwa ni pamoja na kunywa juice ya kitunguu swaumu kama ilivyosgauriwa na mdau mmoja humu JF, lakini hali ipo pale pale. Miaka ya zamani niliugua alcers (vidonda vya tumbo) lakini nilipata tiba fulani mpaka nilipona na nimekuwa nikipima mara kadhaa lakini naambiwa sina vidonda vya tumbo.

Baadhi ya madaktari wamekuwa wakisema kwamba kwa dawa nazokunywa hawaamini kama amoeba huwa haiponi au minyoo haifi. Wanachoamini wao ni kwamba mazingira ninayoishi ndiyo yanayosababisha nipate infections mara kwa mara. Madaktari hao walinishauri mambo kadhaa ya usafi ya kuzingatia. Kutokana na mateso nayopata, nimejitahidi sana kuzingatia masharti hayo, ikiwa ni pamoja na kuepuka kula vyakula mahotelini, kunywa maji yaliyochemshwa, kujiepusha na maji kuingia kinywani wakati wa kuoga, kutokula matunda na vitu kama kachumbali, n k. Pamoja na hatua hiyo, bado hali ya maumivu ipo na nikipima naambiwa aidha nina amoeba ikiwa kwenye early stage au nina minyoo aina ya ascaris. Kwa upande wa Dar nimetibiwa hospital za Agakhan, Mikocheni, Legency na vituo mvalimbali vya afya. Nikiwa Mwanza nimetibiwa sana Bugando na Sekoture. Mbeya nimetibiwa mara mbili hospitali ya rufaa na hospitali moja ipo eneo la Uyole bahati mbaya sikumbuki jina.

Ndugu zangu na hasa wadau wa jukwaa hili JF Doctor, naomba msaada wenu. Nachotaka kujua ni:-

(1) Je, kuna dawa gani nyingine ya amoeba nayoweza kujaribu ambayo ni ya uhakika katika kutibu amoeba ukiachana na hizo nilizotaja kwa uchache? Au ni tiba gani mbadala ya uhakika nayoweza kupata ili kuondoa kabisa ugonjwa huu?

(2) Kuna dawa za kienyeji baadhi zinatoka Zanzibar zinauzwa pale Kariakoo karibu na stendi ya daladala za Mwenge. Baadhi zimeandikwa kwamba zinatibu aina zote za minyoo including amoeba. Je, ni kweli kwamba amoeba ni minyoo? Kama ni minyoo, je hakuna uwezekano wa diagnosis ya kimaabara kuchanganya interpretation ya amoeba na minyoo ya ascaris? Nauliza hivi kwa sababu isije ikawa wakati mwingine natumia dozi kubwa za amoeba wakati tatizo ni minyoo ya ascaris au kinyume chake?

Wadau naomba msaada wenu wa kitabibu, asante.
 
Mkuu Dumelambegu, pole sana. Tatizo lako linafanana sana na hali inayonikuta kiasi cha kufikiri nina HIV lakini nimepima mara nne hivi naambiwa -ve. Dawa zote za amoeba ulizotaja kwa uchache nimetumia. Hata hivi navyochangia uzi huu nimetoka kukamilisha kunywa dozi mbili mfululizo la tinidazol. Bado sijaenda kupima nasubiri siku 7 zipite lakini dalili nazosikia ni kama sijapona bado. Gas ni nyingi tumboni na maumivu yapo.

Wakati fulani nilitumia juice ya vitunguu swaumu kwa kufuata ushauri uliotolewa humu jamvini na mdau mmoja. Nilipata nafuu ya muda mfupi kama wiki moja hovi halafu shida ikarejea tena. Kwa kweli na mimi nipo anxious kusikia wadau watashauri nini kuhusu tiba ya amoeba ili nami nijaribu.
 
