Kwanini unapaswa kununua bond au Hati fungani ya NMB?

Kwanini unapaswa kununua bond au Hati fungani ya NMB?

Kitabu cha "Cashflow quadrant" cha Robert Kiyosaki kinatuhusu sana hapa.

Jamaa anayaponda sana haya mabenki. Tabia ya mabenki ni kukopesha kwa riba kubwa lakini yenyewe yanauza hati fungani zao kwa riba ndogo sana. Lengo lao ni kupata faida kupitia hela ambayo hawajaifanyia kazi. Kwa kifupi, taasisi za kifedha si rafiki wa watu ila wapo kifaida.

Sasa hivi ni kweli mtu uweke mil 2 kwa mwaka halafu eti upewe 260,000 kama faida. Hivi hii inaingia akilini kweli?

Kutatua tatizo, Kiyosaki anashauri watu wawekeze muda wao kwenye Financial intelligence. Kila mtu akiwa na uelewa wa pesa atakuwa na jicho la tatu na kuona fursa zinazomzunguka na kuzifanyia
kazi kupata faida.

Fursa zipo nyingi sana. Tatizo ni kukosa macho ya kuziona. Kwa mfano mmoja tu: Kununua nafaka kipindi cha mavuno na kuziuza kipindi cha masika. Debe la mahindi kipindi cha mavuno maeneo ya Gairo huwa ni shs 7000. Lakini kipindi cha masika debe hilohilo hufika hadi shs 14,000. Kwahiyo ukiwa na mil 2 unanununua madebe 300. Baada ya miezi 5-6 unakuja kuyauza kwa shs 4000000. Ukitoa gharama za dawa na usafiri unabakiwa na 3.5 m. Unaweza kuona hapo profit margin.

Na huo ni mfano mmoja tu lakini kuna mifano lukuki ya aina hii. Tatizo kubwa tulilo nalo ni kutokuweka kipaumbele kwenye kuwekeza kwenye elimu ya fedha na biashara. Matokeo yake wanakuja hao watu wa NMB na kujifanya wanatupenda sana kiasi cha kutuhifadhia HELA ZETU ili zizae. Hawana upendo mkubwa kiasi hicho.

K
 
Inashawishi na inamvuto kuliko uwekezaji wa fixed account
 
Kitabu cha "Cashflow quadrant" cha Robert Kiyosaki kinatuhusu sana hapa.

Jamaa anayaponda sana haya mabenki. Tabia ya mabenki ni kukopesha kwa riba kubwa lakini yenyewe yanauza hati fungani zao kwa riba ndogo sana. Lengo lao ni kupata faida kupitia hela ambayo hawajaifanyia kazi. Kwa kifupi, taasisi za kifedha si rafiki wa watu ila wapo kifaida.

Sasa hivi ni kweli mtu uweke mil 2 kwa mwaka halafu eti upewe 260,000 kama faida. Hivi hii inaingia akilini kweli?

Kutatua tatizo, Kiyosaki anashauri watu wawekeze muda wao kwenye Financial intelligence. Kila mtu akiwa na uelewa wa pesa atakuwa na jicho la tatu na kuona fursa zinazomzunguka na kuzifanyia
kazi kupata faida.

Fursa zipo nyingi sana. Tatizo ni kukosa macho ya kuziona. Kwa mfano mmoja tu: Kununua nafaka kipindi cha mavuno na kuziuza kipindi cha masika. Debe la mahindi kipindi cha mavuno maeneo ya Gairo huwa ni shs 7000. Lakini kipindi cha masika debe hilohilo hufika hadi shs 14,000. Kwahiyo ukiwa na mil 2 unanununua madebe 300. Baada ya miezi 5-6 unakuja kuyauza kwa shs 4000000. Ukitoa gharama za dawa na usafiri unabakiwa na 3.5 m. Unaweza kuona hapo profit margin.

