Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Basi inatosha tulia sasa au mpaka utupiwe majini😂
 
yan jamaa hajaripoti hata kazin lakn maneno kibao..kashajiona tayari na usikute kumbe kashamfollow dotto magari insta😂
Mkuu nyie wa Vijijini huko ndio mnaambiana dotto magari ana magari ya kuuza??? 🤣 anyway mimi nilisha screenshoot gari la kununua since nipo jobless hata hela ya kula sina ila nilikuwa na dream za gari.
 
Wakuu nikitulia suala la kuwaambia jinsi nilivyoanza hustle za kusaka mrija , interview ngapi nimefanya mpka kufanikisha etc.... Ila kikubwa wakati wa Mungu ukifika umefika... Cz hata hiyo Oral sikuwa perfect kivile. Yani kuna maswali nimejibu mle ndani ila nimetoka nje sikumbuki niliongea nini..
So hata kama umeona ulijibu vibaya oral huwezi jua, sifikirii kama wanaangalia tu ulichojibu... Nahisi appearance ,yako... Kujiamini kwenye kujibu, thn usiwe mbishi ,usiwapotezee muda kama hujui with comfidence sema tu hapo twendeni swali la mbele... Mimi nakumbuka maswali 2 sikujibu kabisa.

Niliwaambia twendeni mbele wakaniuliza , Twende thn utayarudia au niweke hujui nikamjibu weka sijui. Na kweli nilikuwa sijui.
 
Sasa unamkuta mtu mwengine anaulizwa swali anaona hapa hajui thn anaakaa kimya ..wakimwambia twende swali jengine...anasema ooh Noo... wait .thn aanaanza kuunga point anaitafuutaaa anapata moja anakaa kimya , huku anafikiria wanamwangalia tu ...wanasema tena twende anakataa..mpka wenyewe wanauliza swali linalofuata . Sasa anakuwa kama anawaletea ubishi flani hivi. Wakati kuna kijiji nje na wao wanatakiwa wasailiwe.

Mimi niliingia oral moja na hiyo ndio niliyotoboa , niliingia youtube nikaangalia jinsi gani unatakiwa ujibu alooo kwanza sauti inatakiwa itoke ,🤣 usmile , uwaangalie usoni, usijipigilee sana mpka mtu akikuona ajue aaahh huyu mbona kama hana shida kivile... Usikae bila kuambiwa ,usinyanyuke bila kuambiwa.. tia huruma. Fata maelekezo.
 
Unakuta raia ananyuka Suti ,yani ile yenyewe kabisa. Sio suit kachumbari zile za karume pale...Yani Suit yenyewe kabisa.. ananukia unyunyu saa moja kaliiiii 🤣. Bro pendeza ila usipendeze sana mpka waone mambo safi ....
 
Mkuu hakuna ukweli wowote na hizo Mambo z kuaga au kutokuaga, ila kwa Akili ya kawaida tu unaaga watu ili iweje ilhali unaenda kubeti?

Aga kama kitu una UHAKIKA nacho, ila unaaga alafu baada ya muda watu wanaendelea kukuona tena uraiani ni wazi utaonekana ulifeli interview, sasa Kwanini uwape watu vitu vya kusema

We Sepa kimya kimya na lengo ni kukaa kwa Amani kitaa pindi utakaporudi kuskilizia ili ata ukizingua watu hawajui kama ulienda interview

Huwa inakera watu wanapojua ulienda interview na bado unaonekana kitaa Tu ata kama utumishi watachelewa kukupangia kituo wao hawajui hayo, wao wanajua ulifeli Tu na kuonekana Mzigo kitaa

Turudi kwenye point ya msingi nini ufanye utoboe, Kwanza inaonekana Kada yenu inatoa Ajira chache ndomana hadi Written wanaanza kuchukua 75, it means nawewe inabidi uset standard ya kuanza kupata kuanzia at least 75

Written ya Kwanza hukufika 50, ila ya pili ukafika 65, that means ya pili uliongeza juhudi katika kujiandaa, ndo kitu unachotakiwa kukifanya kwenye interview inayofata, kwenye Written jitajihidi uwe miongoni mwa best performer kisha kwenye Oral acha Lucky ichukue mkondo wake

Na kingine cha muhimu kabisa, mitihani ya Utumishi sio necta, jitajihidi kwa mbinu yoyote ile uhakikishe unapata mark's za kutosha, unapoingia kwenye pepa chagua watu ambao unajua wako vizuri, na hasa wale fresh from school vichwa waga bado viko fresh, au jamaa zako ambao unajua walikuwa visomo sana ndio ukae nao

