Kwanini tuna watakatifuza (kuwapa utakatifu) viongozi waovu?

Kwanini tuna watakatifuza (kuwapa utakatifu) viongozi waovu?

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2016
Posts
14,311
Reaction score
36,056
Amani iwe nanyi

Maandiko matakatifu yanasema, tutahukumiwa kwa kadiri ya matendo yetu. Kwani ata mambo tuyafanyayo sirini, mwenye-enzi Mungu ambaye ndiye hakimu wa haki anayaona.

Kwa muktadha huo basi, sisi wanadamu tunapata wapi mamlaka ya kuwatakatifuza viongozi wetu? Nina pata ukakasi ninaposikia kiongozi huyu au yule anafanyiwa mchakato ili atangazwe mtakatifu au yuko mbinguni.

Huu ujasiri tunautoa wapi, je sisi ni mawakala au wasaidizi wa huyo hakimu wa haki? Je hatuoni kama tuna mpangia nini cha kufanya wakati anatekeleza majukumu yake? Ni nani anayeweza kumpangia Mungu kitu cha kufanya au kushawishi namna ya kutekeleza majukumu yake.

Mungu wetu ni mwenye huruma na si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa rehema, lakini hatupaswi kumdhihaki. Utakatifu ni kufanana na Mungu, kuwa na matendo yanayo fanana na ya Mungu. Je tuna weza shuhudia hayo kwa hao wapendwa wetu?

Katika mizania ya kibinadamu viongozi wetu waliotangulia mbele ya haki hawakutufanyia haki, walishindwa kuongoza nchi yetu kiuadilifu na hawakutumia rasilimali zetu vizuri.

Kwa miaka zaidi ya hamsini ya uhuru, nchi yetu bado ni masikini na watu wetu bado ni mafukara. Walishindwa kuweka na kutetea haki, watu walidhulumiwa mali zao kwa misingi ya sera za kisiasa ( ujamaa na kujitegemea), watu walikufa kwa njaa kwa kutekeleza sera za vijiji vya ujamaa na uchumi wetu uliporomoka kwa kupigana vita isiyo na msingi na yule joker Idd Amini.

Kwa kuamua kupigana vita peke yake, maisha ya askari, watu, wanawake na watoto wasio na hatia yalipotea. Watu wengi walipoteza mali na wapendwa wao kwa sababu ya vita ambayo ingeweza kuepukika.

Ukiachilia udhalimu wa awamu hiyo, awamu ya tano ndiyo mbaya zaidi, watu walikatwa mikia, waliporwa mali zao, account zao kwenye benki zilifilisiwa na wenyewe kutishiwa vifungo, wanasiasa waliwekwa magerezani, wengine hawajulikani walipo mpaka sasa. Kiasi cha zaidi ya 4 Trillion kimepotea... kimsingi serikali iligeuka jambazi, na mpaka sasa hela za plea bargain hazijulikani zilipo.

Kwa moyo mkunjufu kabisa, nina waomba ndugu zangu, tusimdhihaki Mungu kuingiza siasa zetu za kibinadamu kwenye michakato ya Mungu. Wapo watu wanyonge, wajane na yatima wanaomlilia Mungu kwa madhila ya udhalimu wa viongozi weu, je mnataka Mungu asiwasikilize kwa sababu zenu za kisiasa za kutaka kutukuza na kutakatifuza udhalimu?

Tusimtanie Mungu.
 
Tungekuwa na katiba nzuri wala tusingefika huko. Kwani:

1. Madhwalimu wasingepata nafasi za uongozi.
2. Madhwalimu wasingedumu uongozini.
3. Dhwalimu yeyote angekuwa mahali pake pa kudumu Segerea huko, akin*ea debe kwa wakati.
4. Nk, nk.

Ingepatikana vipi au wapi fursa ya kuchoshana na nyimbo zisizoimbika za legasi hadi mahekaluni huko?
 
