Kwanini steling ya gari haikuwekwa katikati?

wa stendi

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2016
Posts
25,190
Reaction score
27,434
Sana sana yamekuwa left hand au right hand kulinga na nchi husika.
Lakini magari kama yale ya shughuli za ujenzi au kilimo steling imewekwa katikati je kwani haya ya kawaida yalishidikana nini steling kuwekwa pale katikati?
 
Sana sana yamekuwa left hand au right hand kulinga na nchi husika .
Lakini magari kama yale ya hughuli za ujenzi au kilimo steling imewekwa katikati je kwani haya ya kawaida yalishidikana nini steling kuwekwa pale katikati?
Imewekwa pembeni kumsaidia dereva kuchungulia nje kwa urahisi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah kwenye kurud nyuma lazima nigeuke
Kana kwamba unapush Scania yenye Pulling [emoji38][emoji38]

Mtoa Mada wa stendi Nadhani Sababu ni hii apa kuweka Steering Wheel Kati ni wastage of space, So waki weka Pembeni watatengezea free space ambapo mtu ataweza kukaa ndio mana private car nyingi zina Steeling wheel pembeni na sio mitambo yenye uhitaji wa Dereva [emoji848][emoji848]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Utakuja kutuuliza na kwanini viungo vya uzazi viko katika , je ili tuone vizr🙄

The answer ni kuwa . Hizo gari unazozijua zenye stering ya katikati sio gari zinazoendeshwa public. Hilo ulijue.

Stering ya pembeni inasaidia vifuatavyo
1.kusaidia mwendeshaji kuona kilicho nyuma yake pindi atakapotaka kuama upande wa barabara.

2.kusaidia kutambua upande sahii wa barabara unapoendesha ama kupishana na magari mengine. Hasa ule mstari mweupe wa lami ndo mpaka ukizi kwa mwenzio ujue ubingwa.

3.kukupa enjoyment ya chombo, tofauti ya Bajaj trekta na gari ni mfumo pia wa steering power.

Anza na hizo kwanza.
 
Mkuu ukiweka steling kati, matatizo yanakua mengi kuliko faida,
1) mirrors zote zinakua na issue, kwa mfumo wa TZ kuna sehemu ubavuni mwa gari kushoto, huwezi kumuona kwa kupitia kioo cha kushoto (blindspot), ukisogea katikati maana yake na kioo cha kulia kitakua na changamoto. kioo cha kati pia hutaweza kukitumia maana kitakua juu ya kichwa chako.

2) utapoteza siti ya abiria mmoja, maana nafasi itayobaki kulia au kushoto haitofaa kwa mtu mzima kukaa.

3) Steeling inamakorokoro yake yanayosaidia kuifanya iwe nyepesi, sasa kwa kawaida nafasi ya mbele kati inachukuliwa na engine, sasa huoni km itakua ni changamoto kuweka na makorokoro ya steeling mbele kati?

4) huoni pia itakua changamoto kuingia na kutoka kwenye gari? imagine tabu anayoipata abiria wa siti ya nyuma kati kwenye kuingia na kutoka, sasa jaribu kumfikiria dreva atataabika kiasi gani.

5) ukitaka kuchungulia kama mbele kuna gari?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…