Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

b

bonge la topic man maana kitaa hakukaliki. Nishajiendeaga hadi machimboni chunya lkn bdo life halijanipa haueni .nikarudi bongo dili la usimamiz wa sensa kidogo likanipa unafuu Nakumiliki geto la ngwea.Nimejaribu kulizia mishe viwandani malipo mengi ya kimagushi mno 5k per day. Kubeti sitamani coz nafahamu bet zilivoteketeza boom langu. Huwa na waza sana hzi trip Domu za usaili jobles ambae hauna mishe uta afford vipi. Ama nauli mnaomba skani nini? Tupeni ramani wazee mnapunguzaje ukali wa maisha huku kitaani jobless wenzangu?
Mi leo nafungua meza buguruni sokoni nikauze mboga mboga
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Unakuta manzi yeye ni jobless afu anataka mwenye kazi sasa sisi jobless tupendwe na nani??

Unaona sasa shida hiyo Mkuu, na jobless akijichanganya akajidai anajua kupenda amekwisha, ataishia kupewa huduma ya mgao kama umeme na maji pamoja na kupigwa matukio mpaka ajiuzulu mwenyewe.
 
Haya mambo haya, naomba nitoe ushuhuda, me kipindi nipo chuo nlikuwa na hela mno, ni hivi vibiashara vyangu na kidogo walezi wangu walikuwa vizuri na elimu wanaithamini sana. Nlikuwa na boy friend wangu akiniomba 5000, 10,000 sion shida kumpa. Kidogo kwao hawakuwa vizuri na yeye ndo first born, vitu vya ndani nanunua nampa, akija hostel namchambulia vitu nampa, hadi nlimpa jiko la umeme awe anapikia kwake maana chuo warden alikaza. Inshort nlimbeba sana. Nauli za chuo nampa hapo yeye ndo anasoma CPA. Aisee baadae akalamba asali bana TRA, kama custom officer, na mimi nkamaliza chuo maisha yakanipiga, akabadilika kabisa kabisa, nkawa nalia na mapenzi wee[emoji23][emoji1787], akahamishiwa Dar nkahisi labda shida ilikuwa long distance rship, Dar wakamuweka TPA, aisee na mapenzi yakaisha kabisa na mimi nkasema hamna changu hapa, kama ni pesa najua kuitafuta. From then aisee nkajisemea kumbe haya mambo sio ya wadada peke yao. Ata mdada unaweza mvumilia jobless mwenzio hapa akilamba asali tu ndo anakuonaje sijui [emoji1787]. Kikubwa upendo tu.

Duh! Mkuu, pole sana. Jamaa ametusaliti wanaume, mbona wengi tunatafuta wanamke wanaojitambua hivyo!

Tafadhali usiruhusu akufanye uwachukie majobless wenzio. Hata wenye kazi, wapo wenye akili mbovu kama huyo au zaidi.
 
Vijisenti vinatia kiburi sijui kwa nini kwa watu wote(Me na Ke).

Utasikia "Huyu sio type yangu"

Kuna mdada mmoja katika kupiga story, mada ya wachumba ikaingia.

Yeye alidai anataka mwanaume mwenye funguo 3. Ufunguo wa Nyumba, Gari na Duka.

Mwanamke kama huyu ni rahisi kukupiga kibuti akivipata hivyo kwa mwanaume mwingine
Yeye anazo hizo funguo tatu?Tuanzie hapo kwanza.
 
Vijisenti vinatia kiburi sijui kwa nini kwa watu wote(Me na Ke).

Utasikia "Huyu sio type yangu"

Kuna mdada mmoja katika kupiga story, mada ya wachumba ikaingia.

Yeye alidai anataka mwanaume mwenye funguo 3. Ufunguo wa Nyumba, Gari na Duka.

Mwanamke kama huyu ni rahisi kukupiga kibuti akivipata hivyo kwa mwanaume mwingine

Wanawake wa hivi huwa wanatengewa bajeti, let us say laki tano kuanzia kukutana naye mpaka siku ya tukio, pesa ikiisha na mahusiano yameisha. Labda atumie pesa yake kuyaendesha, tofauti na hapo biashara imekwisha.
 
Hahaha, duh! Mkuu, mbona mnafanya maisha ya Jf yawe magumu sana.

Hili jibu lako limenifanya niende kutafuta Panadol kupoza maumivu.

Hujui tu hiyo picha yako ni kwa kiasi gani imefanya wanaume humu tukupe ukarimu wa hali ya juu.

Siumeona wizy alivyokuwa anapata tabu ya kuhakikisha kila ujumbe wako anaukomenti, unadhani angejua ni kidume mwenzetu angehangaika!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom