Kwa mujibu wa katiba ipo hivyo lakini kwenye uhalisia sidhani kama hili linatekelezwa. Hili linatoa picha kuwa Rais yupo juu ya katiba. Mfano 2020, Magufuli aliwateuwa mawaziri wawili kisha ndio akapeleka jina la Majaliwa bungeni.
Nchi hii katiba huwa inakanyagwa na waliowekewa kinga na hiyo hiyo katiba. Hizi loop holes ndio zinafanya watawala kuwa juu ya sheria na kufanya lolote na hakuna la kuwafanya. This is madness.