Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Nilihisi nimekula ban kumbe na wewe ni hivyo hivyo.
 
Kwa kwel Mwenyezi Mungu aendelee kumuongoza mama Samia, kwa vijana ametufungulia njia, ameturudishia upya matumaini. Tunaiman na raisi wetu mama samia

Ni kweli kabisa kamanda, ila hili la kurudisha mamlaka ya kuajiri kwa taasisi husika nina wasiwasi washauri wake wamemdanganya, badala ya kuboresha wamedhoofisha.
 
Wakuu Naomba kuuliza, kwenye tangazo la kuitwa kazini wanasema kuwa barua inabidi ifatwe ndani ya siku 7, zikizidi siku 7 barua itatumwa kwenye sanduku la Posta la muhusika

Sasa tunajua kuwa barua waga zinachelewa sana kufika huko kwenye sanduku la muhusika, je kuna uwezekano kuwa ata zikipita hizo siku 7 mtu akienda utumishi atakuta barua bado IPO?

Kuna changamoto ya kwenda ndani ya week hii kwahiyo badala ya kusubiri nitumiwe posta me nataka Niende week ijayo, je kuna uwezekano nitaikuta barua au nitakuwa nimepishana nayo?

Nahitaji mawazo ya wazoefu, kama kuna ambao waliwahi kwenda kwa kuchelewa ile ndani ya siku 7 utumishi na wakaikuta barua yao
 
Nenda PSRS utaikuta barua yako hawatumi kwenye address maana hamziandiki correctly, upo Dar alafu unaandika p.o box Moshi

Nenda kachukue barua ureport kazini haraka sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…