Kwanza unatakiwa utambue uwanja wa ndege unahitaji eneo kubwa la kutosha kwa ajili ya barabara ya kurukia na kupaki ndege.
Iisitoshe uwanja ulijengwa na wazungu enzi hizo Tanganyika haijapata uhuru hivo baada ya Uhuru Mwl Nyerere alikuja ongeza terminal 2 kwa kuwa tayari barabara ya kurukia ndege ilikuwepo na eneo lilikuwepo.
Pia tambua kuwa wakati uwanja huo unajengwa hakukuwa na makazi ya watu kama unavyoona.sasa ambapo watu ndiyo wamevamia eneo la karibu na uwanja.