Na ukiona swali halitembei Kwa uwezo wako fanya juu chini usaidiwe, muache utoto wa shule kwamba utaonekanaje ukiomba majibu, hapo upo unatafuta future ambayo inaweza ikaamliwa na Makaratasi Tu, kwahiyo jibu swali ambalo Una uhakika nalo Tu na kama sio sumbua watu wakupe majibu

Ukipita Oral hapo waga ni 50/50 haijarishi ulifanya vizuri au ulifanya vibaya, Siri ya oral wanaijua hao hao utumishi, tupo watu ambao tulitoka kwenye oral tumefanya hovyo ila tukapata kazi, ila kazi inaanzia kwenye Written not otherwise
 
Mkumbushe pia anaweza pata marks 50 na asiingie Oral interview [emoji817]
Mimi sikuwa nazungumzia written examinations...nilikuwa nazungumzia oral yenyewe...kuwa pass mark inaanzia 50. Na kuwa huko oral, si lazima ujibu vipengele vyote vya maswali uliyoulizwa ili ufaulu.
 
Mkuu umeongea sahihi kwa asilimia 100% ,ila swala la kupiga chabo hapo au kuingia na supportive material utumishi wakikudaka wanafungia na account yako huwezi omba kazi serikalini tena...

Kuna jamaa wao walitumia mbinu ya kufanyiana bahati mbaya wakadakwa .walifungwa miaka 3 na kuzuiwa kuomba kazi utumishi tena .na tangazo lilitoka. Cheating is prohibited.

Ila vyengine vyote umeongea ni sawa .
 
Mkuu nasisitiza, shukuru umepata hiyo kazi, unavoendelea kushuhudia hapa unaanza kuwavua nguo utumishi.
Maswali mawili hukujibu, na hata uliyojibu hukumbuki ulijibu nini na bado ukachomoka kwa database "best loser".
 
Mkuu hapo kwenye Gharama ni kweli kama hauna side hustle au ndugu ambao wako tayari kuchangia mihangaiko yako basi ujue huwezi kufika kwenye interview

Nachoweza kukushauri tu ndugu, kuwa Oral ndio real deal, so ukishajua hilo pambania written as if ndio ya mwisho, kadri unavozidi kukaa mtaani na ugumu wa Maisha plus stress Akili waga haiwi sharp tena kama mwanzo

Me nataka kuwashauri watu ambao sio fresh from school maana kichwa ina Mambo mengi, unapoenda kupiga Written tengeneza kijiji brother na wala usione aibu maana unajua hali ya nyumbani na unaju hali yako

Utumishi waga hawana Mambo ya kukamia kwenye kusimamia kwa sababu wanajua watainiwa mtaoneana aibu, ila kwanini uone aibu wakati umeenda kutafuta Maisha bro, chukua raia ambazo waga unaziamini kwenye msuli weka pembeni subiri pepa ianze

Cheki pepa kama kuna maswali wewe mwenyewe unaweza kuyapiga anza nayo Kwa speed Kali sana, and mind you, utumishi wanaangalia points and logic basi, usitumie muda mwingi kuandika mavitu kibao yatakupotezea muda Tu wala hawajali, kuwa short/briefly but clear

Ukimaliza maswali/swali ambalo unaliweza sasa geukia washkaji waanze kukupa points kwenye maswali ambayo huyajui, mtu ata akupe points 3 Kati ya 5 hizo beba na ujaze kama zilivo kwani ulikuwa unazijua?

Kikubwa cha kuzingatia wakati wa kuchagua kijiji ni Aina ya watu, chagua watu ambao unaamini/unajua ni watoaji wa msaada, kuna wengine pamoja na kwamba wanasugua kitaa ila bado Wana Akili za kitoto za kushindana, hao watakubania majibu kwa sababu atataka aendeleee kuonekana Bora kuliko wewe

Hii ndio mbinu ambayo Mimi na jamaa zangu wote ambao wapo kwenye Ajira tulikuwa tunaitumia na kwakweli inalipa maana unajikuta Written zote unatoboa na kufika kwenye Oral, huko kama nilivosema mwanzo hakuna Mjanja, ni Zari lako tu ila sasa ili upate hilo Zari inabidi ufike hiyo level
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…