Zawadini
JF-Expert Member
- Feb 2, 2012
- 2,369
- 1,775
Huenda bado unajadili kwa katiba ya sasa. Nimesema haya nikiwa na maono ya katiba hiyo inayotakiwa ambayo haimpi mtu UUNGU MTU.Hata hio katiba ikiwa mpya unadhani inaweza mfunga paka kengele?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huenda bado unajadili kwa katiba ya sasa. Nimesema haya nikiwa na maono ya katiba hiyo inayotakiwa ambayo haimpi mtu UUNGU MTU.Hata hio katiba ikiwa mpya unadhani inaweza mfunga paka kengele?
Unamaana hata hawa Mama anatwanga maji kwenye kinu tu kwa sababu tabia ndiyo inayo tamalaki?Mfumo hauwezi ishinda tabia
Hapo huwezi kujua bayana na kwa uhakika kwani toba ya kweli ni baina ya anayetubu na muumba wake. Dakika moja ya mwisho inatosha sana kwa mtu kuupokea wokovu e.g. Wale majambazi wawili waliosulubiwa pamoja na Yesu msalabani -mmoja alitoa kebehi lakini yule wa pili aliomba msamaha na alisamehewa papo hapo na kupewa zawadi ya kuwa peponi....Uko sahihi kwa upande mmoja lakini hao wote ambao walikua waovu hapo mwanzo waliongoka, wakashika njia za Mungu na wakawa ni mfano wa matendo mazuri yampendezayo Mungu. Shida ni kwa hawa viongozi wetu, je walitubu na kuongoka na jamii ikaona uwepo wa Mungu kwao?
Hawezi badili kituUnamaana hata hawa Mama anatwanga maji kwenye kinu tu kwa sababu tabia ndiyo inayo tamalaki?
View attachment 2586776
View attachment 2586778
Hawezi badili kitu
St. Magufuli utuombeeAmani iwe nanyi
Maandiko matakatifu yanasema, tutahukumiwa kwa kadiri ya matendo yetu. Kwani ata mambo tuyafanyayo sirini, mwenye-enzi Mungu ambaye ndiye hakimu wa haki anayaona.
Kwa muktadha huo basi, sisi wanadamu tunapata wapi mamlaka ya kuwatakatifuza viongozi wetu? Nina pata ukakasi ninaposikia kiongozi huyu au yule anafanyiwa mchakato ili atangazwe mtakatifu au yuko mbinguni.
Huu ujasiri tunautoa wapi, je sisi ni mawakala au wasaidizi wa huyo hakimu wa haki? Je hatuoni kama tuna mpangia nini cha kufanya wakati anatekeleza majukumu yake? Ni nani anayeweza kumpangia Mungu kitu cha kufanya au kushawishi namna ya kutekeleza majukumu yake.
Mungu wetu ni mwenye huruma na si mwepesi wa hasira na ni mwingi wa rehema, lakini hatupaswi kumdhihaki. Utakatifu ni kufanana na Mungu, kuwa na matendo yanayo fanana na ya Mungu. Je tuna weza shuhudia hayo kwa hao wapendwa wetu?
Katika mizania ya kibinadamu viongozi wetu waliotangulia mbele ya haki hawakutufanyia haki, walishindwa kuongoza nchi yetu kiuadilifu na hawakutumia rasilimali zetu vizuri.
Kwa miaka zaidi ya hamsini ya uhuru, nchi yetu bado ni masikini na watu wetu bado ni mafukara. Walishindwa kuweka na kutetea haki, watu walidhulumiwa mali zao kwa misingi ya sera za kisiasa ( ujamaa na kujitegemea), watu walikufa kwa njaa kwa kutekeleza sera za vijiji vya ujamaa na uchumi wetu uliporomoka kwa kupigana vita isiyo na msingi na yule joker Idd Amini.
Kwa kuamua kupigana vita peke yake, maisha ya askari, watu, wanawake na watoto wasio na hatia yalipotea. Watu wengi walipoteza mali na wapendwa wao kwa sababu ya vita ambayo ingeweza kuepukika.
Ukiachilia udhalimu wa awamu hiyo, awamu ya tano ndiyo mbaya zaidi, watu walikatwa mikia, waliporwa mali zao, account zao kwenye benki zilifilisiwa na wenyewe kutishiwa vifungo, wanasiasa waliwekwa magerezani, wengine hawajulikani walipo mpaka sasa. Kiasi cha zaidi ya 4 Trillion kimepotea... kimsingi serikali iligeuka jambazi, na mpaka sasa hela za plea bargain hazijulikani zilipo.
Kwa moyo mkunjufu kabisa, nina waomba ndugu zangu, tusimdhihaki Mungu kuingiza siasa zetu za kibinadamu kwenye michakato ya Mungu. Wapo watu wanyonge, wajane na yatima wanaomlilia Mungu kwa madhila ya udhalimu wa viongozi weu, je mnataka Mungu asiwasikilize kwa sababu zenu za kisiasa za kutaka kutukuza na kutakatifuza udhalimu?
Tusimtanie Mungu.
Je utakatifu ni nini? Mfano wa maisha mema au kuingia mbinguni tu? Je yule jambazi aliyetubu msalabani ni mtakatifu au ni mkazi wa mbinguni?Hapo huwezi kujua bayana na kwa uhakika kwani toba ya kweli ni baina ya anayetubu na muumba wake. Dakika moja ya mwisho inatosha sana kwa mtu kuupokea wokovu e.g. Wale majambazi wawili waliosulubiwa pamoja na Yesu msalabani -mmoja alitoa kebehi lakini yule wa pili aliomba msamaha na alisamehewa papo hapo na kupewa zawadi ya kuwa peponi....
Tuendelee kumuombeaSt. Magufuli utuombee
1. Ni hali ya mtu kujitahidi kuishi maisha yanayozingatia maelekezo ya Muumba wake.1.Je utakatifu ni nini? 2.Mfano wa maisha mema au kuingia mbinguni tu? 3.Je yule jambazi aliyetubu msalabani ni mtakatifu au ni mkazi wa mbinguni?