Kwanini siponi Amoeba? Je, kuna uhusiano gani kati ya Amoeba na Minyoo ya Ascaris?

Ndugu pole sana kwa hilo tatizo. Mbegu za papai ni dawa nzuri sana ya amoeba. Zianike zikauke vizuri then zisage uchanganye kwenye chai kijiko kimoja cha chakula asubuhi na jioni kwa kama siku 3 hivi. Amoeba pamoja na malaria na minyoo yote itatoka. Ila uwe na limau karibu manake zina kichefuchefu. Pole sana ndugu. Ukifanikiwa tupe taarifa
 

Ndugu yangu Nyalotsi usijali kabisa kwa kuniuliza maswali mengi hata kama yanajirudia. Kimsingi, nipo hapa kupata suluhisho la tatizo lililonisibu muda mrefu sana. Kila maelezo utakayohitaji kwangu utayapata kadri ninavyofahamu. Sasa ningependa kujibu maswali yako kama ifuatavyo:-

Muda mrefu umepita tangu nilipoharisha kwa maana halisi ya kuharisha. Mara kwa mara nimekuwa nikipata choo cha kawaida yaani siyo kigumu wala laini sana. Ni mara chache sana napata choo kigumu kiasi cha kuumia.

Kuna wakati nilifanyiwa culture na walibaini typhoid na aina ya dawa ambayo ingefaa. Nilipata tiba na ilinisaidia. Baada ya wiki kama moja hivi niliendelea kujisikia vibaya. Nilipopima niliambiwa nina amoeba.

Umri wangu ni miaka 45.

Afya yangu kwa ujumla kimwonekano ni nzuri. Kwa kuniona, ni vigumu kubaini kama ndiye mwenye hayo matatizo. Nina haiba nzuri tu labda ni kwa sababu nakula chakula kama kawaida ingawa nateseka na maumivu ya tumbo. Kumbuka pia, nimepima mara kadhaa vidonda vya tumbo na kuambiwa sina kabisa.

Kuhusu kuona minyoo, kwa kweli sijawahi kuona. Choo ninachotumia siyo cha shimo. Hivyo, nimekuwa nikikiona choo mara kwa mara na mara zote sijawahi kuona minyoo.

Kuhusu colonoscopy ningependa kujua undani wa kipimo hicho na ni wapi kinapoweza kufanyika nifanye.

Otherwise, nikushukuru kwa kutenga muda wako wa kufuatilia tatizo langu.
 
Nimekupata dumelambegu, hicho kipimo ni kama camera ambayo inapitishwa kupitia njia ya haja kubwa ili kujua matatizo yaliyopo kwenye utumbo mkubwa. Huwa wanafanyiwa watu wenye matatizo tofauti ya utumbo mkubwa. Pia naomba nikuulize swali jingine, ulishawahi kaa na daktari mmoja kwenye matibabu yako? Kosa la mfumo wa afya wa nchi yetu unasababisha watu wawe wanaona na madaktari tofauti katika hospitali tofauti kila siku. Hii husababisha watu kutofuatiliwa vizuri kwenye maendeleo yao. Mf dr aliyeanza na wewe toka mwanzo angekuwa na mwendelezo mzuri wa vipimo pamoja na matibu kuliko ile ya leo uko na huyu kesho mwingine. Unajua consistency ya maelezo inakuwa tofauti kila siku. Na kila unayekutana naye anaanza upya kukuuliza. Ndo maana kwa wenzetu mtu anakuwa na dr wa familia ambaye anakuwa responsible kwa maendeleo ya afya yako kwani you pay him. Ushauri wangu, tafuta daktari(md au specialist wa infectious) ambaye utamuelezea vizuri tatizo lako kuanzia mwanzo mpaka mwisho aafu mjadiliane pa kuanzia. Usimfundishe kufanya kazi ila uwe kama unajadiliana naye kila hatua. (Kuna wagonjwa wanakujaga na kukuambia nahisi nna malaria niandikie dawa, inakera sana hii). Ukimpata ambaye utakuwa unamuona as a private patient ni nzuri zaidi ila ni costful kwani you have to pay for him kwani yeyed ndo ataangalia maendeleo yako kila unavyokwenda hospital.
 
