Kwanini tutumie akiba ya fedha za kigeni kununulia umeme nje na hali tunao humu ndani?

Kwanini tutumie akiba ya fedha za kigeni kununulia umeme nje na hali tunao humu ndani?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Huwa nazungumza sana akiba ya pesa za kigeni sababu ni kitu muhimu sana kwa nchi. Nchi inatakiwa kutumia kwa busara sana pesa za kigeni. Hizo ndizo tunaagizia mafuta, madawa, kulipa madeni na mahitaji mengine muhimu. Ukisikia serikali haina pesa ujue hasa inamaanisha haina hizo reserve currencies.

Tukienda kununua umeme nje hatutalipa kwa pesa zetu. Tutalipa kwa reserve currencies tulizopata kwa shida.

Hizi pesa zinapatikana kwa shida sana. Mpaka tuuze maparachichi, korosho, chai, kahawa, pamba, dhahabu na watalii waje ndiyo tuzipate.

Sasa kama tuna umeme humu ndani wa kutosha na ziada kwa nini tutumie akiba ya maana kuagiza umeme nje? Sababu ya mikoa ya kaskazini kuwa mbali na vyanzo vya uzalishaji wa umeme haiingii akilini kabisa. Hii ishu kama ipo in motion tuiangalie upya.
 
Unadhani umasikini wa hii nchi umesababishwa na wazungu, ni mchanganyiko wa mambo ya kipuzi kama haya ndo tumejikuta tupo hapa Leo.
Hata mwezi haujaisha walitangaza tuna umeme mwingi na tunataka kuuza nje, Jana wanatangaza wanataka kununua umeme nje.
 
Ethiopia umeme wao ni wa bei nafuu kupita huu wa kwetu
Wetu tutauziana kwa Tsh. Wa Ethiopia tutaenda kununua kwa dola. Hilo pekee lingekuwa sababu kubwa kabisa ya kutonunua umeme nje, isipokuwa kama tunaozalisha hautoshi. Na hata kama ni gharama, weka hapa gharama ya kuzalisha unit moja Ethiopia na kuisafirisha hadi Arusha. Na pia weka gharama ya kuzalisha Unit moja Rufiji na kuisafirisha hadi Arusha. Si kusema tu huu bei kuliko huu.
 
Unashangaa hilo tu? Haujiulizi kwa nini tunatumia akiba yetu ya fedha za kigeni kununua mafuta nje ya nchi wakati hapo Lindi na Mtwara tuna gesi nyingi hadi hatujui tutumie kwenye nini?

CCM ni janga la taifa na laana!
 
Gharama ya kutengeneza grid system kwenda kaskazini ndio itamaliza kabisa na kukopa juu bora kulipa opretions bill kuliko capital costs wamesema!
 
Gharama ya kutengeneza grid system kwenda kaskazini ndio itamaliza kabisa na kukopa juu bora kulipa opretions bill kuliko capital costs wamesema!

Hizo ni siasa tu.

Ukinunua maana yake huna incentive ya kutumia chako ambacho unacho, kitu ambacho ni uendawazimu.

Tuliacha mradi wa gesi ambayo tulishatumia mahela kibao ya kutandaza mabomba tukaenda kujenga bwawa la Nyerere. Pesa ikapotea.

Tumejenga bwawa la Nyerere, umeme upo wa kutosha, hatuusambazi, sasa tunawaza kununua!

Sasa ukinunua, ule umeme wa Bwawa la Nyerere utaupeleka wapi?- Ukisema uuze nje, je utatumia miundo mbinu gani ya kuuza nje ambayo unashindwa kuijenga kuupeleka huo umeme ktk mikoa ya kaskazini?

Je hao wanaokuuzia umeme ktk mikoa ya kaskazini wao waliwezaje kuusafirisha huo umeme kutoka ktk nchi zao kuuleta kwetu, halafu sisis tushindwe kuusafirisha wa kwetu kuupeleka kwetu?