Na huo ni mfano mmoja tu lakini kuna mifano lukuki ya aina hii. Tatizo kubwa tulilo nalo ni kutokuweka kipaumbele kwenye kuwekeza kwenye elimu ya fedha na biashara. Matokeo yake wanakuja hao watu wa NMB na kujifanya wanatupenda sana kiasi cha kutuhifadhia HELA ZETU ili zizae. Hawana upendo mkubwa kiasi hicho.

K

Unaweza kuwa sawa ila sio sawa pia.

Kila biashara ina changamoto zake na kila mtu anaona kile anachoona.

Kuna watu wameamua kujikita kwenye biashara za financial markets, humwambii kitu kuhusu hayo mambo ya kilimo.

Na sio rahisi kumshauri mtu aweke bilion 10 zake kwenye mambo ya kilimo.

Za kuambiwa changanya na zako, sio kila wakati Robert Kayosaki yupo sawa.
 
Unaweza kuwa sawa ila sio sawa pia.

Kila biashara ina changamoto zake na kila mtu anaona kile anachoona.

Kuna watu wameamua kujikita kwenye biashara za financial markets, humwambii kitu kuhusu hayo mambo ya kilimo.

Na sio rahisi kumshauri mtu aweke bilion 10 zake kwenye mambo ya kilimo.

Za kuambiwa changanya na zako, sio kila wakati Robert Kayosaki yupo sawa.
Issue siyo "za kuambiwa changanya". Issue ni kuwa na uelewa wa kuona fursa zipi zinatengeneza pesa kwa haraka na in a more secure way.

Robert Kiyosaki hajashauri chochote kilicho tofauti na kile tunachokielewa wewe na mimi. Anashauri watu wawekeze kwenye Financial Intelligence ili wapanue uelewa wao wa kujua fursa na kuziexploit. Wewe huamini juu ya elimu.

Hao unaosema huwaambii chochote juu ya hatifungani wanaangukia kwenye kundi la watu wenye little knowledge juu ya Finance. Wanachoamini ni kuwa biashara zote ni risky. Kwahiyo wako tayari kuvumilia miaka 3 ili apate 3.9 m out of 10. Hivi hii akili au matope?

Kama hayo mahati fungani yenu yanalipa, naomba mfano wa tajiri mmoja tu ambaye ametajirika kwasabu ya hizo hatifungani.
 
Issue siyo "za kuambiwa changanya". Issue ni kuwa na uelewa wa kuona fursa zipi zinatengeneza pesa kwa haraka na in a more secure way.

Robert Kiyosaki hajashauri chochote kilicho tofauti na kile tunachokielewa wewe na mimi. Anashauri watu wawekeze kwenye Financial Intelligence ili wapanue uelewa wao wa kujua fursa na kuziexploit. Wewe huamini juu ya elimu.

Hao unaosema huwaambii chochote juu ya hatifungani wanaangukia kwenye kundi la watu wenye little knowledge juu ya Finance. Wanachoamini ni kuwa biashara zote ni risky. Kwahiyo wako tayari kuvumilia miaka 3 ili apate 3.9 m out of 10. Hivi hii akili au matope?

Kama hayo mahati fungani yenu yanalipa, naomba mfano wa tajiri mmoja tu ambaye ametajirika kwasabu ya hizo hatifungani.

Unajua hati fungani ni nini hasa? Au unazijua tu hizi za NMB? Unajua zinavyonunuliwa? Unajua kwanini mabenki wanapigana vikumbo kununua hati fungani za serikali? Kuna watu wengi sana wamekuwa mabilionea kwa kununua hati fungani. Na hata nikikuambia huwezi kuwajua.

Kwa Tanzania;

1. Reginald Mengi, sio kwamba ananunua hati fungani za Tanzania tu, nchi nyingi nje ya Tanzania.

2. Ali Mufuruki,

3. Wengine hata nikikutajia huwezi kuwafahamu.
 
Yaani nyie riba mnachukua asilimia 22 kwa mwaka halafu sisi mnatupa 13 kwa mwaka..kweli!!!!!
 
