Kwanini sisi waafrika pekee tuna rangi nyeusi tii, tofauti kabisa na binadamu wa mabara mengine?

Ndugu yangu hii ni Melanin colour ni rangi iliyo kuwa bora kabisa na ndio watu walio kuwa civilised kabla ya mtu mweupe kwani huyu mtu mweupe anatokana na mtu mweusi ......jua jambo moja tu kila unapo kuwa na RANGI NYEUSI sn ndio unakuwa na health skin hii ni fact sio Jokes na unapo kuwa mweupe sn ndio ngozi inapokuwa haina afya kwa maana huna kabisa SKIN PIGMENT.

Mtu mweusi anapigwa vita kila corner ili kumdidimiza tu kifikra na kiuchumi sababu wanaogopa kuja kulipiza kisasi kwa mambo yaliyofanyika nyuma .

Hata shule HISTORY mnayo fundishwa ni uwongo mtupu na mambo mengi yapo ya uwongo hata unakumbuka GEOGRAPHY tulikuwa tunaambiwa AFRICA ni BARA la TATU KWA UKUBWA BAADA YA AMERICA ulikuwa uwongo mtupu.



Sent from my SM-G975F using JamiiForums mobile app
 
Watu wa kwanza kufika America ni Vikings na Waafrica, Nilivyojuwa hilo ndio niliamini hii historia imepinduliwa juu chini
 
Ukishaamini asili yako ni laana basi unakuwa umelaaanika na mawazo yako mwenyewe.
 

Mkuu habari yko mimi naungana na wewe na hoja yako hii ni ya ukweli kabisa hiki ndicho kilichokuwepo.

Umemjibu vizuri kabisa VLADIMIR putina kuhusu hoja aliyotoa na mimi hapo kwa kuongezea ni kwamba nakubaliana na wewe ya kwamba evolution haitokei vizazi vinne au vitano na ni kweli asili ya mwanadamu ni Africa.

Uingereza kuligunduliwa fuvu la Cheddar man ambaye ni binadamu wa kale zaidi kuishi uingereza na alikuwa mweusi tiii na mpaka leo fuvu lake lipo makumbusho lakini cha kushangaza wanasayansi waliamua kuwapima DNA watu waliokuwa karibu na eneo fuvu lilipogunduliwa na wakagundua DNA zao zinafanana kabisa na za Cheddar man na cha kushangaza walikuwa wazungu pure hapo ndipo walipokubaliana kwamba ni mazingira ndiyo yaliwafanya wawe wazungu
 
Mtoa mada kaja na facts kwa kutoa mifano iliyo hai wewe umekuja na nadharia tupu sasa huoni kwamba mtoa mada yupo sahihi?
 
Wakaenda wapi? Kwahiyo baada ya ujio wa mzungu katika maeneo hayo weusi wakatokomea ama unamaanisha nini?
 
Kuna sehemu yenye jua kali kuzidi bara Asia specifically Uarabuni? Lakini mbona ni weupe na jua haliwaathiri.
 
mimi sijaamini kwamba ni mbaya ila weupe (wazungu) ndo wanaiona ni mbaya ndo maana wanatubagua na kutuita nyani, na wakaenda mbali zaidi na kusema sisi na uzao wa shetani.
Hata vibonzo vya shetani utakuta vinachorwa katika sura ya kutisha tena nyeusiiii.
 
Andalusia 700AD - 1400 AD Granada and Cordoba in Spain. Ndio maana wahispania na Portuguese wako tofauti sana kimaumbile ukilinganisha na wenzao kutoka Britain na Scandinavia.
Utofauti wao unatokana na nini? Ukiniambia maumbo utakuwa upo wrong maana kama mantiki yako ni kwamba Waafrika waliwatawala hao wazungu basi maeneo hayo pangekuwa na machotara wengi ila sehemu ambayo ni wazungu watupu zaidi ya 95% basi ni Spain.
 
Kuwa unique pekee sio sifa njema kama uko nyuma kwa kila kitu. Unaweza kuwa unique halafu u unique ukawa wenye sifa mbaya.
 
Jiulize kwanza,
1.binadamu yupi ana hasira za kijinga kuliko wengine?

2. Binadamu yupi ana wivu wa kijinga kuliko wengine?

3. Binadamu yupi ni mwizi, mbinafsi na muongo kuliko wengine?

4. Binadamu yupi ni mjuaji na mpenda masifa kuliko wengine?

5. Binadamu yupi hajiamini badala yake anaamini binadamu wengine.

NB. Kwa kifupi ili tupate ukweli na kujiamini zaidi mataifa ya Africa lazima yaungane ili wajue nguvu zetu. Walitugawa ili iwe rahisi kututawala na kupunguza uwezo wetu.
 
