Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Yani mimi mpaka sasa kitu sijakielewa ni mtu amepita hadi Oral kwenye TRA halafu tunamshauri aachane na interview aende akaanze upya written, practicals ndio afike Oral MDA and LGA!

Kwa lugha rahisi kwa mwanaume kuelewa ni sawa na mtu atongoze mwanamke mzuri tena wakishua aliyekuwa anagombaniwa na maelfu ya watu, afike mpaka chumbani kisha zianze kufululiza simu za masela kwamba huyo demu asimguse kwa sababu anangoma! Eti wamshauri kuna demu mwingine hana ngoma, sio wakishua na ni wakawaida wamemtumia namba kwa Whatsapp amtongoze.

Nayeye kweli anakubali kuiacha pisi ya kishua ili aende akatongoze upya.

Kupewa namba ya simu ya demu mwingine sio inshu, je akikataliwa kwenye hatua za mwanzo? Halafu vipi kama kuhusu ngoma kwa wakishua ni tetesi zisizo na ukweli?
KAKA WATU NI WANA ROHO MBAYA, YANI WANAMSHAURI MSELA UJINGA....YANI KAFIKA HATUA MOJA
MBELE BADO STEP MOJA AMALIZE.... WANAMUAMBIA RUDI KAANZE UPYA ...SASA JE AKIENDA HUKO KWENYE UPYA AKAKATWA??? MWANZO JE 🤣🤣YANI BINADAMU WANAMUONEA MTU GERE HATA KUMJUA HAWAMJUI HUYO JAMAA AKIEANDA MDA BASI ATAKUWA HAMNAZO NA YEYE
 
Watu wanamshauri akafanye MDA&LGA wanasababu maalum ujue..

Kama umepitia mkeka wa TRA oral nayo wameingiza watu wengi sana so chance ya kuwa selected ni ngumu ukizingatia taarifa za uvumi kuhusiana na TRA.

1.KUAJIRI KWA KUJUANA.
2.MFUMO USIOELEWEKA WA KUAJIRI MAANA NDO WAMEANZA UPYA KUAJIRI BAADA YA KUJITOA PSRS.
3.HAWANA DATABASE.


Tukirudi PSRS kama jamaa ataweza kufanikiwa kufanya interview ya oral basi tutarajie kupata furaha yake kamili maana anaweza..

1.KUPATA DIRECT POST
2.KUBAKI KWENYE DATABASE.
3.MFUMO WA AJIRA WA PSRS HUKO CLEAR NA UNAELEWEKA ILA TRA BADO PASUA KICHWA.

NA ndio maana Unaona watu wengi wanamshauri aende akafanye MDA LGA.

Hahahahaha! Sawa kamanda.
 
ILA KAMA JAMAA YUKO VIZURI KIUCHUMI.

MJMI NAMSHAURI HIVI.

TAR 5 ORAL APIGE MDA LGA DODOMA.

halfu kwa kuwa practical ya MDALGA ni tarehe 8 basi Tutarajie matokeo kutoka tarehe tarh 6 usiku so wakimaliza oral asiondoke akae mpaka tarhe sita usiku asubiri matokeo .

Yakitoka kama atakuwa amefaulu oral basi waendelee na practical tarh 8 dodoma .

Ikitokea kakandwa aanze safari tarh 7 kuja dar kufanya oral yake TRA.

So kufanya interview TRA naona kutategemeana na majibu ya oral MDA.

Ushauri huu naona unanishawishi zaidi.

Ninachohofia ni namna watu wengi tunafanya assumptions kwamba MDA & LGA atafaulu mpaka kufika hatua ya kusubiri placements. Kitu ambacho inaweza isiwe hivyo au ikawa hivyo.

Utumishi nao wana mauzauza mengi sana ila kwa sasa tumeyasahau kwa sababu hatujaridhishwa na taasisi kurudishiwa mamlaka ya kuajiri.

Mimi nawajua wengi na hata humu wamo ambao hawajawahi kufika Oral na haimaanishi mitihani ya Utumishi kwao ni migumu, huwa inawajia vizuri wakawa na uhakika wa kufaulu lakini matokeo yakaja wamepata marks za hovyo na hawaijui sababu.
 
Sasa TRA wakuwaamini na ww

Hahahahaha! Mkuu hata utumishi kinachotufanya tuwaamini sio kwamba wako fair sana, bali ni kuna watu wasio na connection wamepata kazi tena sehemu nyeti. Lakini hili halimaanishi kwamba ni lazima kila mtu anatendewa haki na hakuna mambo ya connection.

Hata TRA siamini kwamba haya mawazo yetu ya wengi watapita kwa connection basi ni nafasi zote zitajazwa kwa connection.
 
KAKA WATU NI WANA ROHO MBAYA, YANI WANAMSHAURI MSELA UJINGA....YANI KAFIKA HATUA MOJA
MBELE BADO STEP MOJA AMALIZE.... WANAMUAMBIA RUDI KAANZE UPYA ...SASA JE AKIENDA HUKO KWENYE UPYA AKAKATWA??? MWANZO JE [emoji1787][emoji1787]YANI BINADAMU WANAMUONEA MTU GERE HATA KUMJUA HAWAMJUI HUYO JAMAA AKIEANDA MDA BASI ATAKUWA HAMNAZO NA YEYE

Hahahahaha! Nimecheka kwa nguvu kaka. Sio gere, lengo ni kumsaidia mwenzetu kwenye utata anaoupitia ili afanye maamuzi sahihi asitoe boko [emoji23].

Pande zote mbili zinafaida na hasara zake, ndio maana nikatolea mfano TRA kuwa ni manzi anayevumishiwa taarifa mbaya, kumbe inawezekana ni za kweli au sio kweli.
 
KAKA WATU NI WANA ROHO MBAYA, YANI WANAMSHAURI MSELA UJINGA....YANI KAFIKA HATUA MOJA
MBELE BADO STEP MOJA AMALIZE.... WANAMUAMBIA RUDI KAANZE UPYA ...SASA JE AKIENDA HUKO KWENYE UPYA AKAKATWA??? MWANZO JE 🤣🤣YANI BINADAMU WANAMUONEA MTU GERE HATA KUMJUA HAWAMJUI HUYO JAMAA AKIEANDA MDA BASI ATAKUWA HAMNAZO NA YEYE
Sioni kama waliomshauri mshikaji wana maana kama unayomanisha hapa.
pili ,inaonekana wewe ni mgeni wa sahili za TRA, TANROD, IMMIGRATION NK
bila maelekezo ni ngumu sana kutoboa , ndio maana anashauriwa aende PSRS . Ila hajalazimishwa
 
Nimejichanganya kwa kweli, kwenye ratiba wameandika zote tatu, usaili wa kuandika, vitendo na mahojiano. Nipo njia panda, baada ya TRA kubadili ratiba ya usaili wa mahojiano kuwa tarehe 08/11, na hapo jana nimekuwa shortlisted utumishi mda's & lga's

Saili nilizonazo
Tarehe 05/11 -MDA's & LGA's - Written interview -Dodoma
**Tarehe 08/11 -TRA Oral interview- Dar es salaam
**Tarehe 08/11 - MDA's & LGA's - Practical interview -Dodoma
Tarehe 09/11 - MDA's & LGA's - Oral interview -Dodoma

Ushauri wenu wakuu

Piga chini prac ya MDA's & LGA's.

Pia andaa pesa ya kutosha kwa ajili ya hizo safari dar-dom
 
Back
Top Bottom