Kwanini Vyama vya Wafanyakazi havipigi kelele suala la Kikokotoo?

Voltaire

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2013
Posts
1,231
Reaction score
1,189
Kelele zimekuwa nyingi kuhusu kikokotoo, hamna kauli dhabiti iliyotoka toka kwa "Vyama vya Wafanyakazi".
Kazi ya hivi vyama binafsi siioni zaid ya kuvalishwa sare na kuandamana Mei Mosi, serikali tafadhali ongeza kikokotoo mara buku hadi akili ziwakae!

Kila mtu analalamikia chumbani kwake, hakuna hatua yoyote, COSATU ikawe desa lenu!
 
Taifa la misukule ,
 
Vitaanzia wapi, wakati viongozi, wao ni machawa, wa ccm, wakijifsrsgua tu, ama wapotezwe, au wafukuzwe kazi,
 
Chama gani CWT mabumunda?
Wao wanasubiri kuprint tishert za Mei Mosi. Ngoja nikadowee tender.
Vyama vyote mabumunda.
 
Kikokotoo ni meza yenye vinywaji vya wakwe, jaribu kuitingisha uwashiwe moto.
 
Ukisikia sentensi inasema Serikali imezungumza na “wadau na kupata maoni yao, unadhani hao “wadau ni kina nani?
 
Kwa uzoefu wangu toka serikali za mitaa tz hivi vyama vinaongozwa na watu wa masijala. Watu hawa hawana kikubwa wakijuacho zaidi ya kuwa machawa wa ma DED na HoDs hasa zile zenye mafungu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…