Hakika mkuu, katiba nzuri ni matamanio ya kila mpenda haki
Tupiganie katiba nzuri ndugu zangu hata kama waliokuwa washirika wetu wakuu kwenye hili wanaonekana kutepeta.

Katiba ni ya wananchi na nchi ni ya wananchi.

Penye nia pana njia.
 
Tupiganie katiba nzuri ndugu zangu hata kama waliokuwa washirika wetu wakuu kwenye hili wanaonekana kutepeta.

Katiba ni ya wananchi na nchi ni ya wananchi.

Penye nia pana njia.
Hakika mkuu
 
Tupiganie katiba nzuri ndugu zangu hata kama waliokuwa washirika wetu wakuu kwenye hili wanaonekana kutepeta.

Katiba ni ya wananchi na nchi ni ya wananchi.

Penye nia pana njia.
Umenena. Ila haya hayatokuja kuja kwa maneno matupu. Vitendo lazima vionekane. Kungojea katiba iletwe kama maziwa ni ndoto za mchana. Sasa kazi ni kwetu; kusuka au kunyoa.
 
Zile kelele za Katiba Mpya zenyewe naona ni kama zimeshakufa, sasa kama.tumeshachoka kupiga kelele tu, vipi tutaweza vipi kuanzisha vitendo vitakavyoamsha ari kwa watanzania waanze kuipigania Katiba Mpya?

Tatizo letu tuliacha hilo jukumu kwa wanasiasa hasa Chadema, sasa nao ni kama wamelala, matokeo yake tumebaki hatujui wapi pakushika ili kuendeleza yale mapambano, bora kama pangekuwepo na mgawanyo wa mapambano ili kama akilala mmoja, mwingine aamke, kazi iendelee..
 
KWA wakatoliki watakatifu ni cheo cha heshima kama tuzo KWA mema waliyojitoa kwa kanisa. Ni kama kuwapa daraja la heshima.
 
Umenena. Ila haya hayatokuja kuja kwa maneno matupu. Vitendo lazima vionekane. Kungojea katiba iletwe kama maziwa ni ndoto za mchana. Sasa kazi ni kwetu; kusuka au kunyoa.
Hata hio katiba ikiwa mpya unadhani inaweza mfunga paka kengele?
 
Tungekuwa na katiba nzuri wala tusingefika huko. Kwani:

1. Madhwalimu wasingepata nafasi za uongozi.
2. Madhwalimu wasingedumu uongozini.
3. Dhwalimu yeyote angekuwa mahali pake pa kudumu Segerea huko, akin*ea debe kwa wakati.
4. Nk, nk.

Ingepatikana vipi au wapi fursa ya kuchoshana na nyimbo zisizoimbika za legasi hadi mahekaluni huko?
Mfumo hauwezi ishinda tabia
 
KWA wakatoliki watakatifu ni cheo cha heshima kama tuzo KWA mema waliyojitoa kwa kanisa. Ni kama kuwapa daraja la heshima.
By necessarily implication wana maana huyo marehemu yuko na Mungu mbinguni
 
Umenena. Ila haya hayatokuja kuja kwa maneno matupu. Vitendo lazima vionekane. Kungojea katiba iletwe kama maziwa ni ndoto za mchana. Sasa kazi ni kwetu; kusuka au kunyoa.

Ninakubaliana nawe 100%. Palikuwa na uzi humu:

Ni Tanzania tu, tunakotaka mabadiliko bila vitendo

Kwa hakika hadi sasa yote yamekwisha semwa kilichobakia ni vitendo tu:

Ninakazia:

"Vile vile tufike mahali tuambiane ukweli. Wenye maneno matupu au maoni, ni heri wakakaa nayo tu. Hayahitajiki."

Siyo siri tena. Kwa hapa tulipo hatunao viongozi wa kutuongoza kwenye tunayoyataka. Hapa ndipo pa kuanzia:

"Tupange safu za viongozi wetu kulingana na matokeo tunayotaka."
 