Hat I TE="Bavaria, post: 16249485, member: 295384"]Unajua hati fungani ni nini hasa? Au unazijua tu hizi za NMB? Unajua zinavyonunuliwa? Unajua kwanini mabenki wanapigana vikumbo kununua hati fungani za serikali? Kuna watu wengi sana wamekuwa mabilionea kwa kununua hati fungani. Na hata nikikuambia huwezi kuwajua.

Kwa Tanzania;

1. Reginald Mengi, sio kwamba ananunua hati fungani za Tanzania tu, nchi nyingi nje ya Tanzania.

2. Ali Mufuruki,

3. Wengine hata nikikutajia huwezi kuwafahamu.[/QUOTE]
Hati fungani hizihizi za 13%
 
Unajua maaana ya Passive Income???

Muuza vitumbua ametengeneza zaid ya laki tatu ndiyo is it passive income??
Milioni kuzalisha laki tatu kwa mwaka ni mrejesho mdogo dana kuliko muuza jaranga na biscut mwenye mtaji wa laki moja na kuzalisha faida ya laki tatu kwa mwaka. nimesema for big investor its payable but not kwa mwenye hela ya mawazo . Hela kuanzi milion 10 na kuendelea mimi suna tatizo.
 
Unajua hati fungani ni nini hasa? Au unazijua tu hizi za NMB? Unajua zinavyonunuliwa? Unajua kwanini mabenki wanapigana vikumbo kununua hati fungani za serikali? Kuna watu wengi sana wamekuwa mabilionea kwa kununua hati fungani. Na hata nikikuambia huwezi kuwajua.

Kwa Tanzania;

1. Reginald Mengi, sio kwamba ananunua hati fungani za Tanzania tu, nchi nyingi nje ya Tanzania.

2. Ali Mufuruki,

3. Wengine hata nikikutajia huwezi kuwafahamu.
Hizihizi za 13%
 
[QUOTEwezi abo, post: 16249496, member: 49070"]Yaani nyie riba mnachukua asilimia 22 kwa mwaka halafu sisi mnatupa 13 kwa mwaka..kweli!!!!![/QUOTE]
Jamaa wezi sana
 
Kitabu cha "Cashflow quadrant" cha Robert Kiyosaki kinatuhusu sana hapa.

Jamaa anayaponda sana haya mabenki. Tabia ya mabenki ni kukopesha kwa riba kubwa lakini yenyewe yanauza hati fungani zao kwa riba ndogo sana. Lengo lao ni kupata faida kupitia hela ambayo hawajaifanyia kazi. Kwa kifupi, taasisi za kifedha si rafiki wa watu ila wapo kifaida.

Sasa hivi ni kweli mtu uweke mil 2 kwa mwaka halafu eti upewe 260,000 kama faida. Hivi hii inaingia akilini kweli?

Kutatua tatizo, Kiyosaki anashauri watu wawekeze muda wao kwenye Financial intelligence. Kila mtu akiwa na uelewa wa pesa atakuwa na jicho la tatu na kuona fursa zinazomzunguka na kuzifanyia
kazi kupata faida.

Fursa zipo nyingi sana. Tatizo ni kukosa macho ya kuziona. Kwa mfano mmoja tu: Kununua nafaka kipindi cha mavuno na kuziuza kipindi cha masika. Debe la mahindi kipindi cha mavuno maeneo ya Gairo huwa ni shs 7000. Lakini kipindi cha masika debe hilohilo hufika hadi shs 14,000. Kwahiyo ukiwa na mil 2 unanununua madebe 300. Baada ya miezi 5-6 unakuja kuyauza kwa shs 4000000. Ukitoa gharama za dawa na usafiri unabakiwa na 3.5 m. Unaweza kuona hapo profit margin.

