Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Hii ya TRA noma saana niliomba kwenye position 3 mkeka umerudi wamenitupa kwenye position ambayo walitoa nafasi moja tu na wameitwa watu zaidi ya 176... Dah! Laaleki hapa ndo taaabu inapoanza,, mawazo ya niende au nisiende yanakuja
Ingekuwa ni PSRS ningekushauri uwende Ila uko TRA itabid usikilizie moyo, maamuzi kwako mkuu
 
Siyo mbaya akiwahoji. Ajibu email waliyomtaarifu kuwa hajawa shortlisted kwa kuwaomba walitazame upya suala lake, kama kweli ana uhakika kuwa kuna aliowazidi lakini wameitwa kwenye usaili!

Sawa boss, nitahakikisha namjulisha hili.
 
Wengi wameachwa vigezo walivyo tangaza na walichofanya tofauti, kwanza kuanzia mfumo wao umekaa ovyo unahitani marekebisho ili iwe rahisi kuomba ajira. Nibora wawe wawazi kwamba wanataka vigezo kadhaa kuliko kukata majina watu bila reason ya msingi na mtubkafuatabutaratibu wote .
Kama TRA watachiwa waendelee na mfuomo wao, kuaniri huko ni ngumu sana kwa watu ambao hawana connection.Imeisha hiyo.

Hahahahahaha. Hili uko sahihi sana boss. Nakuunga mkono, maboresho yanahitajika.
 
Kwa izi za TRA tutegemee kusikia mengi wale wa kujitolea, internship hao tayari washasign mikataba ya kudumu, bado wale tumetumwa na mjamba, sijui dada kaniagiza hao nao watalamba asali bila pingamizi, sasa tusubirie izo gombania goli nawahakikishieni wataziuza nahakika pesa zitatembea, afadhali ya PSRS
Watu wamekaa bar Magomeni wanapangia watu vituo vya kazi kabla ya interview
 
Wakuu APC Mbweni ni uelekeo gani?naomba mifahamishe namna ya kufika
Hiyo iko maeneo ya Mbweni Moga panda gari za Bunju shukia Kituo kinaitwa Kwa Jumbe, vuka barabara fanya kama unarudi nyuma kidogo ulipotoka kuna lami inaingia upande wa kushoto, hapo kama utachukua boda au bajaji itabidi uchukue anayepafahamu au uulizie tu akupeleke APC Hotel and Conference Centre
 
kitambo sana niliacha kupoteza muda, kama ufahamu kuna watu wanautumia huo muda wa wewe unaopoteza kutafuta ajira kukuchapa
Hizi fikra zimenijia siku za karibuni baada ya kuona mwaka umeisha kama wiki kwa kusubiria placement mpaka sasa haijulikani lini zitatoka.
Ni miezi mitatu sasa nimestop kuomba tena
Wakati wa Mungu ni wakati sahihi,

Nami nlikua mmoja wa wasioamini katika Database, Hatimae database hio imenitoa baada ya miezi zaidi ya 10 tangu nifanye Oral,

Tuamini katika bidii zetu na zaidi katika wakati wa Mungu
ukawe mtumishi mwema hongera sana.
 
Back
Top Bottom