Mkuu Nyalotsi, ukweli ni kwamba sijawahi kukaa na daktari mmoja kwa muda mrefu na hii inatokana na nature ya kazi yangu. Otherwide, nakubaliana na wewe kwa asilimia mia moja kwamba kutokuwa na daktari mmoja kumechangia kwa kiasi kikubwa kushamiri kwa tatizo langu la tumbo.

Lakini vilevile kuna tatizo la msingi la madaktari ninaokutana nao kuwa na sifa moja ya kutokuwa wafuatiliaji na wadadisi kiasi cha kutosha kwa lengo la kumsaidia mgonjwa. Siwezi kuwalaumu kwa sababu inawezekana hali hii ni mojawapo ya viashiria vya maslahi duni ya madaktari wetu hapa nchini kwa ujumla. Nasema hivi kwa sababu katika mara zote ambazo nilibahatika kuonana na madaktari tena wale wanaoitwa specialists wa magonjwa ya tumbo, nilitoa maelezo ya kina sana kuhusu historia ya tatizo langu. Nilijua kwa kuwa precise kwenye maelezo ya namna ninavyoumwa, wakati gani nilianza kujisikia hivyo na mazingira ya maisha ninayoishi kila siku, ingetoa picha nzuri kwa daktari kwanza kuelewa ukubwa wa tatizo lakini pili ku-single out tatizo kabla hata ya kufanya uchunguzi wa kina. Ajabu ni kwamba pamoja na kutoa maelezo hayo, nimekuwa nikiishia kutibiwa kwa mtindo wa kawaida kabisa usiohusisha utafiti mwendelezo. Hali hiyo imenikuta Mikocheni Hospital, Bugando na Agakhan Dar es Salaam. Mara zote nimekuwa mwoga wa kumweleza dokta namna ya kushughulikia tatizo langu kwa mwelekeo wa kiuchunguzi ulioelezwa hapo juu. Huwa naona kama ni kuingilia utaalam wa mtu tabia ambayo siyo nzuri. Pamoja na hayo, nitafanyia kazi ushauri wako.

Asante.
 
Kuhusu namna ya kupunguza gesi tumia maziwa fresh ya moto changanya na asali halisi vijiko viwili asubuhi na jioni.

Mkuu Munyangaa, nashukuru kwa ushauri wako ingawa naona kama una mwelekeo wa kutatua matokeo ya tatizo la msingi. Nadhani ni vizuri nijielekeze katika kutatua kiini cha tatizo yaani kisababishi cha gas nyingi tumboni. Bila shaka, ushauri ninaopewa wadau wengine unaweza kupelekea kupata ufumbuzi wa tatizo langu la msingi. Hata hivyo, ili gas isiniumize kwa sababu tayari ipo, nitatekeleza ushauri wako.
 
Mkuu Dalbega, dawa hii mbadala sijawahi kuitumia. Nitajaribu kuitumia. Labda niulize, chai inatakiwa iwe nyingi kiasi gani? Nadhani dawa hii naweza kuitumia hata kama nitakuwa kwenye uchunguzi wa kina wa tumbo langu, kama alivyoshauri Nyalotsi hapo juu.
 
Mkuu dumelambegu, daktari wa jumuia ni tofauti na personal/family doctor. Unatakiwa umpate daktari ambaye utaongea naye na atakuwa anakufanyia follow up yeye, na kama hayupo basi atakueleza umuone nani ambaye atakuwa amemuachia your history. You have to pay for his time ili akutengee muda akiwa free. Hii ya kwenda na kumkuta daktari consultation room, wagonjwa wengi na malipo asubiri mwisho wa mwezi mshahara wa serikali/mwajiri inatucost tulio wagonjwa. Kwa mtu mwenye nafasi inatakiwa kuopt for loss lakini upate the best.
 