Ninakubaliana nawe 100%. Palikuwa na uzi humu:


Kwa hakika hadi sasa yote yamekwisha semwa kilichobakia ni vitendo tu:

Ninakazia:

"Vile vile tufike mahali tuambiane ukweli. Wenye maneno matupu au maoni, ni heri wakakaa nayo tu. Hayahitajiki."

Siyo siri tena. Kwa hapa tulipo hatunao viongozi wa kutuongoza kwenye tunayoyataka. Hapa ndipo pa kuanzia:

"Tupange safu za viongozi wetu kulingana na matokeo tunayotaka."
Tunapanga vipi hizo safu za uongozi?
 
Zile kelele za Katiba Mpya zenyewe naona ni kama zimeshakufa, sasa kama.tumeshachoka kupiga kelele tu, vipi tutaweza vipi kuanzisha vitendo vitakavyoamsha ari kwa watanzania waanze kuipigania Katiba Mpya?

Tatizo letu tuliacha hilo jukumu kwa wanasiasa hasa Chadema, sasa nao ni kama wamelala, matokeo yake tumebaki hatujui wapi pakushika ili kuendeleza yale mapambano, bora kama pangekuwepo na mgawanyo wa mapambano ili kama akilala mmoja, mwingine aamke, kazi iendelee..

Mpigania haki hachoki. Anayejinasibu kuwa mpigania haki akichoka huyo ni opportunist tu.

Katiba ni ya wananchi na nchi ni ya wananchi. Tunao ufumbuzi wa matakwa yetu kwa kuwaweka wanasiasa maslahi (opportunists) pembeni wanako stahili.

Kwenye uzi huu hapa chini palikuwa na mwarobaini wa hili:

Makamanda tunayo ya kujifunza kwa Raila Odinga

Manguli wengi wakiwamo maprofesa Shivji, Lwaitama nk wamekuwa na mawazo kama haya kwa muda mrefu.

Hizi siasa za kugombea upinzani ukuu, ubunge, uwakilishi, udiwani, ruzuku na vya namma hiyo baina ya vyama hazina maslahi kwetu wala hailipi.

"Kutwa kucha yule msaliti miye ndiye bora. Kwamba miye ndiye mpinzani wa kweli yule anatumiwa, nk."

Katiba mpya italetwa kundi moja la watu wasiokuwa malaika? Watu hao wanaweza kuwa waliwahi kutuhumiwa, kuhukumiwa au watu safi wasiokuwa na tuhuma wala hukumu dhidi yao.

Tunaka katiba mpya; vyama kuzodoana au machinga, vicoba, mama lishe, na kadhalika kuzodolewa ni kwa maslahi ya nani?

Tunataka katiba mpya; kupalilia utengano wa namna yoyote ni kwa manufaa ya nani? Hatuna hata utayari wa kujifunza kwa wengine?

Makamanda tunayo ya kujifunza kwa Raila Odinga

Penye nia pana njia.

Cc: Zawadini Paskali
 
Mpigania haki hachoki. Anayejinasibu kuwa mpigania haki akichoka huyo ni opportunist tu.

Katiba ni ya wananchi na nchi ni ya wananchi. Tunao ufumbuzi wa matakwa yetu kwa kuwaweka wanasiasa maslahi (opportunists) pembeni wanako stahili.

Kwenye uzi huu hapa chini palikuwa na mwarobaini wa hili:


Manguli wengi wakiwamo kina Prof. Shivji wamekuwa na mawazo kama haya kwa muda mrefu.

Hizi siasa za kugombea upinzani ukuu, ubunge, uwakilishi, udiwani, ruzuku na vya namma hiyo baina ya vyama Haina maslahi kwetu wala hailipi.

"Kutwa kucha yule msaliti miye ndiye bora. Kwamba miye ndiye mpinzani wa kweli yule anatumiwa na CCM."

Katiba mpya italetwa kundi moja la watu wasiokuwa malaika? Watu hao wanaweza kuwa waliwahi kutuhumiwa, kuhukumiwa au watu safi wasiokuwa na tuhuma wala hukumu dhidi Yao.