Lini waafrika walikuwa wamoja hadi useme wamewagawa ?
 
Ona hapa ramani ya rangi za ngozi miaka kadhaa iliyopita.

Utaona hata Afrika si "weusi" wote, maana kabla ya Wabantu kufika Afrika Kusini wakazi asilia si weusi. Vivyo hivyo Uhindi Kusini wako weusi sana. Pamoja na Australia. Watu "weupe" wanaweza kuishi pekee penye Jua kidogo. Siri yake ni kinga cha melanini katika ngozi (kinga dhidi ya mionzo hatari), na pia haja ya kupata Jua la kutosha ili mwili uweze kujenga vitamini (na hapa weusi-weusi wana hasara penye Jua kidogo).

Wataalamu huamini kwamba rangi nyesui kiasi ilipotea kwenye kaskazini kama miaka 6000 - 10,000 iliyopita, ilhali "weusi" uliongezeka kwenye ukanda wa tropiki penye Jua kali.
 
Nadharia ya mageuzi(Evolution) inaweza kuwa mada rahisi au ngumu kuielewa. Leo nitajaribu kuifanya iwe nyepese, nitatoa mifano mirahisi sana. Kabla sijakujibu swali lako kuhusu rangi ya mwafrika, nitaanza kuelezea maana ya nadharia ya mageuzi(Evolution/evolution theory), uteuzi wa asilia(natural selection) baadae ntakuja asili ya mwanadamu na mwafrika na kujibu maswali yako ya ustaarabu(civilization) japo itakuwa subjective zaidi.

Nini maana ya Nadharia ya mageuzi(Evolution)? kwa lugha raisi ni maendeleo ya maisha hapa duniani, evolution ndio inayoongoza uwepo wa maisha hapa ulimwenguni zaidi ya miaka 3.5 billion iliyopita. Maisha yalianza kama bacteria na hao bacteria wakagundua sex(kujamiiana) wakaanza kufanya mabadiliko mpaka dunia kukatokea binadamu , samaki, bacteria ,mijusi ,vyura na nk. Kuelewe zaidi kuhusu evolution tutachukulia mfano wa wanyama ila ntatumia mfano wa ndege na baadae mbwa(nikizungumzia artifical selection).

Kwa wanyama evulution inaanzia pale kwenye mbegu za kiume(sperm cell) and yai la kike(egg) cell hizo huwa zinapata mutation kwasababu ya kimazingira au kwa bahati mbaya tuu (kumbuka hii ni bahati tu hamna cell inaamua ipate mutation) . Baada ya hii mutation kinachofuata ni kuunganisha hizi seli mbili na kutengeneza mtoto. Watoto wote wanaozaliwa japo wana fanana na wazazi wao ila kila mmoja ni wakipekee, pia viumbe wanapenda kuzaa watoto wengi kwasababu ya kuongeza nafasi ya jamii yao kuishi, maana watoto wengi wa viumbe hufa wakiwa watoto. Nikitolea mfano hili jambo la upekee wa watoto ni pale watoto wa wazaa mmoja wanakuwa wengine warefu, wengine wafupi, wengine wananguvu wengine wanyonge na hizi tabia zao zinachangia katika natural selection.

Sasa tuje kwenye natural selection hapa ndio utaelewa nini maana ya evolution vizuri. Tuanze na mfano aliotumia darwins.
Katika kisiwa flani x kuna ndege walipeperushwa na kibunga kutoka bara la amerika wakatua kwenye hiko kisiwa x. Hiko kisiwa kilikua na vyakula ya kutosha na hakukuwa na maadui ambao walikuwa wanawau . Ndege wakazaliana sana (kumbuka kuwa kiumbe chochote hapa duniani kinakazi tatu amabazo ni kujistiri asife, kutafuta chakula akishashiba anatafuta kiumbe mwenzake na kuzaa nae) kama unakumbuka hapo juu kuwa mzazi mmoja anazaa watoto wenye tabia na muonekano tofauti japa wanafanana na wazazi wao na wao wenyewe kwa asilimia fulani. Kwahiyo jamii ikaongezeka na chakula kiaanza kupungua , hapo ndio vurugu linapoanza . Kwahiyo katika utofauti wao, kuna ndege walipata midomo ya kupasua mbegu , wengine kula wadudu na wengine kula vitu vingine ila kuna wengine hawakuzaliwa na sifa za kama hao ndege wengine kwa hiyo wao kupata chakula ikawashida wakafa njaa na DNA zao hazikupitishwa kwa vizazi vingine. Tukirudi kwa walioweza kuishi wakawa wanajitenga kutokana na sehemu zao za kula, kwahiyo wapasua mbegu wakawa wanakaa kivyao na wala wadudu wakawa wanakaa kivyao(kizungu wanaita Niche).

