Kwanini unga hauwadhuru wasanii wa Majuu?

Singida ndio home

JF-Expert Member
Joined
Feb 23, 2012
Posts
3,188
Reaction score
3,370
Najiulizaga sana hivi ni kwanini unga cocaine hutumiwa na wasanii wengi sana majuu lakini bado wapo fiti labda kwa zamani ndo kina whitney houston na bobby brown ndo waliharibikiwa, ila ukija bongo wasanii wakigusa tu ndo kwaheri mfano kina chidi, rayc, tid, mfaume, daz baba, qchief, na wengine tushawapoteza kama kina ngwea na Langa


Mwenye uelewa tupe darasa
 

Kanga ndiyo msanii gani?
 



mtafute DMX NA EMINEN ndo utajua habar ya unga
 
Unajuaje hawaathiriki kama wa kwetu?
unawaona kama unavyo waona hawa wa kwetu?

Wasaniii wa nje wanafanyakazi katika makampuni makubwa
na hivyo hayo makampuni yana waataalam wa PR na masuala ya image sana tu
hiyo ndo tofauti

picha zao wakiwa wamechoka hasimbai sana
picha zao zinazosambazwa na za studio na make ups....
 
Mbona mimi natumia lakini sijaharibika?
 

Wanaathirika sana tu.

Lakini pia, rehab facilities bora pia zipo.

Ukitaka uone athari za madawa basi nenda kwenye hood au trailer parks.

Crackheads nje nje....
 
Ni staili tu ya kutumia hii mihadarati. Ni kama bangi tu... wengine wanaharibika na wengine hata huwezi jua kama wanavuta bangi, tena ni waheshimiwa
Ila mjomba sio mchezo watu wanaumia na hii ngada
 

Wasanii wa Ulaya / Marekani ( wabwia unga ) wanakula balanced diet huku Wasanii wa Kibongo ( wabwia unga ) wanakula just a diet.

Mlo kamili wa msanii Jay Z anayetumia dawa za kulevya ni kama ufuatao:

  • Maziwa
  • Cornflakes
  • Bread
  • Vegetables
  • Chocolate
  • Meat
  • Spaghetti
  • Irish Potatoes
  • Hamburger
  • Pizza
  • Chicken
  • Fish
Mlo kamili wa msanii Mfaume anayetumia dawa za kulevya ni kama ufuatao:
  • Kisamvu
  • Maharage ya kiporo
  • Chips za mafuta ya Transfoma
  • Mchicha ulioungua
  • Dagaa waliochacha
  • Pilau bichi
  • Wali nyama aliyepikiwa na Nzi ndani yake
  • Maziwa fresh ya Ng'ombe mwenye Kifaduro
  • Kuku waliokuzwa kwa vidonge vya kukuza makalio ( matako ) ya Dada zetu.
  • Maji ya kunywa ya Mto Ruvu yaliyojambiwa sana na Mamba na Viboko
Mkuu kwa mtiririko huo wa hapo juu nadhani utakuwa umeshapata jawabu la swali uliloliuliza. Nakutakia kila la kheri!
 
Wao hawachoki sbb wana mkwanja mrefu ht atumie dawa kiasi gani kuchoka labda ikitokea na pesa zimeisha.afu wenzetu wanatumia just for fun huku wanatumia kuondoa mastress w lazma wachoke.kingine wanatumia unga mchafu umechakachuliwa umejazwa mavalium na madawa mengine mabovu.kule wanapata kitu fresh from skuli
 
ngada ikikukolea ni balaa hata uwe nani itakutepetesha tu kama umetumia muda mrefu. hata hao wa majuu wanalegea na kupoteza dira na kufa kabisa tu,ona maradona,whitney,dmx,tyson,michael jackson,. tofauti ni kwamba wao wapo kwenye mazingira mazuri na pia wanakula cocaine ya kiwangoo sio hizi cement wanazokula huku bongo. pili wa majuu wanakula vizuri na kufanya mazoezi sana ndio maana hata athari zake kiafy na kiakili zinakuwa ndogo tofauti na bongo. huku kwetu mtu hata chai hajanywa kashavutta mzigo wa tsh 5,000/= tayari asubuhi. hawawezi hiyo kitu kwani inahitaji gharama kubwa mno kuimudu ili uendelee kula stimu zake. me nawashauri wavute bangi,hayo ndo madawa pekee watayoweza kumudu tena wale vizuri washibe then ndo wavute. Cocaine Na Heroin ni gharama mno,kwa sisi wabongo ni kujitesa na kupelekea kifo cha mapema tu.. Inasikitisha sana ukiwakuta mateja wakiwa hawajavuta,ni maumivu matupu kuanzia saikolojia mpaka mwili.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…