Kwanini Somo la Hisabati bado ni changamoto?

Kwanini Somo la Hisabati bado ni changamoto?

Pengine tatizo sio somo. Tatizo ni namna ya ufundishaji wa somo.

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
kwa Darasa la SABA tatizo sio ufundishaji bali tatizo ni UTUNGAJI WA MTIHANI WENYEWE WA HESABATI.
mbona mitihani ya masomo mengine hawalalamiki?! Hesabati tu!!
tatizo lipo kwa NECTA namna wanavyo tunga mtihani wa hesabati kwa darasa la 7 hauzingatiii umri wala maarifa ya watahiniwa.
 
Kila kitu ni mapenzi watoto wengi wa Kitanzania hawajaekewa mapenzi ya kupenda hesabu tangu wadogo inapelekea hata wanapoingia shule wanalikacha hilo somo
 
Tatizo wamewarundikia syllabus nyingi na ngum ambazo hawana faida nazo kwenye maisha halisi....

Vipenyo,mistatili,tafuta x n.k nilifundishwa afu sijawahi kutana nayo mtaani zaidi ya magazijuto.
kwa mataifa mengine maswali kama hayo wanaulizwa wanafunzi wa vyuo lkn kwa hapa Tanzania mtoto wa Darasa la Saba ndio wanaulizwa maswali kama hayo!!!
Watoto wa Darasa la 7 kwa hapa kwetu TZ wanakuwa kati ya miaka 9 hadi 13 bado wadogo kabisa kimaarifa lkn unakuta anapewa mtihani ambao haulingani kabisa na maarifa yake!!
 
kwa Darasa la SABA tatizo sio ufundishaji bali tatizo ni UTUNGAJI WA MTIHANI WENYEWE WA HESABATI.
mbona mitihani ya masomo mengine hawalalamiki?! Hesabati tu!!
tatizo lipo kwa NECTA namna wanavyo tunga mtihani wa hesabati kwa darasa la 7 hauzingatiii umri wala maarifa ya watahiniwa.
Kinachotakiwa kuzingatiwa ni umri au topics zilizokuwa covered?

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app
 
kwa mataifa mengine maswali kama hayo wanaulizwa wanafunzi wa vyuo lkn kwa hapa Tanzania mtoto wa Darasa la Saba ndio wanaulizwa maswali kama hayo!!!
Watoto wa Darasa la 7 kwa hapa kwetu TZ wanakuwa kati ya miaka 9 hadi 13 bado wadogo kabisa kimaarifa lkn unakuta anapewa mtihani ambao haulingani kabisa na maarifa yake!!
Tuna shida kwenye sekta ya elim,mtoto wa darasa la 5 ana masomo 9 mpaka 12,huu si mzigo
 
Kiongozi math yaonekana ngum pia ni sababu walim weng wako shallow kweny ufundshaj
Mwalimu mwenyewe anakuja class kameza maswali yake mawili matatu! Kisha anawatemesha saingine anayumba yumba mpaka sio vyedi 😅 unategemea mwanafunzi aelewe😎 na kupenda somo?
 
Kila kitu ni mapenzi watoto wengi wa Kitanzania hawajaekewa mapenzi ya kupenda hesabu tangu wadogo inapelekea hata wanapoingia shule wanalikacha hilo somo
Somo la kipuuzi sana na linafundishwa kwa vitisho na stiki kwa sana 😅! Anyways tukiachana na basic operations zile za std 1-4 (Magazijuto)! Kitu kingine ambacho nimekitumia maishani kwenye hesabu ni conversion ya units of measurements tu ndio huitumia zaidi otherwise nilichopata o level kimenitosha!
 
Kulikuwa na Malengo ya kupunguza Miaka kwa Elimu ya Msingi, badala ya kuwa miaka 7 kama ilivyo sasa ilipendekezwa wasome kwa muda wa miaka 6 tu.
tuna wataalamu wa elimu wengi tu wamejazana wizarani na ktk taasisi binafsi ila hakuna mjadala wa kina unao fanyika juu ya elimu yetu haswa kuanzia na Elimu ya Msingi ambayo ndio Msingi wa kizazi cha Kitanzania.
 
