Kwanini waandishi wa habari Tanzania hawaripoti taarifa zenye maslahi mapana kwa Taifa letu?

Kwanini waandishi wa habari Tanzania hawaripoti taarifa zenye maslahi mapana kwa Taifa letu?

Tasnia ya habari Tanzania ni pasua kichwa mkuu hii inachangizwa na sababu mbalimbli ambazo kwa namna moja ama nyingine zinafanya waandishi kuogopa kufanya investigative journalism ( Habari za uchunguzi)

Mosi,waandishi wamepoteza dira kwa kuacha maadili ya kazi yao na kusaka nafasi za uteuzi hii imepelekea wengi kuwa makasuku mfano ni Mwandishi nguli Pasco mayalla.

Pili,Kupotea na vifo vya utata kwa waandishi wa habari ndani ya nchi hii nani asiye jua juu ya kupotea kwa Bwana Azori ngwanda wa Mwananchi communication limited? Bado tasnia ya habari haija sahau kifo Cha Daudi Mwangosi wa channel Ten mkoa wa Iringa vipi kuhusu kifo Cha utata Cha bwana Stani katabalo

Tatu,sheria kandamizi zipo bado tusijitoe ufahama kujisaulisha kwamba sheria zimebadilika zipo mfano ni The Media Service Act of 2016.licha kwamba sheria hii imetoa mwanga mzuri kwa kutambua Journalism Kama professional lakini Kuna vipengele ni hatari kwa ustawi wa tasnia ya habari nchini.

Nne,Kuto zingatia taaluma (unprofessionalism) Kuna watu mpaka Leo wanaamini kwamba uandishi ni kipaji(talent) na sio taaluma(professional) ndio maana kwenye media nyingi wamejaa vilaza mfano wakina Mwijaku,Baba levo nk

Tano, Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia yameleta kitu kinacho itwa "Citizen Journalism" hii kitu imekuwa challenge kwa waandishi wengi maana kila mtu ana share habari hivyo Mwandishi lazima afanye jambo la ziada kuonesha utofauti wake na watu ambao sio waandishi.

Kwa uchache naomb niishie hapa GT wataongeza madini muhumu
Kinkunti El Perdedo
Umenena vyema kabisa.

Hongera kwako🤝
 
Waandishi habari hawana tofauti na waalimu wetu wa shule na wahadhiri vyuo vya elimu ya juu.
bagamoyo
Hebu imagine, pamoja na kujaa kwa waandishi mbalimbali Katika "press conference" ya Chadema na madini yaliyotolewa na Naibu Katibu Mkuu, Kigaigai, kuhusiana na Mauaji ya Serengeti, ni jambo la kushangaza Sana, kuwa hdkuna chombo cha habari, kilichoripoti habari hiyo!🥺
 
Uandishi wa habari ulianza kuchezewa taratibu kipindi cha awamu ya pili ya JK, hii ni baada vya CCM kupoteza ushawishi kwa umma. Wakati ule CCM waliunda kikosi kazi kuona ni kwanini CCM imepoteza mvuto kwa umma. Sehemu moja ilionekana ni uhuru wa vyombo vya habari, na mitandao ya kijamii.

Baada ya mkakati ule kuanza, tuliona sheria mbalimbali zikitungwa ili kudhibiti uhuru wa vyombo vya habari, wakati huohuo tukaona CCM ikajaza Makada wake mitandaoni kwenye kile kilichoitwa kujibu mapigo. Hapo tuliona mijadala ikigeuzwa kuwa personal attack ili kuhamisha mijadala, na kwa kiwango fulani walifanikiwa. Alivyoingia Magufuli madarakani baada ya uchaguzi wa 2015, pale ndio rasmi uandishi wa habari zinazotakiwa na umma ulifikia kikomo, ukaja uandishi wa habari unaotakiwa na rais na serikali yake!

