Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Upo sahihi, haswa ukiwa hujui ulipokosea ni wapi.

Nilikandwa TPA, ikafuata TASAC.. na zote nilifika oral. Yaan saivi nikiona hata logo za hizo taasisi nawamaind kichizi

Mungu atusaidie
Duuh!!! I Feel you bro! Hii kitu uliyopitia naelewa sana, ukizingatia written umetoboa kwa mbinde mpk kufika oral lkn yote kwa yote tusikate tamaa ndugu yangu, lets keep it up Mema yako mbele hii hali huwa tunapitia wengi ila sometimes tunatulia tu.....Tuendelee kutumaini kuwa yajayo ni mazuri sana na Mungu atubariki sote ...Ameeen
 
Ameeen
 
Nyie kukandwa kubaya sana hasa kwa taasisi ambayo ulikuwa ukiikubali muda sana, mwenzenu Tangia nimekandwa na TRA najiona sipo sawa kabisa. Hii ni seriously guys.

Hii huwa inatokea sana mkuu na hasa ukiwa na matarajio makubwa kulingana na ulivyojiandaa pamoja na ulivyofanya hiyo mitihani.

Binafsi usail uliopita TMO II nilikosa maksi moja kuingia oral, awamu hii nikaongeza kupiga msuli na kujiamin zaidi lkn baada ya matokeo nimedondokea pua na wkt mtihani niliona wa kawaida.

UKiwa na moyo mwepesi baada ya matokeo kutoka na yasiwe mazuri umaweza pata maradhi kama ulikuwa na matarajio makubwa.

Ushauri wangu ili kuepukana na msongo wa mawazo/ sonona.

1. Kupunguza matarajio makubwa kabla ya matokeo.

2. Kufanya mazoezi, hii inasaidia kurudisha mwili kuwa normal.

3. Kujichanganya na watu tofauti ili kuepukana na mawazo ya kufeli.

4. Kupitia threads tofauti humu JF ambazo ni za kuelimisha, kuburudisha, siasa pomoja na mapenzi na mahusiano(MMU).

5. Kuendelea na ratiba zako kama kawaida huku ukiendelea na kutafuta mrija sehemu tofauti.
 
Umeongea FACT MKUU.
 
Nashukuru kwa ushauri wako mkuu,
 
Umeongea sahihi hii Cha kujipa matarajio makubwa ndo kinachonitesa mimi, baada ya zile za mwezi wa 4 kutokuitwa katika usahili kutokana na vyeti kutokuwa certified, niliumia pia nikajisemea ninamkosi gani kwani kabla ya hapo nilishakuwa nikiitwa katika usahili bila kupiga muhuri, furaha yangu ilikuja kurudishwa tena baada ya hizi za awamu ya pili kutangazwa hivyo niliona kama nimepewa second chance naimekuja special kwaajili yangu kwa namna nilivyoumia kwenye Ile ya kwanza, hivyo nilipata nguvu kubwa ya kusema hii ni kwaajili yangu.
 
Polee sana, expectations always hurt. Utakua sawa giv it time.
 

Ahaa sawa Mkuu, asante sana. Naomba kama kuna mwingine anaufafanuzi zaidi au tofauti ili nikitoa ushauri nisije bahati mbaya nikashindwa kukidhi kiu ya aliyeniuliza.
 
Take your time hustler ralax

Jikusanye ukiona tena wamepost vacancies apply this utakuwa mtabe sana na over expectation itapungua.
 
Yaaah hyo inatokeaga kutokana na ufinyu wa venue Ila changamoto kubwa inakuja upande wa Oral kama ulifanikiwa zote
@Armstrongs alifanya oral mbili kwa siku moja.

Ukienda siku ya oral waambie una oral 2, moja wakupange uingie mapema, ukimaliza hapo unakusubiri nyingine.
 
Ikitokea mfano Mr. Y academic background alipita form iv/vi, akaenda cert/dip, akafika mpaka bachelor, halafu vyeti vyote akapandisha, huyo mtu ataruhusiwa kushiriki katika nafasi zinazotaka highest qualification, kwa maana ya bachelor. System itamtema akiomba nafasi inayotaka dip/cert aliyokua nayo awali.
 

Ndio mkuu, ukipandisha vyeti vyote, kitakachotumika ni chenye ngazi ya juu. Ukijaribu kuomba nafasi za chini mfumo unakukataa.

Ukitaka kuomba ngazi za chini basi usipandishe vyeti vya ngazi ya juu. Mfano una barchelor lkn ulianzia diploma, basi pandisha cheti cha diploma tu ili uweze kuomba nafasi za ngazi hyo tu.
 
Kweli kabisa ukiweka cha digrii uwezi omba kazi ya diploma au chini ya hapo. Lakini kama una digrii ukasoma na masters, ukiomba kazi kwa sifa ya digrii inakubali na mastarz yenyewe inakubali kwahiyo huyu wa masters wamempa uwanja mpana, lakini mwenye digrii ku apply diploma wamembana
 
Alafu Una registere kwa NIDA🤣
 
Acheni Roho mbaya , vijana wameamua kujiongeza kielimu nyie mkaona wao watafaidi. Kila MTU anahaki ya kuomba KAZI anayotaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…