Kwanini Waafrica wengi waliokua brainwashed wanaamini Kupunguza Idadi ya watu ndio suluhisho la umasikini??

Kwanini Waafrica wengi waliokua brainwashed wanaamini Kupunguza Idadi ya watu ndio suluhisho la umasikini??

kwaiyo hapo uongeze uwezo au upunguze watoto???

marekani ilikua super power si kwa watu milion 2 au tano??

You need atleast 100million to start making some noise!!

Unaweza kutuambia kwann nigeria ni tajiri africa nzima??? ongea kwa mifano basi
Ila wanijeria ndio wanaongoza kukimbia nchi yao. Ukienda kule watu wanaoteka watu kwa ajili ya kupata pesa. Ukiona nchi imefika hatua watuwanafanya utekaji kupata hela ujue hali imefikia pabaya. Tusiongee kwa kusoma tu article za internet safiri uone. Zaa kulingana na uwezo wako usizae ukasubiri serikali ikulelee watoto. Kila mtu anapambania ugali wake hakuna mtu atakuja kusolve shida zako. Pambania ugali wako.
 
Ni kweli inabidi Africa tuzaane sana, 70% ya ardhi yetu ni misitu - inatakiwa ijae hiyo. Kwa kuanza kampeni Serikali yetu ya TZ ifanye promostion ukipata watoto zaidi ya 3, wale waliozidi wote wanakuwa mali ya Serikali kuanzia kuwasomesha, kuwalisha nk.

Hima himaaa Afiricaa ...
Rafiki yangu kila mtu anapambania ugali wake hakuna mtu atakuja kukusaidia kulea familia yako. Zaa kadri ya uwezo wako hakuna Serikali ya Afrika inaweza kusomesha na kuwalisha watoto wa wananchi.
 
Nitajie nchi mmoja ambayo ni super power yenye watu wachache?? Nchi itoke kwene top 20 za nchi zenye watu wachache??

Nitajie nchi moja yenye nguvu zaidi kijeshi yenye watu wachache??
Nitajie nchi yenye ushawishi mkubwa yenye watu wachache??


NB:Idadi ya watu Inauhusiano na Maendeleo na Kuwa taifa kubwa duniani

Zaeni zaeni zaeni ila muweze kuwalisha na kuwahudumia
Mpaka sasa Super power ni mmoja tu duniani, halafu sio kuangalia tu idadi jumla ya watu bali pamoja na "population density na demographic dividend'' pia.
 
Nchi inaweza kuwa na idadi kubwa ya watu lakini wengi si wazalishaji, Sasa unategemea maendeleo gani hapo?

Nchi kuwa na idadi ya watu wengi si kigezo cha maendeleo ya nchi.

Nchi inaweza kuwa na watu wengi wajinga, watu wengi wazee, watu wengi wanawake na watoto n.k

Mzigo mkubwa utaenda kwa serikali kuwahudumia hawa watu.
Ajifunze kitu kinaitwa demographic dividend
 
Sasa utapataje vipaji na talent kwenye population kubwa au utapataje productivity kwene population ndogo!!
Ebu niambie kama kuna siku Mauritius wanaweza wakawazidi GDP Nigeria???

Au rwanda ikaizidi GDP Tanzania

Yaan wao watacheza na hizo kumi kumi sisi tunayoyoma kwenye mia moja naaa
Sweden imeizidi Nigeria na Tanzania GDP
 
Ujerumani ukikosa kazi unalipwa asilimia 80 ya mshahara wako. Ukilipa 49Euro (134632 Tshs) unatumia usafiri wa umma kwenda sehemu yeyote ya nchi kwa mwezi mzima. Ukizaa mtoto serikali inakulipa kila mwezi kwa kila mtoto mpaka napofikisha miaka 25 na Elimu ni Bure mpaka chuo kikuu. Haya yote yamewezekana kwa sababu idadi yao ya watu inaendena na GDP yao. Zaa kadri ya uwezo wako usizae ukawaachia watoto serikali. Utatujazia wavuta bangi na makahaba mtaani.
Shida huku kwetu GDP iko kwa walioko madarakani na wanaweka nje ya nchi. Ndiyo maana wanatuhimiza kuzaa kidogo ili wasipate mzigo kutoa huduma.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Nitajie nchi mmoja ambayo ni super power yenye watu wachache?? Nchi itoke kwene top 20 za nchi zenye watu wachache??

Nitajie nchi moja yenye nguvu zaidi kijeshi yenye watu wachache??
Nitajie nchi yenye ushawishi mkubwa yenye watu wachache??


NB:Idadi ya watu Inauhusiano na Maendeleo na Kuwa taifa kubwa duniani

Zaeni zaeni zaeni ila muweze kuwalisha na kuwahudumia
North Korea chini ya Kim Jong Un Jr


Ina watu milion 25 ila ni moto wa kuotea mbali kijeshi Marekani mwenyewe anamgwaya!


Nyie endeleeni kuzaana kama Panya na wanaozaliwa wanakuja kuendesha bodaboda!

Wenzenu wanazaana ila sehemu kubwa ya wanaozaliwa wanakuwa rasilimali kwenye mikakati ya nchi!


Nyie mnazaa wakina Mwijaku, babalevo, Haji Manara ,
 
Shida huku kwetu GDP iko kwa walioko madarakani na wanaweka nje ya nchi. Ndiyo maana wanatuhimiza kuzaa kidogo ili wasipate mzigo kutoa huduma.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Sio kwamba wasipate mzigo wa kutoa huduma angalia nchi zetu ni wasomi wangapi wanaweza kutumia taaluma yao kisawa sawa. Kuna wakugurugenzi wa wilaya hawawezi hata kuchambua Balance sheet na projections. Sasa huyu mtu yupo hapo anafanya nini.Bora muwe wachache smart kama Singapore na Japan.
 