Tunaka katiba mpya vyama kuzodoana au machinga, vicoba, mama lishe, na kadhalika kuzodolewa ni kwa manufaa ya nani?

Tunataka katiba mpya kupalilia utengano wa namna yoyote ni kwa manufaa ya nani? Hatuna hata utayari wa kujifunza kwa wengine?


Penye nia pana njia.

Cc: Zawadini Paskali
Dah Mkuu fanya kuhariri kwanza halafu nirudie kusoma.
 
Amani iwe nanyi

Maandiko matakatifu yanasema, tutahukumiwa kwa kadiri ya matendo yetu. Kwani ata mambo tuyafanyayo sirini, mwenye-enzi Mungu ambaye ndiye hakimu wa haki anayaona.

Kwa muktadha huo basi, sisi wanadamu tunapata wapi mamlaka ya kuwatakatifuza viongozi wetu? Nina pata ukakasi ninaposikia kiongozi huyu au yule anafanyiwa mchakato ili atangazwe mtakatifu au yuko mbinguni.

Huu ujasiri tunautoa wapi, je sisi ni mawakala au wasaidizi wa huyo hakimu wa haki? Je hatuoni kama tuna mpangia nini cha kufanya wakati anatekeleza majukumu yake? Ni nani anayeweza kumpangia Mungu kitu cha kufanya au kushawishi namna ya kutekeleza majukumu yake.

Mungu wetu ni mwenye huruma na si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa rehema, lakini hatupaswi kumdhihaki. Utakatifu ni kufanana na Mungu, kuwa na matendo yanayo fanana na ya Mungu. Je tuna weza shuhudia hayo kwa hao wapendwa wetu?

Katika mizania ya kibinadamu viongozi wetu waliotangulia mbele ya haki hawakutufanyia haki, walishindwa kuongoza nchi yetu kiuadilifu na hawakutumia rasilimali zetu vizuri.

Kwa miaka zaidi ya hamsini ya uhuru, nchi yetu bado ni masikini na watu wetu bado ni mafukara. Walishindwa kuweka na kutetea haki, watu walidhulumiwa mali zao kwa misingi ya sera za kisiasa ( ujamaa na kujitegemea), watu walikufa kwa njaa kwa kutekeleza sera za vijiji vya ujamaa na uchumi wetu uliporomoka kwa kupigana vita isiyo na msingi na yule joker Idd Amini.

Kwa kuamua kupigana vita peke yake, maisha ya askari, watu, wanawake na watoto wasio na hatia yalipotea. Watu wengi walipoteza mali na wapendwa wao kwa sababu ya vita ambayo ingeweza kuepukika.

Ukiachilia udhalimu wa awamu hiyo, awamu ya tano ndiyo mbaya zaidi, watu walikatwa mikia, waliporwa mali zao, account zao kwenye benki zilifilisiwa na wenyewe kutishiwa vifungo, wanasiasa waliwekwa magerezani, wengine hawajulikani walipo mpaka sasa. Kiasi cha zaidi ya 4 Trillion kimepotea... kimsingi serikali iligeuka jambazi, na mpaka sasa hela za plea bargain hazijulikani zilipo.

Kwa moyo mkunjufu kabisa, nina waomba ndugu zangu, tusimdhihaki Mungu kuingiza siasa zetu za kibinadamu kwenye michakato ya Mungu. Wapo watu wanyonge, wajane na yatima wanaomlilia Mungu kwa madhila ya udhalimu wa viongozi weu, je mnataka Mungu asiwasikilize kwa sababu zenu za kisiasa za kutaka kutukuza na kutakatifuza udhalimu?

Tusimtanie Mungu.
Mkuu; Nakupongeza kwa kuandika kwa ujasiri bila kupepesa macho maoni na mtazamo wako mintaarafu Utakatifuzaji wa watu/viongozi.

Katika hili; Napenda kuchangia kama ifuatavyo:
1. Ni lazima tukubali kwamba kuna mawasiliano baina ya Binadamu na Mungu Muumba wetu. Mifano ni mingi mno e.g. ni katika mawasiliano hayo tulipewa amri 10 n.k. Mungu alikuja kwetu kwa njia ya mwanaye physically na kuongea nasi etc.etc.