Tulipo na tunakoelekea kama huna mtu ambaye uko naye in contact afya zetu zinawekwa rehani. Na ili iwe hivyo you have to pay for him kwa hela ya kumuona katika regular basis(siyo rushwa) manake kumwajiri ni ngumu kidogo. Kusubiri madaktari wa kuonwa kama jumuia ndo inayowagharimu wajawazito wengi kwani wanakuwa hawana close follow ups za hali yake ili intervention ya mapema ifanyike
 
Mkuu labda ungeachana na dawa za Hopsitilai, jaribu kutafuta kiini cha tatizo. Inawezekana sio Amoeba ikiwa ni upungufu wa vitamini fulani. Kuna mdau kakuambia B-Complex umuhimu wake soma hapo chini. Lakini pia jaribu wakati wote unapotumia dawa kali kama Antibitic kutumia pia na Multivitamins kwa kuwa dawa nyingine zinaondoa aina fulani ya madini au vitamini mwilini. Hivyo ukipona utapata maradhi mapya ambayo yanatokana na kuathiriwa kwa cell katika damu na kina ya mwili kushuka kitaalamu inaitwa (UKIMWI) sio HIV hapana!!.


Jaribu kununua pia Multi vitamins inatwa "21st Century Dietary Supplements" zainapatikana katika maduka makubwa ya Dawa muhimu kama Nakiete, S.H Amon, Amazon, na mengine mengi tu. Zipo za "Men" na "Women" tumia hizo za "Men" sambamba na B-Complex zitasaidie mwili kuweka sawa.



Tafuta Unga wa Dona uwe unatumia kwa ugali,

Here are HOME REMEDY FOR AMOEBA TREATMENT:

Amoebiasis Home Relief Cures | Amoebiasis Alternative Remedies

1 Comments

[TABLE="class: pagenav, align: center"]
[TR="bgcolor: transparent"]
[TH="class: pagenav_prev, bgcolor: transparent"]< Prev[/TH]
[TD][/TD]
[TH="class: pagenav_next, bgcolor: transparent"]Next >[/TH]
[/TR]
[/TABLE]


Fast Relief Home Remedies for Amoebiasis



Amoebiasis is characterized by frequent bowel movements which is caused due to bacterial or amoeba infection in the intestine.


Characteristic Symptoms


1. Semisolid stools containing mucous and blood in some cases. This has to be given great care and taken to the doctor immediately.
2. Amoebiasis is characterized by pain or recurring diarrhea in the abdomen. It's generally characterized by frequent diarrhea and hand to hand constipation.
3. The causing organism can be found in the fresh stool and this could even from medium for spreading if not properly disposed.
AYURVEDIC VIEW


The 4 types are:

1. Fire humor problem - This distortion is caused due to the pitta or digestive and excretory system problems.
2. Pitta disorder - Pitta disease is caused due to Blood flow disorders. This will create more dullness and increase in argumentative tempore and general emotional imbalance.
3. Phlegm Body Humor vitiation - This is caused due to the irregularities in body fluid supply or loss of water in the body.
4. Air body humor - This could be translated as caused due to the dosha or irregularities in the air cavity.
Amoebiasis Relief | Cures at Home


1. Dried power of bilgri is mixed with honey is to be taken twice a day. Take approximately 1tbsp of dried bilgiri for the best results.
2. A combination mix of approx ½ gm powdered nutmeg in buttermilk has to taken twice a day.
3. Fresh Juice extracted from young neem leaves and flowers serves as a perfect remedy for amebosis. This hs to taken twice a day till the cure.
4. A fruit of bael has to mixed with jaggery to form a pul like material. This remedy is found to great benificial effects.
5. Take the pulp fo the fruit of bael mixed with some jaggery.
6. Lemon Juice on an empty stomach is good to increase the fighting qualty agianst amebeosis.
7. A mix of isabgol powder and yougurt, cumin seeds serves is an excellent ayurvedic cure for ambeosis. This recipe serves excellently 2 to 3 times a day.
8. Acute Ayurvedic Amoebiasis Remedy - Here roast the unripe furity of bael and mix it with dried ginger powder. This has to taken with buttermilk 2 or 3 times a week.
9. Take jamun preparations or eat the fruit during the season.
10. Isbgol is found to be an excellent remedy for constipation. This could be taken for acute ambeosis. This holds together the stool and facilitate for the smooth passage of stool.
11. Fried Mango tree flowers is an excellent remedy for amebeosis.
______________________________________________________________________________________________________________


This article can also be accessed through



Amoebiasis Home Relief, Alternative Remedies, Amoebiasis Alternative Medicines, Amoebas Relief at Home, Stomach Infection Cures at Home



 
Asante sana ndugu yangu Nyalotsi na Mungu akubariki sana kwa mchango wako. Believe me, maelezo yako ya-create a new erra ya maisha yangu kiafya. Nitajitahidi nimpate daktari siyo kwa ajili yangu bali kwa ajili ya familia nzima. Kwangu mimi, sijali sana gharama ilimradi kugharamika huko kutaniletea afya njema kwangu, kwa mke na watoto wangu pia.
 