poleni nyote waganga wapo humu watakuja kukupeni ushauri jaribuni kutoa maelezo zaidi ya vipimo mulivopima ili daktari afahamu nini azingatie kwenye ushauri
 
poleni nyote waganga wapo humu watakuja kukupeni ushauri jaribuni kutoa maelezo zaidi ya vipimo mulivopima ili daktari afahamu nini azingatie kwenye ushauri
Asante Mkuu. Vipimo ambavyo nimekuwa nikifanyiwa mara kwa mara ni vya kupitia stool, urine na damu. Kuna wakati nilifanyiwa culture ya stool. Wakati nwingine nimekuwa na mashaka kwamba labda weledi wa watu wa maabara katika kutafsiri aina ya minyoo siyo mzuri sana au vifaa vya kupimia ndiyo siyo vya uhakika. Any way, bado nina atumaini kwamba wataalam kama akina MZIZIMKAVU wanaweza kutusaidia.
 
Huna tatizo la amiba wala minyoo ya ascaris wala minyoo mingine kwa asilimia 100.Magonjwa hayo mawili uliyataja yanayokusumbua hayawezi kushindikana kupona kwa hali na mazingira ya kawaida.

Ni magonjwa madogo sana.Baccirary dysentry ni ugonjwa unaofanana mno na amiba na huenda hilo ndilo tatizo linalokusumbua kwa sababu kwenye maelezo yako hujagusia.

Hata hivyo kutokana vigezo magonjwa kama amiba, ascaris na baccilary dysentry kwa asilimia 95 ni magonjwa yanayowapata watu wajinga kabisa na watoto wadogo kwa sababu chanzo ni LAZIMA uwe umebugia mavi ya watu wengine kwa njia POOR HYGYNE.

Asilimia 5 hupata magonjwa hayo kwa bahati mbaya .hata hivyo kutokana maingiliano yamagonjwa kibayolojia nina uhakika wewe unatatizo lingine kabisa.

IMMUNE SUPPRESANT DISEASES(magonjwa kupunguza kinga mwilin kama HIV na mengine machache yana uwezo mkubwa wa kuzalisha magonjwa nyemelezi .

Hujapata daktari makini wa kukusaidia.

Ni PM
 
Sometimes patients get cured but still have psychological pain and discomfort.
 
huna tatizo la amiba wala minyoo ya ascaris wala minyoo mingine kwa asilimia 100.Magonjwa hayo mawili uliyataja yanayokusumbua hayawezi kushindikana kupona kwa hali na mazingira ya kawaida.Ni magonjwa madogo sana.Baccirary dysentry ni ugonjwa unaofanana mno na amiba na huenda hilo ndilo tatizo linalokusumbua kwa sababu kwenye maelezo yako hujagusia.Hata hivyo kutokana vigezo magonjwa kama amiba, ascaris na baccilary dysentry kwa asilimia 95 ni magonjwa yanayowapata watu wajinga kabisa na watoto wadogo kwa sababu chanzo ni LAZIMA uwe umebugia mavi ya watu wengine kwa njia POOR HYGYNE.Asilimia 5 hupata magonjwa hayo kwa bahati mbaya .hata hivyo kutokana maingiliano yamagonjwa kibayolojia nina uhakika wewe unatatizo lingine kabisa.IMMUNE SUPPRESANT DISEASES(magonjwa kupunguza kinga mwilin kama HIV na mengine machache yana uwezo mkubwa wa kuzalisha magonjwa nyemelez .hujapata dakitar makin wa kukusaidia.ni pm

Asante sana. Nashukuru kwa maelezo yako ya kitaalam. Kwa kuwa nimehangaika sana. Nitaku-PM.
 
Kuanzia sasa anza kutumia vitamin B complex (Hasa Vitamin B denk au neurosupport kidonge kimoja kwa siku) pamoja na vitamin c (angalau 1000mg kwa siku) kwa mwezi mmoja. punguza nyama nyekundu na sembe.
 