2. Mungu hapangiwi ni nini cha kufanya bali huombwa ili kwa huruma na Rehema yake atujalie (atufanyie) jambo fulani tunalotamani liwepo kwa kuliweka katika mipango yake. Aidha ni katika maombi Mungu huombwa ili kwa Huruma yake abatilishe, aghairi asitende jambo au asitekeleze Hukumu ya haki juu yetu wakosaji e.g. rejea mjadala baina ya Mungu na Ibrahim (Mw. 18: 16-33)

3. Baadhi ya Watu huonekana machoni petu kama ni wema (lakini kama ulivyobainisha hapo juu -Mungu aonaye sirini..) na kwa jinsi tulivyowaona tunadhani ni watu wa kuigwa au ni watu wa mfano mwema. Hapo ndipo dhana ya Mchakato wa kutakatifuza watu inapoingia. Kutokana na mawasiliano baina ya Mungu na Binadamu; Mungu huombwa atubainishie kama mtu huyo kwa maisha yake au mwenendo wake anafaa awe ni mfano wa kuigwa i.e. aitwe Mtakatifu. Na jambo hili huchukua miaka mingi hadi likamilike.

4.Watakatifu; kwa maana ya watu walioingia mbinguni wapo ni wengi mno tena sana. Hayo majina machache sana yaliyoorodheshwa ya watakatifu na yale yanayofanyiwa mchakato ili yaingizwe katika orodha ya Watakatifu ni sample tu. Mimi sijasikia majina ya Kimaasai kati ya wanaoitwa Watakatifu.Lakini ninaamini wapo wamaasai wengi sana watakatifu lakini hawajaorodheshwa na wala hakuna mchakato unaoendelea wa kuwaingiza kwenye orodha na wala sisi hatuna sababu ya kudai kufanyiwa hilo.

5. Viongozi ni watu waliojulikana na watu wengi. Hivyo kiongozi endapo akifaulu katika mchakato huo wa kutakatifuzwa na akatangazwa rasmi kama Mtakatifu, inakuwa ni rahisi kwa watu wengi kumfuatia/kumwiga kwani alikuwa ni mtu maarufu.

6. Mwisho: Hao wanaoitwa ni Watakatifu yapo mambo maovu makubwa ambayo walitenda na ambayo kwa mtizamo wetu ni watu waliokuwa waovu kupindukia. e.g. Mtakatifu Paulo alikuwa muuaji nguli aliuua watu wengi sana na kuteketeza makanisa na alilenga wanaojiita wakristo. Lakini leo huyo ni mmojawapo wa Watakatifu. Yupo na Mt. Thomas wa Aquinas huyo unaambiwa hakuna dhambi ambayo hakuitenda. Lakini leo anaitwa ni mtakatifu. Yupo pia Mt.Monica huyo alikuwa changu doa... Orodha ni ndefu. Kwa hiyo Viongozi wetu hawa wa bongo kufanyiwa huo mchakato ni halali kabisa na hatujui ni yupi atafaulu. Wanafanyiwa mchakato watu wachache kutokana na gharama husika.

Ni hayo tu.
 
Dah Mkuu fanya kuhariri kwanza halafu nirudie kusoma.

Hiyo imehaririwa mjomba kutokea pande za Tanga huku.

Ulitaka ihaririwe kijaluo ndugu?

NIliandika mahsusi nikiwalenga kuwachoma walamba asali, wahuni na vijana wa hovyo hovyo bila kujali kokote kule waliko.

Vipi limekugusa? Kwani wewe ni yupi katika watatu hao?

Vipi limekugusa vilivyo eeh?

Kwamba:

"Dah Mkuu fanya kuhariri kwanza halafu nirudie kusoma"

Kwani wewe ni kipenyo?
 
