Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kumbuka mwingine kaingia kazini ana diploma, kajiendeleza kapata degree so kazi ikitangazwa psrs anaomba maana hakuna kupanda kama miaka hiyo kazi inatangazwa inagombewa. Wapo wengi sana wa hivi.
 
Yaelekea ulifanya vizuri sana,mpaka una hamu nayo hivyo...
Kuwa mpole kidogo,mlifanya kikanda,lazima wataunganisha matokeo Kwa pamoja kwanza ndio wataachia Majina yangu.Sasa endelea kuomba tu.
Sorry, hapa watachukua ratio ya kikanda au watachukua waliofaulu tu hata kama ni Kanda moja. Let assume kama Kanda moja au tatu hakuna aliyepata 50, na waliopata 50 and above ni Kanda moja let say dar tu, je wataziacha Kanda nyingine au watajaribu kibalance Kila Kanda itoe mtu?
 
Suala ni kufaulu upite parsmark...kanda ni kituo tu cha kufnyia mtihni sio kigezo cha kufaulu
 
SAhili zimefanyika kikanda ili kupunguza gharama kwa watafuta ajira, lakini matokeo hayatoka kwa kanda bali yatajumuishwa pamoja na wale waliofika kiwango stahiki ndio watasonga kwa hatua inayofuata.
 
SAhili zimefanyika kikanda ili kupunguza gharama kwa watafuta ajira, lakini matokeo hayatoka kwa kanda bali yatajumuishwa pamoja na wale waliofika kiwango stahiki ndio watasonga kwa hatua inayofuata.
Asante sana kwa majibu mazuri, lakini ingekuwa vizuri zaidi kama wangezingatia selection kikanda ili kwenye usaili wa mahojihano wakutane watu kutoka sehemu mbalimbali ingependeza sana na kuleta faraja kwa baadhi ya watu. All in all wakati wa Mungu ndio sahihi kabisa maishani mwetu.
 
Hauoni kama hii italeta bias fulani kwa baadhi ya mikoa kukosa wawakilishi?

Kinachotafutwa sio wawakilishi wa kanda husika, bali ni vijana wa Kitanzania walifaulu/ wenye sifa husika kulingana na kazi iliyotangazwa kwenda kufanya hayo majukumu.

Kwa hyo baadhi ya kanda kama hawana vijana wenye sifa watasaidiwa na wenzao toka maeneo mengine. Muhimu ni kupata watu wenye sifa ya kufanya hyo kazi.
 
Mkuu kweli unahisi kuna kanda wanaweza kufeli wote?siamini katika hilo.
Ila issue kubwa ni kufaulu tu haijalishi umetoka kanda ipi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…