Kwanini Tanzania iendelee kununua ndege?

Watu na akili zo wanashangilia kununua ndege, a Nation, nchi ya kishenzi hii. What is Ndege?
Wakinunua Rwanda ndio wa kwanza mnaanza kutukana serikali kwamba inapitwa na wilaya ya Rwanda
 
🤣🤣🤣 Nimecheka sana.
 
Jamani Serikali ingetuonea TU huruma Sisi Walala Hoiii.Waache kuendelea kununua Ndege,Ili Sisi tupunguziwe makato ya kwenye miamala.Just imagine,Leo nimemtumia mama yangu hela shs 25,000 ya dawa Kule Kijijini anaumwa.Kanitumia and kwamba alipoenda kutoa hizo pesa kwa wakala,Amekatwa shs 2,900.Kabakiwa na shs 22,000.Sasa Ameshindwa kununua Dawa ya sh 24,000.Toka Jana hajanywa Dawa.Bora Serikali iendelee kufikiria chanzo lingine Cha mapato.Hii tozo ya kwenye miamala inagusa Walala hoi Sana na Wananchi wanyonge.Angalao tuendelee kukatwa Kama TU ilivyokuwa zamani kabla ya budget ya July 2021.Haya makato ya kwenye miamala yahamishiwe kwenye pombe za konyagi,K-Vant,Sigara n.k.AU HATA MAKANISANI Wakatwe 10% ya sadaka wazokusanya,maana makato Haya ya makanisa yatawarudia hao hao waamini wenyewe kupitia huduma za kijamii za ujenzi wa shule,vituo vya afya,maji,barabara n.k.KULIKO ILIVYO SASA AMBAPO BAADHI ya wachungaji Walio Wengi,sadaka wanazitumia kwa matumizi BINAFSI kwa kununua Ndege BINAFSI.Magari na majengo ya kifahari.Eee Mwenye Enzi MUNGU,Tusaidie.
 

[emoji848][emoji15][emoji3525]
 
Kwani kuna mwenye uelewa timamu asiyejua kuwa ndege zinanunuliwa ili wahusika wapate commission a.k.a 10% ?wewe na akili yako CAG kila ukaguzi wa mahesabu anabaini hasara katika uendeshaji wa hiyo biashara bado waendelea ununuzi?

Ni dhahiri kuwa sasa wameamua kufisidi kijumla bila kusumbuliwa kwa kutumia muamala wa uhakika thanks to JPM. A sure legacy.
 
Ngojeni dawa iwaingie, haiwezekani tusiwe na usafiri wa haraka internally/externally kwa sababu ya malofa wachache ambao hawataki kujituma na kufanya kazi ili kujikwamua na umasikini. Wakati SGR inapoanza watu lazima tuwe na choice ya kutumia ndege au treni kwa safari za ndani na nje pasipo na shaka, vile vile kuwa na alama ya taifa. Lazima tukomae na maendeleo ya kweli.
 
Watu wa huko vijijini huamini kabisa kwamba fedha imetolewa na viongozi. Hata ukijaribiu kuwaeleza vipi somo halipandi. Vyombo vyote vya habari vimesaidia Sana kuupotosha ukweli huu. Wakipelekewa umeme huambiwa hiyo ni hisani toka viongozi wao. Itachukua muda Sana sumu hiyo kuondoka .
 
Hilo chaka la kununua ndege linaweza kuwa na ulaji ulionona, haiwezekani nchi hii uchumi upo mochwari bado wamekazana kununua ndege ambazo hazitengenezi faida yoyote.....
 
Waambie mods uwe verified member manake Haina maaana

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…