Inaelekea hawa watawala wetu wanafanya mambo si kwanlong plan, bali maamuzi ya asubuhiasubuhi, anaamka na hili na kile analigeuza kuwa sera ya nchi!
 
Uzoefu unaonyesha kila serikali ya ccm huwa inapiga deal kubwa kwenye nishati huenda hii pia ni zile deals za kawaida, mara symbion, aggreko, IPTL, Songas, mara gas Mtwara so huu unaweza kuwa ni ukurasa mpya wa fweza za kuhonga kuandaa uchafuzi. Kumbuka mara ya mwisho kulamba Bot ilikua ni Kagoda so huenda hapaingiliki au nyimbo hazipangiki sawasawa,

Yetu macho sisi akina pangu pakavu, wapita njia! Labda watamkumbuka mwashamba zamu hii, tusibiri na tuone, wakati ukuta!
 
Huwa nazungumza sana akiba ya pesa za kigeni sababu ni kitu muhimu sana kwa nchi. Nchi inatakiwa kutumia kwa busara sana pesa za kigeni. Hizo ndizo tunaagizia mafuta, madawa, kulipa madeni na mahitaji mengine muhimu. Ukisikia serikali haina pesa ujue hasa inamaanisha haina hizo reserve currencies.

Tukienda kununua umeme nje hatutalipa kwa pesa zetu. Tutalipa kwa reserve currencies tulizopata kwa shida.

Hizi pesa zinapatikana kwa shida sana. Mpaka tuuze maparachichi, korosho, chai, kahawa, pamba, dhahabu na watalii waje ndiyo tuzipate.

Sasa kama tuna umeme humu ndani wa kutosha na ziada kwa nini tutumie akiba ya maana kuagiza umeme nje? Sababu ya mikoa ya kaskazini kuwa mbali na vyanzo vya uzalishaji wa umeme haiingii akilini kabisa. Hii ishu kama ipo in motion tuiangalie upya.
Tuiangalie upya, uiangalie na Nani? Jaribu kuangalia tuone Kama utaweza.
 
Sasa kama tuna umeme humu ndani wa kutosha na ziada kwa nini tutumie akiba ya maana kuagiza umeme nje? Sababu ya mikoa ya kaskazini kuwa mbali na vyanzo vya uzalishaji wa umeme haiingii akilini kabisa. Hii ishu kama ipo in motion tuiangalie upya.
Binafsi naingiwa mashaka na hili jambo
Kutoka Chalinze hadi Tanga, Moshi na Arusha ni pafupi sana kuliko kutoka Ethiopia hadi Arusha;
  1. Huo umeme wa kutoka Ethiopia ni kiasi gani tofauti na ule wa kutoka Stiglers?
  2. Kinachofanya gharama kuwa kubwa kusafirisha umeme katika umbali wa Km 500 ni kitu gani?
  3. Kinachofanya gharama ya umeme kutoka Ethiopia Km 2000+ kuwa nafuu ni kitu gani?
  4. Je mabwawa ya Nyumba ya Mungu Mwanga, Hale na Pangani Tanga yana shida gani?
 
CCM wanatamba kwamba wamefua umeme wa kumwaga afu nyuma ya mlango wanakwenda kununua umeme nje ya nchi.
 
Wakati wa gesi ya Mtwala tuliambiwa kukatika umeme itakuwa history na bei itakuwa chee kiasi kupikia mkaa itakuwa ni anasa.

Ujio wa bwawa jipya ndio ilikuwa balaa, yaani tuliambiwa tutakuwa na ziada ya kuuza nje na watu wa masoko wako busy kutafuta wateja, kwani megawatts zitakuwa nyingi sana.

Sasa ahadi zote hizi zimefeli kabla jogoo hajawika hata mara Moja akiwika mara ya tatu nchi itakuwa tayari ni koloni la mtu.
 
Back
Top Bottom