Kuanzia sasa anza kutumia vitamin B complex (Hasa Vitamin B denk au neurosupport kidonge kimoja kwa siku) pamoja na vitamin c (angalau 1000mg kwa siku) kwa mwezi mmoja. punguza nyama nyekundu na sembe.
Asante Mkuu. Kwa hali niliyonayo nitanunua na kunywa dawa hizo. Samahani Mkuu kwa usumbufu, je, unaweza kunipatia maelezo japo kwa kifupi kuhusu umuhimu wa hizo dawa na hasa kuzingatia maelezo yangu kwenye thread hii? Asante.
 
Asante Mkuu. Kwa hali niliyonayo nitanunua na kunywa dawa hizo. Samahani Mkuu kwa usumbufu, je, unaweza kunipatia maelezo japo kwa kifupi kuhusu umuhimu wa hizo dawa na hasa kuzingatia maelezo yangu kwenye thread hii? Asante.

ukiwa desparate na ugonjwa utakuja lishwa na shahawa na kuambiwa ni dawa. Hiyo dawa aliyokuambia haina tofautina na kula nyama, mboga za majani, matunda nk. Hiyo ni dietary drugs. Siwezi nikasema huumwi ila naweza kusema umepona lakini hujiamini kama umepona. With all drugs mentioned naweza kukuambia unahitaji kuamini kwamba nguvu ya MUNGU inaponya.
 
Mkuu.@Dumelambegu Pole sana kwa hayo Matatizo yako jaribu Dawa yangu hii ya Tiba Mbadala kisha uje hapa utupe Feedback umepona au bado? Fanya hivi: Tafuta majani 7 ya tunda la Mpera uyaoshe vizuri kisha uwe unayatafuna na

kumeza yale mate yake usile yale majani uhakikishe umafanya hivyo uamkapo asubuhi kabla ya kula kitu majani hayo ya

Mpera ni machungu lakini ndio dawa yenyewe ukisha kutafuna kama dakika 5 kisha uyateme hayo majani kisha ukae

kama dakika 15 kisha waweza kula kitu au kunywa maji ya kawaida fanya hivyo kila siku kwa muda wa siku 10. Kisha

nenda kapime mardhi yako kujuwa kuwa umepona au bado?

What are the herbal treatments of amoeba?


Sounds ridiculous but this is the most effective treatment here in the Phillipines. Take the new sprouted leaf of a Guava (leaf) in a guava tree of course.5-7 pieces may do. wash it with water. And chew it thoroughly inside your mouth until

crushed.the taste may be bitter but the purpose of chewing is to extract the fluid inside the guava leaves.swallow the fluid

with your saliva (do not spit out) if guava leaf if totally crushed. swallow it, swallow the crushed leaf that u just chewed. Do

not drink any liquid yet. Let it be digested for 10-15 mins. after then you can then drink water or any re hydrating liquid.


Hope this herbal treatment of mine may help you.

iStock_000010929769Small1.jpg

Majani ya Mpera yanatibu Ugonjwa wa Amoeba chanzo: by MziziMkavu
 
ukiwa desparate na ugonjwa utakuja lishwa na shahawa na kuambiwa ni dawa. Hiyo dawa aliyokuambia haina tofautina na kula nyama, mboga za majani, matunda nk. Hiyo ni dietary drugs. Siwezi nikasema huumwi ila naweza kusema umepona lakini hujiamini kama umepona. With all drugs mentioned naweza kukuambia unahitaji kuamini kwamba nguvu ya MUNGU inaponya.
I concur with you but the issue that comes around is the persistance of amoeba and ascaris when he conducts laboratory tests. Why the results are always positive? Should we question the reliability of results? If yes, can this really be true even for the case of Aghakan, Bugando and Legency Hospital, to mention a few? Please help me. I am thinking loudly and am interested to learn more on this particular subject.
 
ukiwa desparate na ugonjwa utakuja lishwa na shahawa na kuambiwa ni dawa. Hiyo dawa aliyokuambia haina tofautina na kula nyama, mboga za majani, matunda nk. Hiyo ni dietary drugs. Siwezi nikasema huumwi ila naweza kusema umepona lakini hujiamini kama umepona. With all drugs mentioned naweza kukuambia unahitaji kuamini kwamba nguvu ya MUNGU inaponya.
Unachosema ni kweli. Nimeumwa kiasi cha kuwa tayari kula chochote ilimradi nihakikishiwe kuwa kitanisaidia kupona amoeba. Ngoja niendelee kunywa hizo dietary drugs kama nilivyoshauriwa na mdau. Sidhani kama zina madhara considerable yoyote kiafya.
 