NECTA tusitunge Mtihani wa Hesanati kwa Darasala la 7 kwa nia ya kuwakomoa na kwa nia ya kuaminisha wanafunzi waione hesabati ni ngumu, wacheni kuwawekea mbwembwe watoto ambao kimsingi bado hawajalomaa kimaarifa.
 
Dhana ya somo gumu tumewapa sisi wenyewe wadau wa elimu! Hii dhana inakua kizazi na kizazi
akili zikibadilika mawazo yakibadilika mtizamo huu hasi ukibadilika somo halitakua Gumu.
 
kwa Darasa la SABA tatizo sio ufundishaji bali tatizo ni UTUNGAJI WA MTIHANI WENYEWE WA HESABATI.
mbona mitihani ya masomo mengine hawalalamiki?! Hesabati tu!!
tatizo lipo kwa NECTA namna wanavyo tunga mtihani wa hesabati kwa darasa la 7 hauzingatiii umri wala maarifa ya watahiniwa.
Tatizo sio kutunga mitihani mkuu.. ata ukitungapepa rahisi sanaaa wakufeli watakuwepoo wengi tu.. ili somo halina msingi mzuri, pia watoto wana umri mdogo sanaa.. hawana uwezo mkubwa wa utambuzi katika kutatua matatizo ya kihisabati
 
Wanafunzi wa Darasa la Saba wamemaliza Mitihani yao ya kumaliza Elimu ya Msingi, lkn ktk tathimini ya haraka haraka wanafunzi wengi wanalalamika kuwa mtihani wa somo la Hisabati ulikuwa mgumu sana.

Swali ambalo nimejiuliza:

1. Kuna tatizo gani ktk somo la Hisabati kwa Elimu ya Tanzania?

2. Ni somo la Hisabati ndio Gumu au Wanao tunga mitihani ya somo la Hesabati ndio wanafanya somo lionekane kuwa gumu?
nadhani kuna haja kwa mamlaka ya Elimu kutazama kwa makini ili ibainike.

Tusitunge mitihani kama vile tunawakomoa wanafunzi. tuwapime kwa viwango vyao na kwa kulingana na upeo wao wa akili tusiwape mitihani ambayo iko juu ya uwezo wao.

Kwani kuna ulazima wa kutunga maswali "complicated"? kwa maoni yangu sioni kama kuna ulazima.
Mkuu; Naomba nianze hv: Nyumba inakuwa imara kutokana na uimara wa msingi wake. Somo la Hisabati linajengwa tangu mtoto akiwa nyumbani, then chekechea, halafu darasa la kwanza n.k. Kwa hiyo kama NYUMBANI mtoto hajapata exposure ya hesabu ni wazi Mwl. wa chekechea ana kazi ngumu sana. Na kama Wazazi wa Mtoto nao watasema na Kuamini kwamba Hesabu ni ngumu na hawamtii moyo (Encourage) mtoto wao kupenda Hisabati basi ni mlolongo unaendelea hadi chuo kikuu. Watoa Mitihani wanazingatia sana Syllabus na pengine kuna kitu kinaitwa Moderation. Maswali yanayoulizwa yanakuwa yamepitiwa tena na kurekebishwa kiwango cha kila Mwanafunzi ALIYEKUWA MSIKIVU kwa Mwl. wake anayamudu. Ni ukweli usiopingika (Hata ww ni shahidi) Mitihani ya shuleni ile ya Kumaliza Muhula Terminal exams au Mock huwa ni migumu zaidi ya ile ya Kitaifa.
Sasa, kwa vile Msingi wa Somo la Hisabati kwa mwanafunzi tangu mwanzoni ni Mbovu na ameaminishwa kuwa Hisabati ni Ngumu tutegemee nini hapo? Kumbuka hata watunga mitihani nao ni wazazi na pengine wanao watoto waliofanya Mtihani huo wa Hisabati ambao wameutunga.
Tusilaumu Watoto, Waalimu, Watunga mitihani peke yao Bali tuanzie HASA HASA kwa sisi wazazi ambao hatujali kufuatilia daftari la Hisabati (IKiwa ni pamoja na masomo mengine) ya mtoto na MBAYA ZAIDI tunawasikiliza/Tunawadekeza watoto wanapodai Hisabati ni ngumu. Mitihani haitoki nje ya kile Mwanafunzi alichofundishwa darasani -Never. Sasa kama mtoto alishaaminishwa kwamba Hisabati ni ngumu tutegemee nini? Utakapomwuliza habari ya Mtihani Atakujibu - Hisabati ilikuwa Ngumu. Tukumbuke Hisabati ndio mambo yote- Hakuna Shule, Chuo au Course yeyote ambayo Hisabati haitatakiwa kwa namna moja au nyingine. Kwa hiyo Tupende-Tusipende hatuna budi kujikita kwenye kuipend na kuifahamu Hisabati. (By the way, mm co Mwl.) lakini naipenda Hisabati.
 
