Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Ni asubuhi nyingine Tena.
Tunashukuru kwa uzima.
Tuwe na matumaini mapya.

Leo trh 13/01/2024 nakamilsha miez Saba(7) tangu kufanya oral naamini PDF ijayo ni zamu yangu[emoji120]..

Kitaa cha moto kwel kweli.
Hawajawahi kutoa placement yenye kada yako kabisa? au walishawahi kutoa?
 
Wote ambao walifaulu oral watapata nafasi kwa muda wao.

PSRS wanapoita watu wengi oral huku nafasi zikiwa chache sio kwamba wanataka kuwapotezea watu muda, hapana.

Hapo inakuwa ni Advantage kwa pande zote mbili(PSRS na Jobless). PSRS wataokoa muda wa kusaili mara kwa mara kwa nafasi zile zile kwa kuweka hao akiba ili waje kuwapangia nafasi baadae. Jobless wanakuwa wanaokolewa pia kwenye ishu ya muda na gharama za kwenda kufanya usaili tena.

Kwahiyo pindi ukiitwa kwenye usaili, kuwa na malengo 2 hata kama nafasi ni 1.

Lengo la kwanza, kafanye usaili ili upatw hiyo nafasi kwa muda huo.

Lengo la pili, kafanye usaili ili ubaki database endapo lengo la kwanza likikwama. Kukaa database ni ushindi kulinganisha na yule aliyeogopa kwenda kufanya kisa nafasi ni 1 na akaamua kutoenda ili asipoteze muda na pesa.

Mimi nilijiwekea hayo malengo 2 hasa lengo la pili baada ya kukandwa saili za mwanzo(saili 3). Bahati nzuri nikaangukia kwenye lengo la kwanza, pia hata kama ningekwama kwenye lengo la kwanza ningekuwa nishatimiza lengo la pili hadi sasa maana tayari kundi letu lote tushapangiwa kazi
Ubarikiwe kwa Ujumbe mzito...
 
Back
Top Bottom