Kwanini tukio liwe karibu na Ubalozi wa Ufaransa?

Kwanini tukio liwe karibu na Ubalozi wa Ufaransa?

Umeongea ukweli na kwa uchungu sana.

Ni kweli baadhi ya watu wanaajiriwa kwa MEMO na kwa sababu wana ndugu zao wenye vyeo bila kuwa na moyo wa ndani wa utumishi.

Lakini nadhani kwenye hii issue, hata kama una moyo wa utumishi namna gani uvamizi waliyofanyiwa hawa askari ungempata askari yeyote yule.
Sikatai mkuu ila jamaa hadi anachukua silaha kwa askari wawili waliokuwa nazo ni shida sana.

Haiwezekani askari awe na silaha kisha abweteke, wanatakiwa kuwa makini sana wawapo na silaha zao.
 
Ukiangalia video ile vizuri inaishiria kwamba jamaa alikua na tatizo la akili, yule sii gaidi hamna gaidi wa namna hiyo, angekua gaidi zaidi ya police 10 wangekufa pale kwanza hawana shabaha mtu iko kati kati ya barabara peke yake bila kizuizi chochote wanapiga lisasi zaidi ya 20 na mnamkosa askari zaidi ya 30.
Waliwahi kuua fisi kwa risasi arobain wakati wananchi huua fisi kwa mkuki mmoja tu.
 
Akili za kupiga risasi na kujua silaha alikua nazo ila wengi watu wa aina yake wanapata vichaa kutokana na trauma za vitaa, wanashindwa ku balance akili zao na wanakua na chuki na police.
Hapo nimekuelewa.
 
TETESI: Inasemekana jamaa alishuswa na bodaboda na akaenda kwenye kibanda cha askari pale kwenye makutano kama vile ana shida.

Akachomoa bastola na kuwauwa askari wawili, askari mmoja akapigwa risasi kwenye bega.

Akachukua silaha za wale askari akawa anatesa nazo.

Lakini kwanini iwe maeneo yale? Alikuwa mgeni mjini?

1. Nyumba ya balozi wa uingereza ipo kama mita hamsini kutoka kwenye sehemu ya tukio ambapo askari walipigwa risasi na kuna ulinzi wa askari wenye silaha.

2. Bank ya Stanbic ipo jirani na kawaida wanakuwepo askari wenye silaha za moto.

3. Ubalozi wa ufaransa upo maeneo yale yale ambapo kuna askari wenye silaha.

Lakini pia tukumbuke kuna msafara uliyokuwa unakaribia kupita ile barabara. Ulikuwa ni msafara wa nani?

Sheria ya ulinzi hairuhusu askari kuacha lindo na kwenda sehemu nyingine, isipokuwa pawe na genuine reason.

Kwanini walichagua hilo eneo?
Askali polisi ndiyo wazembe. Nadhani walijisahau. Kwa kawaida, ukiwa askali lindoni akikukaribia mtu lazima umuamuru mita kazaa asimame na mikono juu aseme shida yake. So askali ni wazembe!!!!!
 
1. Angekuwa Hana akili timamu asingeweza kupiga risasi yule jamaaa aliyemfuata kwenye kibanda
2. Angekuwa Hana akili timamu angeua raia hovyo kwenye daladala, magari binafsi na bajaji..lakini yeye shida yake ilikua ni Askari tu
 
Askali polisi ndiyo wazembe. Nadhani walijisahau. Kwa kawaida, ukiwa askali lindoni akikukaribia mtu lazima umuamuru mita kazaa asimame na mikono juu aseme shida yake. So askali ni wazembe!!!!!
Mudawote: Sio uzembe wa askari. Kumbuka pale askari wanapokaaga ni kibanda cha nje upande wa baharini, na watu huwa wanapita pale.

Kuna bodaboda mmoja alimgonga mtu maeneo ya pale pale leo, baada ya askari kupima ajali, askari akamwambia bodaboda aache pikipiki hapo ili ampeleke aliyemngonga hospitali.

Jamaa alivyorudi kutoka hospitali amekuta yule askari aliyemwachia pikipiki ndiye kapigwa risasi. Sasa jamaa anaumiza kichwa hiyo pikipiki anaipataje au na yeye atajumuishwa kwenye hiyo issue.
 
Hivi bongo hatunaga sniper..mbona Ile ilikua kazi ya dakika mbili tu..kuliko kurusha risasi hovyo
Ninachoelewa mimi, hata mtu awe mlenga shabaha vipi, kulenga mtu anayetembea ni kazi kubwa na hasa unapolenga na kujibanza kwa kuibia.
 
Inasemekana jamaa alishuswa na bodaboda na akaenda kwenye kibanda cha askari pale kwenye makutano kama vile ana shida.

Akachomoa bastola na kuwauwa askari wawili, askari mmoja akapigwa risasi kwenye bega.

Akachukua silaha za wale askari akawa anatesa nazo.

Lakini kwanini iwe maeneo yale? Alikuwa mgeni mjini?

1. Nyumba ya balozi wa uingereza ipo kama mita hamsini kutoka kwenye sehemu ya tukio ambapo askari walipigwa risasi na kuna ulinzi wa askari wenye silaha.

2. Bank ya Stanbic ipo jirani na kawaida wanakuwepo askari wenye silaha za moto.

3. Ubalozi wa ufaransa upo maeneo yale yale ambapo kuna askari wenye silaha.

Lakini pia tukumbuke kuna msafara uliyokuwa unakaribia kupita ile barabara. Ulikuwa ni msafara wa nani?

Sheria ya ulinzi hairuhusu askari kuacha lindo na kwenda sehemu nyingine, isipokuwa pawe na genuine reason.

Kwanini walichagua hilo eneo?

UPDATES:

Askari polisi watatu ndiyo waliyopigwa risasi na yule gaidi kutumia pistol.

Mlinzi wa SGS pia amefariki, na takriban raia sita wamejeruhiwa.
Mkuu achana na ambush...ni kitu mbaya...
 
Mkuu achana na ambush...ni kitu mbaya...
Ni ambush kweli, japo askari waliamini jamaa ana shida kweli, lakini kumbe alikuwa ana lake kichwani.

Yule askari aliyepigwa bega kumbe alikuwa anakimbia ndiyo akawashwa ya nyuma na kudondoka akikimbilia baharini.
 
Inawezekana! Japo sijafurahia askari wetu. Walivyompiga risasi na jamaa akadondoka, ilitakiwa kumnyang'anya silaha na kuokoa maisha yake ili wapate mengi kutoka kwake.
Askari wa Africa hawa heshimu wahai wa watu, kwaza kulikua hamna haja ya kumumiminia lisasi nyingi mtu tayari kasha pingwa chini, askri wetu wanakosa uledi na professionalism.
 
Back
Top Bottom