Hii ikapelekea ndege kwenye niche moja kuzaliana na kurithisa tabia na muonekana wa kupasua mbegu na vilevile wale wala wadudu walifanya hivyo hivyo. Ikumbuke kila kizazi kinazidi kutofautiana na kizazi kilichopita kwahiyo kutokana na ushindani wale viumbe waliokuwa wanaweza kupambana ndio walioweza kuishia na kuzaliana (hii inaitwa population pressure which bring survival of the fit enough) ikapita miaka zaidi ya mamilion japo walikuja ndege wa iaina moja kwenye kisiwa baadae wakawa tofauti kabisa kufika hatua wakawa aina ya ndege tofauti(specie) kiasi kwamba hawawezi tena kuzaa (wapasua mbegu walikua hawawezi tena kuzaa na walala wadudu).

hapo juu ndio ndege niliowazungumzia.

Kwa mfano huo wa juu nadhania umeanza kuelewa maana ya evolution. Ikumbukwe evolution haipangi kuwa hii kitokee huwa anatokea kwa bahati ila natural selection ndio inamalizia kazi ya kuchukua wale ambao wameweza kuhimili mazingira. Kwa kuongezea tuu evolution pia haiweizi tokea kwa kitu ambacho hakipo mfano pundamilia hana mabawa kama ndege hii itampasa pundamilia arudi hatua nyingi nyuma za kievolution afikie ile hatua ambapo zebra na ndege walishare mzee wao mmoja(so evolution has no reverse).

Mfano wengine ni kati ya mwanaume na mwanamke wanaume hawahitaji maziwa ila yapo hii inatokana na gharama ya kutengeneza gene inayoondoa maziwa kwa mwanaume kuwa kubwa sana na vilevile jinsi ya ovary zinabadilika kuwa pumbu na kinembe kuwa uume (Nimetumia mfano wa mwanaume kutokea kwa mwanamke , kwasababu binadamu wa kwanza kinadharia na kiushahidi alikua mwanamke).
Kwahiyo cha kuchukua kutoka hapo juu kabla hatujaendelea mbele ni evolution hutokea kwa bahati(bila mpangilio) ila inapangwa vizuri na natural selection, pia evolution hairudi nyuma(kama yanga nyuma mwiko😂🤣😂) .

Mpaka sasa nahisi utakuwa umeshanielewa mambo ya kuhusu evolution na natural selection sasa tunaweza kuikabili nadharia ya asili ya mwanadamua. Kabla hatujaenda mbali nataka kukusihi ufute ile picha uliyosoma sekindari na shule ya msingi kama sisi tumetokana na sokwe na evolution of a man/evolution ni kama mstari mmoja

Hii picha ya juu imetumika kuchanganya watu wengi ulimwenguni japo ilitumika kurahisia maelezo . Kwahiyo chukulia asili ya binadamu na mabadiliko yake kama picha hapo chini.

Binadamu anatoka na genus Homo na specie Sapiens, japo sisi ndio specie iliyobaki kwenye genus homo na sisi ni wamisho kufika hapa duniani. Sitoelezea sana jinsi ya sisi imekuwaje tumeweza simama na kuwa na akili hii ianhitaji uzi wake maalumu.
Tuje sasa kwenye mada yenyewe kwanini mwafrika ni mweusi na wengine ni weupe na kwanini nchi zinazoitwa zina joto hazina watu weusi.

Naomba nikukumbushe tuu kuhusu mutation niliyoelezea hapo kuwa kila kiumbe kanapitia mutation na hizo mutation kama zikitokea kwenye mbegu za uzazi basi sitarithishwa kwa vizazi vijavyo. Binadamu wa kwanza alikuwa mweusi na mpaka sasa mwafrika ni mweusi inatokana na gene moja inayoitwa melanin(gene ni kipande kwenye DNA ambayo ndio inataarifu kiwanda cha kutengeneza protini(ribosome)) hii melanine ndio inatupa dark pigmentation lakini inatumika kuzuia seli za binadamu za ngozi zisiuliwe na UV kutoka kwenye jua , maana miale ya UV huwa zina haribu cell DNA ambayo inaleta leta cancer ndio maana albino huwa wanapata cancer za ngozi kwasababu hawana/haifunguki hii gene ya melanin. Ila pia miale ya jua inatusaidia kutengeneza vitamini D(kwa ajili ya mifupa na meno) kwasababu sisi binadamu hatuna uwezo wakutengeneza vitamini yeyote( sina uhahika labda kuna chache tunaweza tengeneza).

