Kwanini Ufaransa, Canada, Ujerumani zipo NATO?

akili zako fupi mwenyewe,kuchangia kwa lugha nzuri kama wenzakn umeshindwa?? Kama utaki ungepita kimya kimya tu.
 
Kwa kifupi hapa naona tatizo ni hili dude mrusi.
Urusi alituma maombi kujiunga NATO akakataliwa, NATO si hawasemi wapo dhidi ya nani basi Russia ikawadhihaki kwa kutaka uanachama. Tatizo la Russia huwa ana ego na hujikuta ana mamlaka juu ya majirani. Russia iliitwa na Marekani iwe inashiriki kwenye mazoezi ya pamoja ya majeshi ya Ulaya ikaweka masharti magumu. Mwaka 2003 washirika walipoenda Iraq ikaonekana kuna majeshi yana mafunzo mabovu hasa Ukraine na Poland. Marekani ikaanzisha program ya kufundisha majeshi ya Ulaya yenye changamoto, wakafanya na exchange program kutembelea training facilities, weapons storage sites na mambo ya kijeshi yasiyo ya siri. Kwenye programu hizo Urusi ilikubali ziara za kutembeleana na makamanda wake wakajionea standards za majeshi kadhaa mengine ila haikutaka training ya pamoja, nayo ilitembelewa na wakashauriana vitu kadhaa ambavyo kimojawapo kilitekelezwa ni ujenzi wa training ground mpya ya Mulino. Rheinmetall kampuni ya Ujerumani ndio ilipewa tenda ikaweka NATO standards.

Russia wala hachukiwi, ila the way anaishi na majirani ndio wasiwasi wao. Kuna uwezekano Russia ikaingia mgogoro na Kazakhstan jirani wa Kusini, kuna uwezekano China na Russia warudie kugombania mipaka ila hakuna uwezekanowa Marekani kupigana na Canada.
Urusi yumo kwenye BRICS
BRICS sio ushirika wa kijeshi ni wa kiuchumi, kama ambavyo NATO ni wa kijeshi tu. Wala usitarajie South Africa itaziacha Marekani, Ufaransa, UK, Canada eti iende kwa China na Russia.

Na usitarajie Brazil iikumbatie Russia iiache Marekani, kasome ushirikiano wa Brazil kwenye silaha na Westerns companies. Tafuta hata kampuni yao pendwa ya Embraer inapewa hata tenda za silaha na wazungu ila sio Warusi, na ina license kibao za wazungu.

Wala usitarajie India kujiweka kwa Urusi pekee. Tazama weapons sales za tangu Trump anaondoka madarakani mpaka sasa, za Urusi kadhaa zimefutwa na za Marekani zimetekelezwa.

China tu ndio anabaki kwenye BRICS akiwa na uwezo wa kufanya alliance ya kijeshi na Russia. Ila naye kashauriwa asitoe msaada kwa Urusi kwenye vita ya Ukraine akakubali. Russia leo hii anaenda kwa Iran kuomba msaada wa drones wakati China ina drones za kila aina
 
Unafikiria urusi anaweza kubali
Myusa ni mjanja mjanja sana inabidi kuwa nae makini sana hakuna kitu anakifanya kwa hasara na urusi nadhani anamjua vizuri ndio maana anamkwepa ukiona myusa anakudharau ujue huna kitu lkn lkn kama anakufuatafuata ujue kuna kitu anakitafuta na ana mbinu nyingi za kuingia.
 
Mataifa ya ulaya yanamuogopa sana urusi.... urusi ni kama dude linalotisha mno....sio yakuichukulia poa hata kidogo
Wanaogopa sababu kiongozi wao ni sawa na kichaa tu ambaye hatabiriki
 
Sasa mkuu T14 armata ukizingatia kuwa ujerumani alikuwa na biashara binafsi na urusi ,ni kwa nini akuamua kuwa neutral ili asimamie maslahi yake??
 
Wamekubali kushikwa makalio na Marekani acha waendelee kushikwa wakitiwa ndole ndo wataamka
 
Unafikiri Putini akiichukua kiurahisi Ukraine ataishia hapo tu??
Wajerumani wanafikiria miaka 20 na zaidi mbele yako unayaweza maslahi ya biashara tu.
Sasa mkuu T14 armata ukizingatia kuwa ujerumani alikuwa na biashara binafsi na urusi ,ni kwa nini akuamua kuwa neutral ili asimamie maslahi yake??
 
Ujerumani ndo nchi inayoongoza kuwa na military base nyingi za marekani na wanajeshi wengi wa marekani
 
Unafikiri Putini akiichukua kiurahisi Ukraine ataishia hapo tu??
Wajerumani wanafikiria miaka 20 na zaidi mbele yako unayaweza maslahi ya biashara tu.
Putin angeachiwa kuchukua Ukraine kirahis asingehishia hapo angeamin Poland na mwisho wa siku angesema ujerumani mashariki irudi mikononi mwake

Lengo la marekani na urusi ni kujaza vibaraka wao nchi za ulaya Ila urusi anakumbatia udikteta na hii ni ku-tokea kipindi cha ussr alikuambatia madictactor hata sahivi sera za urussi ni kukumbatia madikteta, huku marekani akikuambia mfumo wa democrasia ndo maana inakua rahis kwa nchi za ulaya ambazo nyingi zimestaarabika kumkubali marekani kuliko urussi, japokua marekani naye ana mapungufu yake

Hata project za urusi za gesi ni ili baadae kuja kuzitumia kama fimbo ya kuwaadhibu ulaya, lengo la urussi ni kufanya ulaya kuwa colonial lake kwa kujaza marais vibaraka ulaya nzima
 
Vilaza wa Africa hawaelewei hili wanapoona EU imekomaa na Russia kwenye uvamizi wake wa Ukraine.
 
Kupitia vita hii, Russia ajitafakar mno juu ya uswahiba wake na China.
 
Hili la vibaraka nadhani western ndio wanaongoza duniani kuwa na vibaraka weng na hasa afrika ndio maana afrika tunaishi kama digIdigi.
 
Bro uwa nakushangaa na uwa nawashaanga jamaa amendika hoja tupu wewe unakimbilia matusi Sasa nani anakili fupi kama si wewe ndo unaakili fupi?
 
Kupitia vita hii, Russia ajitafakar mno juu ya uswahiba wake na China.
Bado ni marafiki wazuri sana. Si lazima ujiingize matatani kwa maslahi ya rafiki yako, China ina sera na malengo yake wala haijajipanga kupigana karne hii. Ukorofi wa China tutauona kuanzia 2030s.

China hawezi unga mkono vita ya Ukraine wakati naye ana Taiwan pale wala hajaanzisha vita. Anaona ni busara kutotumia nguvu kwa Taiwan itakuwaje aone ni sawa kutumia nguvu zake kwa Ukraine
 
Bro uwa nakushangaa na uwa nawashaanga jamaa amendika hoja tupu wewe unakimbilia matusi Sasa nani anakili fupi kama si wewe ndo unaakili fupi?
narudia tena mataifa ya ulaya hayaburuzwi , ni inshu ya maslai + Usalama ndo inawafanya kuwa upande mmoja na USA , nchi za ulaya sio nchi za afrika au nchi asia , na mgogoro wa urusi na west , ulikuepo hata kabla ya uwepo wa marekani duniani , ni kituko kusema ufaransa au ujeruman wanaburuzwa kuwepo ndan NATO , eti wao hawatak
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…