Tatizo elimu yetu haitusaidii, tulisoma advance Moja ya factor kubwa kukua Kwa ulaya ni demographics revolution, china walilijua Hilo ndio mana alipoingia mao tse tong aliwahamasisha Watu kuzaa mpaka ikafikia wachina kuwa ni 20% ya Watu wote wa dunia. Wazungu hawataki tupige hatua ndio mana wanatulisha matangopori
Vijana wamezagaa mtaani hawana kazi na ajira halafu mnashauri watu wazae. Mtazasha vibaka tu. Nchi kama Finland ina watu milioni tano lakini wana maisha bora na ni nchi ya watu wenye furaha. Na wanatupa misaada ya mabilioni.
 
Unajuaje wamekuwa brainwashed na hawajasema hivyo kwa kuelewa mambo?

Hii hoja yako ina logical fallacy inayoitwa non sequitur. Umeunganisha mambo yasiyo na muungano wa moja kwa moja.

Logic yake ni sawa na hii hapa chini.

1. Rais wa Tanzania ni mwanamke Mzanzibari. Hii ni fact inayojulikana.

2. Fatma Karume ni mwanamke Mzanzibari. Hii ni fact inayojulikana.

3. Hivyo, kwa vile rais wa Tanzania ni mwanamke Mzanzibari, na Fatma Karume ni mwanamke Mzanzibari, basi, Fatma Karume ni rais wa Tanzania.

Umefanya logical non sequitur hiyo hiyo.

1. Kuna nchi zina watu wengi.

2. Kuna nchi tajiri zenye watu wengi.

3. Hivyo, ili tuwe tajiri, tuongeze watu.

Hujaangalia factors nyingi sana, kama vile, kuna nchi zenye watu wengi ambazo si tajiri, kuna nchi zenye watu wachache tajiri, hujaangalia uwezo wa nchi kutumia watu wake, hujaangalia population and resources, technology etc.

Hujaangalla "correlation is not causation".

Hujaangalia economic sustainability.

Hujaangalia the probkem of induction. Inawezekana katika dunia ambayo hizo nchi zikiendelea, dunia ya ujima na mercantilism, ilikuwa kweli ukiongeza watu unaongeza ufanisi wa uchumi, lakini je, kika kilichokuwa kweli jana ni lazima kiwe kweli leo?

Katika dunia ambayo ardhi na resources haziongezeki, utaongeza watu mpaka wapi ili usije kuleta madhara?

Kama tatizo lako si watu -watu unao wengi ambao huwatumii vizuri, hawana kazi, au wako underemployed- hujui kutumia hawa watu waliopo na wanaishia kukisa huduma za jamii, elimu na lishe bora, ukiongeza watu bila kujua kuwatumia utataua vipi matatizo yako? Utahakikisha vipi huongezi tatizo?
Nakurudia 😂
 
Vijana wamezagaa mtaani hawana kazi na ajira halafu mnashauri watu wazae. Mtazasha vibaka tu. Nchi kama Finland ina watu milioni tano lakini wana maisha bora na ni nchi ya watu wenye furaha. Na wanatupa misaada ya mabilioni.
Ukifunga uzazi ndio ajira zitapatikana!
hawana kazi kwasababu nchi inaongozwa na wajinga! mmeshindwa kulima hata tikit mtengeneze juice ya tikiti kiwanda kinaajiri watu wangap, kilimo kinaajiri watu wangap na wafanyabiashara wa matunda na wauza juice??
 
Nitajie nchi mmoja ambayo ni super power yenye watu wachache?? Nchi itoke kwene top 20 za nchi zenye watu wachache??

Nitajie nchi moja yenye nguvu zaidi kijeshi yenye watu wachache??
Nitajie nchi yenye ushawishi mkubwa yenye watu wachache??


NB:Idadi ya watu Inauhusiano na Maendeleo na Kuwa taifa kubwa duniani

Zaeni zaeni zaeni ila muweze kuwalisha na kuwahudumi
Nchi hizo zimecreate ajira Ili ziwe land of opportunities sasa mtu Yuko na financial instability alafu aendelee kufyatua watoto nn kitatokea . Cheki nchi kama Australia ilivyopitiaga kipindi kigumu miaka ya themanini watu wakaanza kujiuwa kutokana na mental stress baada ya kupitiwa na redudunce. Waka rephrase a situation now they are good mtu ana miaka ishirini ameoa na ana maisha mazuri, nitafutie bongo mtu wa umri huo kama ana watoto amezalishwa na kutelekezwa watoto wanakuwa chokoraa wa mitaan kwann watu wa hivyo wasijizuie kuzaa? Ad wakati ukiwa sawa .
 
Nchi hizo zimecreate ajira Ili ziwe land of opportunities sasa mtu Yuko na financial instability alafu aendelee kufyatua watoto nn kitatokea . Cheki nchi kama Australia ilivyopitiaga kipindi kigumu miaka ya themanini watu wakaanza kujiuwa kutokana na mental stress baada ya kupitiwa na redudunce. Waka rephrase a situation now they are good mtu ana miaka ishirini ameoa na ana maisha mazuri, nitafutie bongo mtu wa umri huo kama ana watoto amezalishwa na kutelekezwa watoto wanakuwa chokoraa wa mitaan kwann watu wa hivyo wasijizuie kuzaa? Ad wakati ukiwa sawa .
Mkuu hiyo ni poor thinking ! umasikin unasababishwa na poor distribution of wealth!
Sasa mbona bado katika uchache bado ni masikini??
CHINA na inawatu wengi kama bara lote la africa lakin matajir sisi masikini wakat tupo kwene bara lenye ukubwa 10 times ya china
 
Back
Top Bottom