Kwanini Vinywaji Vikali ( K-vant, konyagi, valuu n.k) haviwekwi kwenye friji?

Akili 2

JF-Expert Member
Joined
Jul 2, 2018
Posts
1,221
Reaction score
1,849
Salama wakuu

Ningependa kujuwa sababu za msingi na za kueleweka kuhusu Vinywaji Vikali,, Nimeenda maeneo mengi kunywa ila sijabahatika kukuta asilimia kubwa ya Vinywaji Vikali vikiwa kwenye friji je sababu kubwa huwa ni ipo?

Ningependa kujuwa ni maeneo gani naweza pata K-vant ya baridi au konyagi ya baridi Sana

Asante
 
Sababu ni rahisi kinywaji chochote chenye alcohol chini ya 15 kinaweza kuwekwa kwenye friji ila zaidi ya hapo hakina tatizo.

Yaaani ukiifungia K-vant yako leo ukainywa kidogo na usiweke kwenye friji unaikuta na makali yake yaleyale ila jaribu kwa Serengeti Lite yako uone
 
Hahahahah kwamba serengeti itachacha mkuu?
 
umejibu vilivyo, upo sahihi kabisa.
 
Ooohh kumbe,
 
sijui tuwaulize nini walevi. badala ya kuwaza mambo ya maana unawaza k-vant.
 
MKUU VIPI KUHUSU WINES ULISHAWAHI ONA ZIMEWEKWA KWENYE FRIJI???
 
Hata kinywaji chenye alcohol chini ya 15 kabla hujafungua sio lazima uweke kwenye friji na kinaweza kudumu muda mrefu tu.

Nadhani labda mtoa maada alichomaanisha ni kwa nn pombe kali hainywewi ikiwa ya baridi?
 
Sababu ya kuwekwa kwenye fridge ni kuweza kupata ladha nzuri zaidi..it's not about pre servation...ukitaka kupata taste nzuri ya wine inywe ikiwa ya baridi...hizo spirits haziwekwei kwenye fridge coz most of them watu hawanywi dry wanachanganya na vinywaji laini ambavyo vinakuja baridi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…