Na huo ni mfano mmoja tu lakini kuna mifano lukuki ya aina hii. Tatizo kubwa tulilo nalo ni kutokuweka kipaumbele kwenye kuwekeza kwenye elimu ya fedha na biashara. Matokeo yake wanakuja hao watu wa NMB na kujifanya wanatupenda sana kiasi cha kutuhifadhia HELA ZETU ili zizae. Hawana upendo mkubwa kiasi hicho.

K
Ukweli mtupu mkuu, ndiyo namalizia kusoma cashflow quadrant yani ni kama nimezaliwa upya vile kiakili.
 
Mimi nikiwakopesha nyie nmb sh 1,000,000 kwa miaka 3 mnanipa riba ya sh 390,000 kabla ya kodi. Vipi na nyie mnaweza kunikopesha hiyo sh 1,000,000 kwa miaka 3 nikawapa hiyo riba ya sh 390,000?
Mabepari wanasema ukiwekeza kwao ni low risk na wao wakiwekeza kwako ni high risk kwa hyo the lower the risk is,the lower the returns and the opposite is correct.
Tugeuze hio iwe vicevesa,ninyi mtupe wateja then kwa mwaka turudishe kwa hio riba ya 13% kama mtakubali
 
Chukua hiyo 1M nenda shamba lima kwa kawaida kabisa hata nyanya kwa miezi minne tu utakuwa na faida zaidi ya hiyo.
 
Ukweli mtupu mkuu, ndiyo namalizia kusoma cashflow quadrant yani ni kama nimezaliwa upya vile kiakili.

Waliosoma vitabu vya Kayosaki hawajawahi kuwa mamilionea achilia mbali kufanikiwa.

Utaishia kuwa inspired tu.

Baada ya miaka mitano ujipime kama umetimiza vingapi kupitia stories za Kayosaki.
 
Waliosoma vitabu vya Kayosaki hawajawahi kuwa mamilionea achilia mbali kufanikiwa.

Utaishia kuwa inspired tu.

Baada ya miaka mitano ujipime kama umetimiza vingapi kupitia stories za Kayosaki.
Mbona unajichanganya? Hicho kitabu kinahamasisha watu wawe na Financial Intelligence ili waweze kufikiri independently. HAKITOI UTAJIRI. Wewe unaanzisha argument tofauti kabisa.

Haya tuambie watu waliosoma vitabu gani ndiyo waliwahi kuwa matajiri?

Utajiri siyo kusoma vitabu, bali uwezo wa kuapply principles za vitabu in the practical life. Kuna watu hawasomi na ni matajiri wa kutupwa kwasababu walijifunza kanuni za kutengeneza utajiri kupitia njia tofauti na kusoma vitabu.

Hizo hati fungani zenu hata kwa mtu ambaye hajui kusoma ni wizi mtupu. Huwezi ukanishawishi niweke 2 millions halafu nipate laki 2 kama faida. WIZI wa hali ya juu.
 
Uwekezaji katika Bond au Hati fungani ni aina ya uwekezaji ambao imekuwepo kwa muda mrefu sana katika nchi mbalimbali,

Hata hivyo hapa nchini kwetu dhana hii ya uwekezaji bado inaonekana kwa ni ngeni miongoni mwa watu wengi

Bondi au Hati fungani ni nini?

Ni uwekezaji ambapo mwekezaji anaikopesha serikali au kampuni, na serikali hiyo au kampuni inaahidi kumlipa mwekezaji huyo baada ya hatifungani hiyo kukomaa,

Kwa kawaida faida inayoambatana na uwekezaji katika bond hugawiwa kila baada ya miezi 6.

