Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Dah ! Rahsully kimya sana , jamaa wameamua kutupigia chini nini maana hii sio data base tena aisee tunaenda miaka miwili sasa hivi ,maana ni mwaka na miezi minne sasa toka tumepiga ile interview
Yaan nlivyoona wameanza kuita mpaka mwezi wa 9 nkasema duh,nshachinjiwa baharini asee🤣🤣🤣🤣
 
Omba kazi ya examination officer Electrical Engineer Kwa NECTA
Kuna tangazo nimeliona
Aisee mi mpaka cheti ya ERB kisha expire kabisa siwezi omba kazi yoyote mpaka nirenew na nina bonge la deni la fine na michango ya ERB ,sijui hata nalipa vipi .
Na wamekua washenzi siku iz mpaka ulipe madeni yao ndio warenew hiko chet yaan tabu tupu,tunapitia pagumu Acha tu,mtu huna ajira na bado tunalipishwa pesa
 
Nishaota kipara kabisa , mtaani siku hizi vitoto vishenzi na mama zao wananiita " yule mbaba dalali ana midevu flani hivi kama Osama anakaa nyumba ile "
🤣🤣🤣🤣🤣

😂😂😂 mtoto akikataa kwenda shule wanamwambia wekataa shule tuu, somaa useje ukawa kama dalali midevu.. Daah!.

Nakumbuka kuna kipind uko nyuma kabla sijapata iki kibarua cha sasahv nilishawai kufanya kazi ya kushusha mifuko ya cement dereva alikua anatupiga madongo 'wakati mko kwenu ww na dada yako mlikua mnatega shule sasahv dada yako kaolewa aya sasa kazi kwako'. Yeye alikua anajua woote tuliokua tunafanya ile kazi tulikimbia shule..
 
Back
Top Bottom