Mkuu; Nakupongeza kwa kuandika kwa ujasiri bila kupepesa macho maoni na mtazamo wako mintaarafu Utakatifuzaji wa watu/viongozi.
Katika hili; Napenda kuchangia kama ifuatavyo:
1. Ni lazima tukubali kwamba kuna mawasiliano baina ya Binadamu na Mungu Muumba wetu. Mifano ni mingi mno e.g. ni katika mawasiliano hayo tulipewa amri 10 n.k. Mungu alikuja kwetu kwa njia ya mwanaye physically na kuongea nasi etc.etc.
2. Mungu hapangiwi ni nini cha kufanya bali huombwa ili kwa huruma na Rehema yake atujalie (atufanyie) jambo fulani tunalotamani liwepo kwa kuliweka katika mipango yake. Aidha ni katika maombi Mungu huombwa ili kwa Huruma yake abatilishe, aghairi asitende jambo au asitekeleze Hukumu ya haki juu yetu wakosaji e.g. rejea mjadala baina ya Mungu na Ibrahim (Mw. 18: 16-33)
3. Baadhi ya Watu huonekana machoni petu kama ni wema (lakini kama ulivyobainisha hapo juu -Mungu aonaye sirini..) na kwa jinsi tulivyowaona tunadhani ni watu wa kuigwa au ni watu wa mfano mwema. Hapo ndipo dhana ya Mchakato wa kutakatifuza watu inapoingia. Kutokana na mawasiliano baina ya Mungu na Binadamu; Mungu huombwa atubainishie kama mtu huyo kwa maisha yake au mwenendo wake anafaa awe ni mfano wa kuigwa i.e. aitwe Mtakatifu. Na jambo hili huchukua miaka mingi hadi likamilike.
4.Watakatifu; kwa maana ya watu walioingia mbinguni wapo ni wengi mno tena sana. Hayo majina machache sana yaliyoorodheshwa ya watakatifu na yale yanayofanyiwa mchakato ili yaingizwe katika orodha ya Watakatifu ni sample tu. Mimi sijasikia majina ya Kimaasai kati ya wanaoitwa Watakatifu.Lakini ninaamini wapo wamaasai wengi sana watakatifu lakini hawajaorodheshwa na wala hakuna mchakato unaoendelea wa kuwaingiza kwenye orodha na wala sisi hatuna sababu ya kudai kufanyiwa hilo.
5. Viongozi ni watu waliojulikana na watu wengi. Hivyo kiongozi endapo akifaulu katika mchakato huo wa kutakatifuzwa na akatangazwa rasmi kama Mtakatifu, inakuwa ni rahisi kwa watu wengi kumfuatia/kumwiga kwani alikuwa ni mtu maarufu.
6. Mwisho: Hao wanaoitwa ni Watakatifu yapo mambo maovu makubwa ambayo walitenda na ambayo kwa mtizamo wetu ni watu waliokuwa waovu kupindukia. e.g. Mtakatifu Paulo alikuwa muuaji nguli aliuua watu wengi sana na kuteketeza makanisa na alilenga wanaojiita wakristo. Lakini leo huyo ni mmojawapo wa Watakatifu. Yupo na Mt. Thomas wa Aquinas huyo unaambiwa hakuna dhambi ambayo hakuitenda. Lakini leo anaitwa ni mtakatifu. Yupo pia Mt.Monica huyo alikuwa changu doa... Orodha ni ndefu. Kwa hiyo Viongozi wetu hawa wa bongo kufanyiwa huo mchakato ni halali kabisa na hatujui ni yupi atafaulu. Wanafanyiwa mchakato watu wachache kutokana na gharama husika.
Ni hayo tu.
Uko sahihi kwa upande mmoja lakini hao wote ambao walikua waovu hapo mwanzo waliongoka, wakashika njia za Mungu na wakawa ni mfano wa matendo mazuri yampendezayo Mungu. Shida ni kwa hawa viongozi wetu, je walitubu na kuongoka na jamii ikaona uwepo wa Mungu kwao?
 
Back
Top Bottom