Pamoja na kukosekana kwa walimu weledi ktk somo la Hisabati lkn kwa maoni yangu Hesabu za Darasa la Saba walimu wengi wanazimudu ila naona tatizo lipo kwa NECTA, Baraza la Mitihani linatunga Mitihani ya luwakomoa watoto wa Darasa la Saba badala ya kupima uwezo wao.
Mtoto wa Darasa la Saba hawezi kumtungia mtihani sawa na wa form 4 au form 2.
NECTA wanapaswa watunge mitihani kulingana na uwezo wa watoto wa Darasa la 7. mtihani uwe standard kulingana na maarifa yao/umri wao.
Mimi naona hicho kigezo cha Uwezo wa watoto sio muafaka kwani watoto wenyewe wanatofautiana sana uwezo ndo maana mtihani ule-ule kwa darasa hilo-hilo linalofundishwa na mwalimu huyo-huyo hutokea mtoto wa kwanza na wa mwisho. Hapo ni uwezo tofauti.
Umri pia sio kigezo kizuri kwani unaweza kukuta aliyekuwa wa kwanza darasani ana umri mdogo kuliko yule aliyekuwa wa mwisho.
NECTA wanatunga Mtihani kwa kuzingatia Syllabus ambayo ni moja kwa nchi nzima.
 
Wanafunzi wa Darasa la Saba wamemaliza Mitihani yao ya kumaliza Elimu ya Msingi, lkn ktk tathimini ya haraka haraka wanafunzi wengi wanalalamika kuwa mtihani wa somo la Hisabati ulikuwa mgumu sana.

Swali ambalo nimejiuliza:

1. Kuna tatizo gani ktk somo la Hisabati kwa Elimu ya Tanzania?

2. Ni somo la Hisabati ndio Gumu au Wanao tunga mitihani ya somo la Hesabati ndio wanafanya somo lionekane kuwa gumu?
nadhani kuna haja kwa mamlaka ya Elimu kutazama kwa makini ili ibainike.

Tusitunge mitihani kama vile tunawakomoa wanafunzi. tuwapime kwa viwango vyao na kwa kulingana na upeo wao wa akili tusiwape mitihani ambayo iko juu ya uwezo wao.

Kwani kuna ulazima wa kutunga maswali "complicated"? kwa maoni yangu sioni kama kuna ulazima.


Mjue Hesabu halafu mje kutamba katika sayansi na teknolojia duniani???------🤣
 
walimu wa Hesabati/Mathematics Darasa la Saba(7) tunaomba uzoefu wenu kwani nyinyi ndio mnajua tatizo haswa ni nini hadi watoto wetu/wajukuu zetu wana ona mtihani wa Hesabati ni mgumu?
je? NECTA wanatunga mtihani mgumu?
au walimu hawafundishi vizuri?
 
Back
Top Bottom