Mkuu.@Dumelambegu Pole sana kwa hayo Matatizo yako jaribu Dawa yangu hii ya Tiba Mbadala kisha uje hapa utupe Feedback umepona au bado? Fanya hivi: Tafuta majani 7 ya tunda la Mpera uyaoshe vizuri kisha uwe unayatafuna na

kumeza yale mate yake usile yale majani uhakikishe umafanya hivyo uamkapo asubuhi kabla ya kula kitu majani hayo ya

Mpera ni machungu lakini ndio dawa yenyewe ukisha kutafuna kama dakika 5 kisha uyateme hayo majani kisha ukae

kama dakika 15 kisha waweza kula kitu au kunywa maji ya kawaida fanya hivyo kila siku kwa muda wa siku 10. Kisha

nenda kapime mardhi yako kujuwa kuwa umepona au bado?

What are the herbal treatments of amoeba?


Sounds ridiculous but this is the most effective treatment here in the Phillipines. Take the new sprouted leaf of a Guava (leaf) in a guava tree of course.5-7 pieces may do. wash it with water. And chew it thoroughly inside your mouth until

crushed.the taste may be bitter but the purpose of chewing is to extract the fluid inside the guava leaves.swallow the fluid

with your saliva (do not spit out) if guava leaf if totally crushed. swallow it, swallow the crushed leaf that u just chewed. Do

not drink any liquid yet. Let it be digested for 10-15 mins. after then you can then drink water or any re hydrating liquid.


Hope this herbal treatment of mine may help you.

 iStock_000010929769Small1.jpg

Majani ya Mpera yanatibu Ugonjwa wa Amoeba chanzo: by MziziMkavu
Mkuu MziziMkavu, asante kwa maelezo yako ya tiba mbadala. Nitatumia pia ushauri wako japo kuna mdau amenihakikishia kuwa kwa maelezo niliyotoa ana uhakika kuwa siumwi. Kwamba ni ukosefu wa imani tu ndiyo unaonisumbua. Inawezekana anachosema ni kweli na maadamu nipo hapa kutafuta tiba, sitapuuza maelezo yoyote kwani wote wanaonishauri au kunielekeza wananitakia mema. Hata hivyo, kama alivyosema mdau NdasheneMbandu, ningependa kujua jambo moja nalo ni kama kweli nimepona kwa nini kila nikifanya diagnosis kwenye maabara inaonekana bado nina amoeba na ascaris? Au kuna tatizo na ubora wa vifaa vya kupimia? Hili la mwisho bado haliingii akilini.

Asante.
 
Unachosema ni kweli. Nimeumwa kiasi cha kuwa tayari kula chochote ilimradi nihakikishiwe kuwa kitanisaidia kupona amoeba. Ngoja niendelee kunywa hizo dietary drugs kama nilivyoshauriwa na mdau. Sidhani kama zina madhara considerable yoyote kiafya.

siwezi kusema maabara zote ni mbovu lakini things done by lab tech muda mwingine huwa nachanganyikiwa. Tuliwahi letewa majibu ya ccta(mtawa) yuko positive. Kufanya sie wenyewe ni negative na kurudia mara ya pili maabara hiyo hiyo majibu yakawa negative. Naomba uniambie apart from abdominal pain ulishawahi kuharisha? ....Damu? Kukosa hamu ya kula? Kuhisi tumbo limejaa? Kunya mnyoo? Kuhisi kichefuchefu? Kukohoa au kubanwa kifua kama mtu wa asthma? Unakula chakula kiasi gani kwa siku? Kina mchanganyiko? Unakunywa maji mara ngapi kwa siku? Kiasi gani?
 
