Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Hii mikando inaonekana imekatisha ndoto za vijana wengi yaani ni sawa unangojea kifo
Nouma washanikanda uko nyuma subiri wee nahisi data base imesha expire, ukiwa mzembe unakufa kwa mawazo mwamba ajawahi piga ata written moja anachagua taasisi

Watu wanaitwa buku wanatoboa watatu kwenda oral na uko bado wanakukanda

Aisee neema ya Mungu itutembelee.
 
Pole mkuu
Maombi muhimu sio waliopata wanajua sana au aliyekosa hajui neema tu ya Mungu ikifika unatoka

Saizi niko sawa kuna mda kila nikifikiria kichwa kilikuwa kinauma

Mda wangu, pesa zangu expectations zangu Dah zilikuwa zinataka kuniua

Wale sio sehemu ya kusema utapata jalibu wait ukipata hewala ukikosa sawa

Psrs sio watu wa mchezo.
 
Hapa kwenye gharama mkuu ndio kunakoleta shida yaani uende interview Dodoma may be mara mbili au tatu halafu uambulie patupu

Halafu kwanini nafasi ni mbili wanaita watu kibao ili iweje
 
Hapa kwenye gharama mkuu ndio kunakoleta shida yaani uende interview Dodoma may be mara mbili au tatu halafu uambulie patupu

Halafu kwanini nafasi ni mbili wanaita watu kibao ili iweje
Karibu kwenye game kufaulu tu written ni kasheshe ila kwa ujumla

Mungu mwm tunaendelea kuishi.
 
Hapa kwenye gharama mkuu ndio kunakoleta shida yaani uende interview Dodoma may be mara mbili au tatu halafu uambulie patupu

Halafu kwanini nafasi ni mbili wanaita watu kibao ili iweje
Kiukweli kiubinadamu sometimes inakera.

Mimi nimeenda Dodoma 2 times Olaaa.

Ya 3 ndo nikatoboa ila hata ivyo Database mwezi huu ndo imeisha.

Nasubiri ya nne nione inakuaje.

Kiukweli ukifikiria gharama Dar Dom.

Kula.

Kulala

Nauli.

Unaweza usiende kwa usaili
 
Mimi hii ni mara yangu yakwanza nataka nibet lakini nitabet kwenye mikeka yenye odd nyingi kwasababu najua itakavyokuwa tunacheza pata potea

Asa mtu una recieved 5 zote ukiitwa utaenda mara ngapi? Je gharama utatumia shingapi?

Halafu uombe Mungu unase hata moja zote zikiwa ola na kamtaji umekatumia kote kwenye nauli na malazi si umejitia umasikini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…