Mkuu Ngoswe,

Katika dawa aina za Dietary Supplements nimenunua na kuanza kutumia NEUROSUPPORT. Je, hiyo inafaa? Je, naweza kuendelea kutumia hiyo pamoja na B-Complex?

Asante.
 

mkuu, colonoscopy inapatikana pale hindu mandal dsm lakini sikushauri kwa sababu nami nina tatizo kama lako na nimeshawahi kufanya colonoscopy haijaonyesha kitu...kipimo pekee cha kujua tatizo lako ni choo tu. Na ni vyema kila mwezi au kila baada ya wiki mbili upime choo chako maabara.
 

nadhani nilikutumia post mbili, ya kwanza nimekushauri kuhusu tatizo la msingi ambalo ni amoeba na ya pili ndio hii ya kuhusu kuondoa gesi....asali na maziwa ukinywa haikupunguzii kitu chochote mwilini zaidi ya kuwa chakula na dawa kwa wakati mmoja
 
haya maradhi hayaonekani kama ni tishio lakini kiuhalisia yanatumaliza mno.
 
hawa madaktari wa tanzania ni incapable sana, wanapima magonjwa na kujua tatizo lakini wanakosa tiba sahihi ya kumpa mgonjwa
 
Ndugu Pole sana maana hata nimeshindwa nikushauri nini maana madawa umetumia mengi na kuendelea kuyatumia unazidi kuusumisha mwili na solution hajapatikana. kiukweli mimi vitunguu shaumu vilinisaidia ndio maana mpaka leo ni rafiki wa nyumba yangu yaani hakosekani kwenye matumizi mbalimbali ya mapishi. ila ninachohisi unatakiwa kwanza uujengee mwili wako kinga yaani kula matunda na vitamins mbalimbali.

Naona hapo juu kweli wamekushauri mengi sasa ni bora uanze na kimoja usichange kila kitu usijetengeneza sumu bure.

Halafu kwa wewe kama ndio imeshakuwa sugu usiende pupa. Nenda taratibu. Maana waweza fanya yote lakini still mswaki unapiga na maji yasichemshwa.

Nakuombea upone:
 
Madaktari wetu tanzania hawako seriuos na afya za wagonjwa mana unaenda kupima tatizo linaonekana lakini hupati dawa kukutibu upone
 
Tiba sahihi ya kutibu amoeba ni hii.

tumia kwa pamoja dawa hizi

1.dawa ya minyoo ie zentel au vumtrex
2.Antibiotic = DOXCYCILLIN
3.FLAGYL
4.ARITHROMYCIN
5.PANADOL
6.VITAMIN B
7.YOMESAN...........HAIPATIKANI ILA DUKA MOJA TU HAPA MJINI LA WAHINDI LINAITWA SHAMSUDIN PHARMACY LIPO POSTA ULIZA KUANZIA JMO, INGIA KATI APO MTAA WA SAMORA/UPANGA KARIBU NA MSIKITI MMOJA WA WAHINDI (muslim hindus)

kwann utumie hizi dawa kwa pamoja??????

1.Amoeba anaishi ndani ya minyoo so unatibu mzizi wa tatizo sio matokeo ie carrier. au unaua mama.

2.Yomesan inatibu hookworm kwa kuua kichwa chake badala ya kiwiliwili.kumbuka huwa wanakatika kichwa kinabaki na kuji form upya.
3.flagyl na erithromizin ndio tiba sahihi ya amoeba mwenyewe
4.antibiotic ni kwa ajili ya combination/ various bacterias/minyoo/askaris etc incl magonjwa ya zinaa au nyemelezi
5.vitamin b kukuletea hamu ya chakula.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…