kwahiyo baada ya kungundua umuhimu wa melanin na umuhimu wa vitamini D tuanze sasa safari ya binadamu kubadilika rangi, Kama inavyojulikana binadamu wa kale alikua mtu wa kutangatanga kwahiyo kundi la bindadamu liliondoka huku tanzania(Afrika mashariki) miaka kati ya (10000 - 10000) hiko kipindi bado dunia ilikua na baridi hao watu walipofika bara la ulaya tena hapo caucasus walifanya makazi wengine walisambaa kwenda asia wengine waliingia amerika ya kusini. Ila tutajadili ya hawa wa ulaya kufanya uzi uwe mfupi.

Kama nilivyokwisha kueleza mambo ya evolution na natural selection, tuanze angalia sababu ya kwanza ni uchache wa miale ya jua kwahiyo binadamu wa enzi hizo wakaanza pata tabu kutengeneza vitamini D3 kwaajili ya meno na mifupa nadhani mnajua mtu akiwa na mifupa milaini hawezi kimbia kwahiyo kutafuta chakula kwakwe inakuwa shida (nakukumbusha kiumbe chochote kina kazi tatu kwa mtirirko kuishi kula na kuzaa) kwahiyo watu wenye mifupa milaini walikufa mapema bila kuzaa na vizazi vyao vilipata vurugu lile lile na kwenye meno kama unameno mabovu kupata magonjwa na kushambuliwa na bacteria,virus na vidudu vingine ni rahisi kwahiyo nao walikufa mapema na ikumbukwe kibogoyo hali nyama (enzi hizo binadamu alikua hajagundua kilimo so chakula ni nyama au matunda).

Ikumbukwe evolution haisimami kwahiyo katika wale waliofika ulaya wakazaa watoto ambao ni weupe wao ikawa rahisi kutumia miale hafifu ya jua la ulaya kutengeza mifupa yenye nguvu kwahiyo waliweza kupata chakula na wao wakazaa watoto walirithisha hizo mitutation za melanin D so baada ya vizazi vingi watu weusi walipotea na wakabaki wazungu hapo tunaona natural selection watu wote unaowaona ni weupe asili yao jua ni hapo Caucasus.

Nikijibu swali la kwanini waarabu hawawi weusi tena , ninakujibu kwa nadharia mbili ya kwanza nilishasema kuwa evolution huwa hairudi nyuma kwasababu ya gharama na yapili inaitwa collective learning hii imesaidia binadamu asibadilike bali aishi na kuyaongoza mazingira yake. Mwarabu mweupe (Ikumbukwe uarabu ni tamaduni na sio race) yupo hapo jangwani si zaidi ya miaka 6000 hii haiwezi mpelekea abadilike haraka na hivyo pia kipindi mwarabu mweupe anaanza tawala hapo mashariki ya kati kilimo kilishagunduliwa na nguo pia zilishagundulia kwahiyo jua halikuweza kumchoma kama vile wazee wake walivyotoka afrika wanatembea uchi. uwezo huu wa jamii kujifunza maarifa kutoka kwa vizazi vilivyopita ndio inaitwa collective learning hii ndio imasaidia binadamu kuweza kupambana na natural selection kwa kiasi kikubwa.

Tuje kwenye civilization hilo ni somo lingine kubwa nimeona nisilijibu kwasasa ila ntabainisha vitu vya kusoma ili uweye elewa . tatufa za sababu kwanini mageuzi ya kiviwanda yalitokea UK na sio china( wakati china ilikua inachimba makaa ya mawe na chuma zamani kukilo uingereza)
NB: Mimi sio mtaalamu wa maswali ya evolution, nimejifunza yote haya kwa kuwa ni udadisi wangu kwahiyo kama kuna taarifa hapo nimeandika sio sahii naruhusu kurekebishwa na kama kuna kitu kinahitaji ufananuzi zaidi naruhusu pia kujaziwa. Elimu ni bahari sayansi haina mwisho hamna kitu sahii milele kwenye sayansi bali sayansi ipo kufichua uongo wa nadharia za huu ulimwengu.
Mimi ni mfuasi wa evolution na natural selection , nameandika hii ili msomaji wangu usipate maswali kuhusu niliyoongea kama nayaamini au nafundisha nisichoamini pia siamini katika mambo ya dini,mizimu,uchawi ,mungu na mashetani yake.
chamwisho kabisa mimi sio mwandishi mzuri nimejitahidi kuandika kwa kiswahili hizi mada ngumu naoma tuvumiliane kwa makosa ya kisafuri na kisanifu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…