Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Huwezi kujiamini kwa kitu ambacho aliyekufanyia usaili sio ndugu yako Wala hauna mahusiano nae.Kikubwa tu Wakati wako Ukifika kama Mungu Kaamua basi kazi itakuwa yako tu hata ushindani uwe vipi.Kikubwa tupende kushukuru Mungu Kwa kila jambo liwe Baya au zuri tulipokee.
 
Ahsante kwa kushare hiki kisa, mwanzoni nadhani mimi nilikuovertake maana nilianza kuhadithia habari za kukuona kule kwa kukuhisi jinsi mlivyokuwa na suti zenu.

Uliishia kusema kidogo nimepatia[emoji3][emoji3][emoji3]

Hizi ndio changamoto katika utafutaji
 
Yes hapo nlikuwa nacheka tu ila ata baada ya kukubaliwa mapema bado moyo ulikuwa unaniuma.
 
Dala dala za saba saba tuachie sisi wenye roho ngumu na wabahili(certified Jobless)[emoji3][emoji3][emoji3].

Mimi nishazijua kitambo utaratibu wao wa kujaza hadi mlango ufungwe na mtu aliyopo nje.

Huwa nafika hapo nusu saa kabla ndio napanda na kusubiri hiyo nusu saa watu wajae tuondoke.

Asubuhi nafika pale 7 7 saa kumi na mbili kami au na dk kadhaa, nusu saa ya kujaza, dk zilizobaki ni kujikokota(maana hizo dala dala hazina speed kama za Dar) hadi UDOM.

Siku ya Oral ya NAOT nilipofika na jina langu likaitwa moja kwa moja maana nilifika saa 1 na dk 5 - 10.
 
Kuna jamaa wa utumishi aliniambia "Hivi umesoma una degree kweli wewe "? Siku ya written. Moyo uliniumaaaaa,nikapotezea nikapiga mtihani nikarudi zangu Tandahimba. Pamoja na kuniambia vile matokeo oral yakatoka nikaitwa nikaenda Asha Rose Migiro nikapiga oral nipo nasubiri placement.Nikipata asante Mungu nikikosa asante Mungu ila nitaendelea kuomba na kupambana.
 
Knsa aisee inabdi wawe watu wenye hurma sn
 
Pole sn mkuu ndo majibu ya walioshiba wengi wao ubinadam wao uko mbali sn
 
Kuna watu wa panel wengine Wana roho nzuri sana, Kuna mmama aliniuliza swali nikawa nalijibu huku moyoni najua kabisa hapa napoteanaa. Nilivyomaliza akanifafanulia akaniambia unajua flani tunazungumzia kitu flani, nikasema ngoja nianze upya akaniruhu, nikatiririka sometime ananiambia hiko umesema taja kingine! Sema placement HAIJATOKA mda mrefu sana Naamini pdf hii yenye vumbi nitakuwemo
 
Umenikumbusha huu mkeka uliondoka na mwanangu kimasihara.
Jamaa yangu alikuwaga hana imani kbs kuwa kuna kutoboa psrs, baada ya kuona ss tunaaply na yeye akaaply TRA, KUMBUKA lengo lake kubwa lilikuwa kuja kutest wanatoaje pepa, wanasahihishaje, ili ajipange sasa kwa saili zijazo. Akapiga written kawaida tu akaona hapo hatoboi akajua sasa maswali wanatoaje akarudi home kula msuli heavy, matokeo yanakuja kutoka ya ORAL YUMO [emoji3][emoji3][emoji3] HALAFU KUMBUKA KASHAKULA MSULI MZITO WA SAILI ZIJAZO. kwahiyo jamaa akaenda kupiga oral kiulaini sana kwasababu alikuwa anajinoa na kweli akapata kazi.
Nikajifunza zaidi huku PSRS NI KAZI NA kazi ni Ridhiki na Mtoaji ni Mungu WAKATI WETU UKIFIKA NARUDIA TENA WAKATI WETU UKIFIKA HAKUNA WAKUPINGA NA HATUTATUMIA NGUVU KUBWA SANA, kwahiyo tusiache kuomba, tusiache kuthubutu Ni suala la muda tu. PSRS hakuna cha ugenius wala ujuaji ni suala la muda tu kwasababu tunatafuta ridhiki ambazo ndio kazi zenyewe na Mpaji ni Mungu.
 
Hata mimi niliomba like kujaribu,heee! Nikashangaa ombi la 1 tu nimeitwa written na nikaitwa oral,sasa sijui kwenye placement nini kitajiri.Vyovyote poa tu.
 
Sure kbs wengine huwa wastaarabu sana mtu unaingia usaili saa7 hujala kutoka saa 1 mpk panelist aliniuliza unaonekana hujala tangu asbh[emoji3][emoji3][emoji1787][emoji1787]
 
Mimi hapo kwenye address nilipaacha tu blank, ili watakachokitaka nikiandike ndio nikiandike hapohapo. Sijawahi kuulizwa chochote kuhusiana na address kwenye interview zote, so huwa pako blank tu siku zote. Siku watakaponikaba nipajaze, hapo ndipo nitajaza kama wanavyotaka sasa.
 
Sure kbs wengine huwa wastaarabu sana mtu unaingia usaili saa7 hujala kutoka saa 1 mpk panelist aliniuliza unaonekana hujala tangu asbh[emoji3][emoji3][emoji1787][emoji1787]
Pole mkuu,ni palepale Asha Rose Migiro? Halafu hapana miundombinu mizuri ya kula.Inatakiwa ifunguliwe cafe nzuri na classic na chakula kiwe affordable. Watu wanashinda njaa sn sn pale Asha Rose Migiro.
 
Pole mkuu,ni palepale Asha Rose Migiro? Halafu hapana miundombinu mizuri ya kula.Inatakiwa ifunguliwe cafe nzuri na classic na chakula kiwe affordable. Watu wanashinda njaa sn sn pale Asha Rose Migiro.
Hapohapo migiro sio rafiki kbs, kwanza tulipigwa na jua, na hiyo njaa kisha tukaanza saa6 usaili its was so sad maana tulichoka kabla ya tukio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…