Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Nimekua nikihidhuria mikando toka mwaka 2022. Katika mabadiliko haya, mikando inazidi kuwa migumu, mosi, coverage, aptitude inatoa fursa kwa wakandaji kutunga mkando kwa topic/modules/course nyingi zaidi.
Nakubaliana na wewe sababu ni MCQS ambapo kila topic/module inaweza kutoa swali.

Kwenye written ya kuandika kwenye karatasi ndio topics chache zilikuwa zinatolewa hasa swali likiwa la kuelezea
 
Mkuu kwa hizo post za wakemia kuna mdau kasoma lab akiomba wanamwambia hawez kuapply na kaweka vyeti vyote kwa hii changamoto utumishi wanaweza kumsaidia maana zile ajira za lab za nyuma aliweza kuapply vzuri tu
Amesoma Lab ipi?

Medical Lab au Lab Technology ?
 
Wakuu hivi paper za utumishi huwa hazivuji?
Unajua binadamu ni mtu mwenye tamaa,lolote linaweza kutokea maana akiingia tamaa anaweza vujisha ila kwa kifupi wapo makini sana utumishi
Jiandae vyema tu mkuu utafaulu tu hakuna janja janja ndo maana unaona watu wanapiga namba za viatu hapo na amechoma nauli kigoma to dom😂
 
Asee Kwa hiyo hao jamaa wa utumishi wanakaza hata kwa watoto wa vigogo😂

Kuwa chujio la watoto wa vigogo na sisi wagonga ulimbo ni moja?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…