Kwanini Tundu Lissu hakutangaza nia mapema ya kugombea uenyekiti wa Chama taifa?

Decree Holder

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2015
Posts
2,559
Reaction score
3,745
Inawezekana kabisa TAL aliamua kugombea uenyekiti wa Chama taifa mapema zaidi lakini hakutangaza kutokana na historia ndani ya chadema. Historia inaonesha viongozi wote ndani ya chadema walioonesha kuutaka uenyekiti mapema waliundiwa zengwe na kupewa kesi za usaliti kuwazuia kugombea uenyekiti.

Kwa mfano kilichompata Chacha Wangwe kwani alionesha nia mapema sana mwaka 2008 takribani mwaka mzima kabla ya uchaguzi wenyewe. Aliundiwa zengwe akavuliwa uongozi na kuwa labeled msaliti.

Mwingine ni Zitto Kabwe alionesha nia mapema sana akawa labeled msaliti akavuliwa uanachama kabla hata hajagombea.

Kwa kutambua historia hiyo Lissu aliamua kuficha nia yake ya kuutaka uenyekiti wa Chadema na badala yake akatangaza na kutia nia nafasi ya makamu mwenyekiti wa Chama mapema zaidi. Hata alipoulizwa kuhusu uenyekiti alikataa katakata na kuapa kwamba asingempinga mbowe kwenye uenyekiti kwani amemsaidia sana.

Mbowe akaingia katika mtego na kuamini kuwa Lissu atatetea nafasi ya makamu mwenyekiti wa Chama taifa na siyo kugombea uenyekiti wa Chadema.

Ni Lissu peke yake Kati ya wanasiasa waandamizi ndani ya chadema aliyefanikiwa kuchukua fomu na kurudisha tena katika namna ambayo ni ya kushtukiza.

Katika hili Lissu amecheza kama Pele.
 
Acha kutoka povu, Box litaamua ni Lissu ama Mbowe kuongoza CDM kwa miaka mitano.
Wajumbe 1200 ndiyo watachagua nani mwenyekiti mpya wa chama chao.
 
Ni Lissu peke yake Kati ya wanasiasa waandamizi ndani ya chadema aliyefanikiwa kuchukua fomu na kurudisha tena katika namna ambayo ni ya kushtukiza
Mkuu, hapo unataka usemeje kwa mfano? Maana ukizingatia alivaa almost full military gear, mtu anaweza kuchanganyikiwa akiunganisha hizo dotsi.
 
Lissu ni Judgment Debtor
 
ni kwasababu hana maono, hayuko huru kifikra na kiuchumi, mpaka wanaomfadhili wamuelekeze cha kufanya ndipo aamue 🐒
 
Mwambieni huyo Lissu wenu aache kupoteza muda kwa Don.
 
Ni kweli Lissu hakuwa kabisa na nia wala mpango kugombea uenyekiti, nia yake ni kutetea umakamo.

Baada ya kutofautiana na Mbowe, Mzee baba akaamua kumflush TL out of Chadema kwa nafasi yake kumpa Wenje, ndipo Lissu akaamua kama mbway na iwe mbway, mmenianza, mimi namaliza!, akaamua kumvaa Mbowe!.
Katika hili Lissu amecheza kama Pele.
Ni kweli TL amecheza kama Pele ila anajua jinsi wanachama wao walivyo manyumbu, hivyo hawezi kumshinda Mbowe ila atawasumbua, na tena Chadema wawe makini sana, wakileta ujinga wowote, tarehe 21 January hakuna Uchaguzi.

P
 
Labda wanataka kumpa Kibatala kazi ya ziada huko mahakamani maana amekaa loose muda mrefu sana. sarakasi za mahakamani wote wanaziweza huko ndiko kitakacho elekea baada ya tarehe 21/01/2025
 
Hii counter attack aliyofanya Lissu imemstua sana Sultan na nyumbu wake,mayowe kila corner.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…