Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Leo jioni admin anaachia pdf lingine. Safari hii ni reeeefuuu. Watu wa afya mtanenepa kwa raha msimu huu
Hii ndo mida ya ma-pdf ya nguvu. Hadi kufika kwenye saa tatu tatu za usiku hivi kuna watu watasahau ghafla adha waliyokutana nayo katika harakati za kusaka ajira kupitia mikando ya PSRS! Ni sawa na mjamzito kujifungua, utungu wote unatoweka ghafla mara baada ya kujifungua!
 
Tupeni ushuhuda mlioenda kufuata barua vipi vituo ni mkoa ulikoomba au popote kambi?
 
Polite jambo mzeee
Ila ni wizard ya afya mzeee hakuna shida maisha ni mkoani pale pale mjini πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
DAh kuna mwamba yeye kaenda leo kufuata barua anasema kapangiwa health centre labda kama ananipanga tu
 
Katibu - Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira Katika Utumishi wa Umma anapendakuwatangazia waombaji kazi wote wa Kada za Ualimu ambao wameitwa kwenyeusaili kupitia tangazo la kuitwa kwenye usaili la tarehe 15 Oktoba, 2024 kuwa usailihuo umesitishwa kwa sasa mpaka hapo mtakapojulishwa tena.

Kusitisha ni tofauti na kuahirisha! kusitisha ni kutokufanyika! kuahirisha ni kusogeza mbele! walimu jiandaeni kupangiwa vituo kwa mujibu wa taratibu za Tamisemi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…