Kwanini tunapenda kushabikia vita?

Kwanini tunapenda kushabikia vita?

Mimi siwaelewi watu wanaoshabikia vita kama vile ni Premier League. Hivi hatuelewi huko Ukraine, Gaza na sasa Lebanon watu (ikiwa pamoja na watoto) wanakufa, wanapata ulemavu na maisha yao kuharibiwa kwa kosa ambalo sio lao?

Unahisi kabisa excitement ya watu wanapozungumzia mabomu yanavyoangushwa, nyumba zinavyolipuliwa na wanajeshi wanavyovamia!

Kwa kweli inasikitisha.

Amandla!
Waulize wanajifunga mabomu kulipua wasiohusika, Kisha wanaficha silaha kwenye makazi ya watu
 
Hiki kitu huwa nawambia watu sana, ni reflection ya elimu yetu
Majority ya watanzania hawana critical thinking, wengi ni wajuaji tu, wanapenda ushabiki na kwenda na vichwa vya habari, vichwani 0

Huu ushabiki wa simba na yanga wameuweka kwenye kila kitu
Sasa iwapo Hamas wameenda wenyewe kuipiga Israel na kisha wakajinadi kuwa wanaenda kuifuta Israel kwenye uso wa dunia unadhani hiyo ni habari ndogo?

Unadhana haina athari kwenye uhusiano wa kimataifa?
 
Waulize wanajifunga mabomu kulipua wasiohusika, Kisha wanaficha silaha kwenye makazi ya watu
Ukraine wanajilipua? Hind Rajab alijipua?

Ninazungumzia kushabikia mauaji ya wananchi bila kujali ni wa upande gani. Kama binadamu hicho sio kitu cha kushangilia.

Mwisho wake tunakuwa kama Omega Mwaikambo ambae wakati wenzake wanapigana kuokoa maisha ya waliotharika na moto uliotokea katika ghorofa la Grenfell yeye alikuwa amekana kupiga picha maiti na kuzirusha kwenye social media platforms!

Unapoona maisha ya binadamu yeyote hayana thamani kabisa ndio mwanzo wa kukosa ubinadamu.

Amandla...
 
Hivi akija alien akakuuliza umuelezee sababu au chanzo cha vita ya Israel na Palestine, utamuelezea vipi ili aone binadamu ni kiumbe mwenye akili timamu?
 
Mimi siwaelewi watu wanaoshabikia vita kama vile ni Premier League. Hivi hatuelewi huko Ukraine, Gaza na sasa Lebanon watu (ikiwa pamoja na watoto) wanakufa, wanapata ulemavu na maisha yao kuharibiwa kwa kosa ambalo sio lao?

Unahisi kabisa excitement ya watu wanapozungumzia mabomu yanavyoangushwa, nyumba zinavyolipuliwa na wanajeshi wanavyovamia!

Kwa kweli inasikitisha.

Amandla!
Ni namna ya mwisho ya kushikishana adabu,baada ya manunda kufikia kiwango cha kutokuelewa katika utaratibu wa kawaida
 
Mimi siwaelewi watu wanaoshabikia vita kama vile ni Premier League. Hivi hatuelewi huko Ukraine, Gaza na sasa Lebanon watu (ikiwa pamoja na watoto) wanakufa, wanapata ulemavu na maisha yao kuharibiwa kwa kosa ambalo sio lao?

Unahisi kabisa excitement ya watu wanapozungumzia mabomu yanavyoangushwa, nyumba zinavyolipuliwa na wanajeshi wanavyovamia!

Kwa kweli inasikitisha.

Amandla!
Mi nazani vita yenye mtazamo wa Derby ndio yenye mapenzi zaidi kuliko vita zingine, mfano vita ya Urusi na Ukraine sizani kama Kuna ushabiki kama hi inayoonekana ni Derby.
 
Back
Top Bottom