Nami hilo tatizo lilinisumbua saana hadi nilipoanza matibabu kwa dr Kurwa aliyepo Mwanza
 
siwezi kusema maabara zote ni mbovu lakini things done by lab tech muda mwingine huwa nachanganyikiwa. Tuliwahi letewa majibu ya ccta(mtawa) yuko positive. Kufanya sie wenyewe ni negative na kurudia mara ya pili maabara hiyo hiyo majibu yakawa negative. Naomba uniambie apart from abdominal pain uulishawahi kuharisha? ....Damu? Kukosa hamu ya kula? Kuhisi tumbo limejaa? Kunya mnyoo? Kuhisi kichefuchefu? Kukohoa au kubanwa kifua kama mtu wa asthma? Unakula chakula kiasi gani kwa siku? Kina mchanganyiko? Unakunywa maji mara ngapi kwa siku? Kiasi gani?

Mkuu Nyalotsi, nashukuru kwa kuuliza maswali ya kitabibu yenye mwelekeo wa kujua undani wa tatizo langu na hatimaye kupatikana kwa suluhisho. Majibu yangu ni kama ifuatavyo:-

. Yes, nimewahi kuharisha japo siyo mara kwa mara.
. Yes, mara ya mwisho results zilionyesha traces za damu
. No, sijawahi kukosa kabisa hamu ya chakula
. Yes, sometimes huwa najisikia kushiba bila hata kula
. Hapana, sijawahi kunya minyoo inayoonekana dhahiri
. Hapana, sijawahi kujisikia kichefuchefu serious
. Hapana, sijawahi kubanwa kifua kabisa
. Kwa siku nakula milo miwili mchana na jioni
. Ni nadra sana kula mchanganyiko. Matunda nayaogopa
. Asubuhi nakunywa maji lita 1 kwa wakati mmoja, mchana lita 1 kwa interval fulani na jioni ni chini ya lita 1.

Hayo ndiyo majibu yangu kwa maswali uliyouliza.
 
Sorry for asking tena Dumelambegu, last episode ya kuharisha ilikuwa lini? Yalikuwa majimaji au choo laini? Umeshawahi fanyiwa stool culture? Na umri wako(if you dont mind)? na afya yako ikoje,any signs za kupungua-? Unajua mtu anayetumia dawa za minyoo kama kweli ipo ikifa inatolewa kwa njia ya haja. Kama unatumia choo cha maji(indian type) utaiona tu unless uwe unalenga kwenye kashimo. Na mtu anayekuwa na minyoo kwa muda mrefu kunakuwa na competition ya nutrient ko unajikuta unakula lakini unapungua ndo maana kwa watoto ambao ni vulnerable unaona kabisa kwamba afya yake ni mgogoro. I can suggest colonoscopy kujua what is exactly going on in your colon(utumbo mpana). Happy new year!!
 
Mkuu pole sana, nadhani hili tatizo ni kubwa tanzania lakini wataalam hawajalichukulia serious, hata mm nina experience the same problem.nimetumia dawa nyingi sana mbadala na za hospitali as u said mleta mada bt hakuna mafanikio....naomba utibiwe hospitali moja na ikiwezekana ufungue fail for record ili ukienda further iwe rahisi kusaidika..nadhani better treatment ni hizi za hospitali mana za kienyeji kama kupona ningepona mimi.go on trusting god huku ukiendelea kutibiwa.....nenda osterbay phamacy kuna flagyl zipo kwenye kikopo kimeandikwa kabisa. Kimoja kinauzwa 500 chukua vya siku kumi na anti biotics...hata mm hapa namalizia dozi hyo inasaidia kidogo.hata mm majibu ya maabara ni kama ya kwako, amiba na minyoo...pia kuna dawa moja inatumika kutibu kichocho ni adimu sana bt itakusaidia inaitwa plaz quantel....pole sana ni imani yangu tutapona
 
Kuhusu namna ya kupunguza gesi tumia maziwa fresh ya moto changanya na asali halisi vijiko viwili asubuhi na jioni.
 
Back
Top Bottom