Benki ya NMB ambayo ndiyo the most profitable bank, na ndiyo benki iliyo sambaa zaidi nchini Tanzania kwa sasa imetangaza uuzaji wa hatifungani yake, ambapo imeanza kuuzwa kutoka tarehe 10 May na itauzwa hadi tarehe 8 June 2016, kupitia madalali 10 wa soko la Hisa la Dar es salaam Mfano Arch Financials & Investments Advisory Limited wanaopatikana katika jengo la NIC life house lililopo mtaa wa sokoine posta jijini Dar es salaam, (Tel:+25522732922396,Mob: 0784952814) au Kupitia Tawi lolote la NMB lililo karibu nawe

Kwa Kiasi kidogo tu cha uwekezaji cha shillingi laki tano (500,000) unapata faida ya asilimia 13% kwa mwaka kwa muda wa miaka mitatu ambapo faida hii inakuwa inalipwa mara mbili kwa mwaka, bila kusahau kuwa bondi itakapo komaa "mature" NMB itakulipa pesa yako yote uliyokuwa umewekeza awali

Hati fungani hii ya NMB walengwa wakuu ni wawekezaji wadogo na wakati, japo hata wakubwa hawajazuiwa na ndiyo maana kiwango cha chini cha uwekezaji ni Tsh 500,000/= Tu na kuendelea, tofauti na Bondi nyingine za makampuni zilizo wahi tokea hapa Tanzania

Chukulia kama umewekeza Shillingi 1,000,000 kwa riba ya 13% kwa mwaka, hivi ndivo itakavyokuwa

1.Interest=Principal*Rate* Time

=1,000,000*13/100*1year

=Shillingi 130,000

2.Lakini interest hii inalipwa mara mbili kwa mwaka hivyo malipo ya mkupuo wa kwanza yatakuwa ni TZS130,000/2 =TZS 65,000/=

3.Kila mkupuo wa malipo unatozwa kodi ya zuio ya 10%

=65,000-(65000*10%)

=65,000-6,500

=TZS 58,500

Hivyo kufikia Disemba 2016(baada ya miezi 6) utapokea Shillingi 58,500

4.Baada ya miaka 3, uwekezaji wako katika hatifungani hii utakuwa umekuingizia Shillingi 351,000 (58,500*6) kutoka katika uwekezaji wako wa Shillingi 1000,000. Shullingi 1M yako itakwa imekuwa hadi kufikia shillingi 1,351,000 pasipo wewe kufanya chochote, umeingiza pesa hizi ukiwa umekaa tu nyumbani au upo kwenye shughuli zako nyingine.

Isitoshe endapo utapata dharura, kabla miaka mitatu haija isha,na ukahitaji hizi pesa zako bado una nafasi ya kupata pesa zako ulizo wekeza , ambapo utaweza ku uza hatifungani hii katika soko la Hisa la Dar es salaam, kupitia madalali wake

Source : TzInsight
Asante kwa elimu, nilikuwa sijui hii kitu!
Najiuliza, sasa kama mimi ni mjasilia mali, nikiweka 1,000,000 Ths katika kununua maajisay, na kuuza siwezi nikapata hiyo faida hiyo mara kumi kwa mwaka? Nauliza tu nikijaribu kuweka hati fungani na kuziwekeza katika biashara ndogo ndogo!
 
Chukua hiyo 1M nenda shamba lima kwa kawaida kabisa hata nyanya kwa miezi minne tu utakuwa na faida zaidi ya hiyo.
Kwa kupanga hivi ni rahisi mno lakini ukija kwenye implementation ndio kasheshe huanzia hapo
Gharama za kuanzia kuandaa shamba kununua mbegu kupanda palizi madawa maji nk nk
Upatikanaji wa soko unaweza kutoka shamba unapeleka mzigo wako gari ikapata hitilafu njiani mzigo ukaoza wote au hata ajali..na wakulima wengi hawana utamaduni wa kukatia bima mazao yao
Mbaya zaidi unafika sokoni nyanya zimefurika inabidi uuze kwa hasara
Hivi vitu sio rahisi kihivyo
 
Back
Top Bottom