Kwa sasa uandishi uliopo kwenye vyombo rasmi vya habari ni unaotakiwa na serikali, na sio unaohitajiwa na umma. Sehemu pekee waandishi walipo huru ni kwenye kuripoti habari za simba na Yanga ambako hakuna madhara kwa walioko madarakani, lakini sio kuripoti habari ya maslahi ya umma yaliyo kinyume na matakwa ya serikali. Yaani sasa uandishi wa habari umewekewa speed governor iitwayo uchochezi, usalama ni kusifia serikali tu hata kama unasifia uongo huwezi kuchukuliwa hatua yoyote.
 
Nimekuwa nikifuatilia waandishi wa habari wa nchi hii, nikagundua kuwa zile habari muhimu sana, zenye maslahi mapana kwa Taifa hili hawaziandiki na badala yake, wao Kila siku ni kuandika "mapambio" ya kusifu na kuabudu viongozi walioko madarakani!

Waandishi wa habari wa nchi yetu, wamejijengea tabia ya kuwa hata kama ni "minor issue" ilimradi lmefanywa na watawala wetu wa CCM, basi watai-report kwa ukubwa Sana, wakati "big issues" kama hizo za kuuawa kwa raia zenye utata, wakizifukia!

waandishi wa habari Wana dhamana kubwa Sana ya kutuhahabarisha sisi wananchi kuhusu matukio mbalimbali yanayotokea hapa nchini.

Nikitoa mfano ni wa habari hii ilivyotokea majuzi ya Mauaji ya watuhumiwa watatu wa Mauaji wa ujambazi, yaliyotokea huko Serengeti, Mkoani Mara, ambapo uongozi wa Chadema, umetilia shaka Mauaji hayo, baada ya taarifa ya RPC wa Mara, kuwa watuhumiwa hao wa ujambazi, waliuawa, baada ya kurushiana risasi na askari.

Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema, kwa waandishi wa habari, ni kuwa taarifa hiyo inatia shaka Sana, kutokana na "circumstancial evidence" ya Mauaji hayo yalivyotokea.

Tufahamu pia wajibu namba moja wa Jeshi letu la Polisi, ni kutulinda sisi raia pamoja na mali zetu.

Kwa hiyo uongozi huo wa Chadema, umemuomba Rais Samia, aunde Tume ya Majaji, kuchunguza Mauaji hayo.

Uundwaji wa Tume hiyo ya Majaji, kwa tukio lenye utata, haitokuwa jambo geni, kwa kuwa kama mkumbukavyo, wakati wa utawala wa awamu ya nne, ya Jakaya Kikwete, aliunda Tume ya aina hiyo, baada ya Mauaji ya watu, ambao Polisi wetu walitoa taarifa kuwa waliwaua "majambazi" hao wakati wakijibizana risasi.

Hata hivyo baada ya Tume hiyo kutoa ripoti yake, ikaeleza kuwa hao waliotajwa na Jeshi letu la Polisi, kuwa walikuwa majambazi, hawakuwa majambazi, bali walikuwa wafanyibiashara halali wa madini, toka Ifakara!

Ili kuujua ukweli wa Mauaji yanayoendelea nchini kwetu, siku hadi siku, kwa madai ya Polisi, kuwa wameuawa baada ya kujibizana kwa risasi, inabidi Rais Samia, aunde Tume hiyo ya Majaji, Ili kuondoa utata huu, kwa kuwa kwa mfumo wetu wa utawala, mhimili pekee unaoweza kutoa hukumu ya kifo ni mhimili wa Mahakama baada ya kupokea ushahidi.

Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa sheria zetu, hakuna mtu mwingine yeyote aliyepewa mamlaka hiyo ya kuua raia bila kwanza kupata ushahidi usiokuwa na shaka.

Kuendelea kuruhusu mtindo huu wa Polisi kujichukulia sheria mkononi, Taifa hili tunaliingiza kwenye hatari kubwa, kwa kuwa leo yamewakuta hao raia wa Serengeti, nani anayejua who is next, may be it can be you or me.

Mungu ibariki Tanzania
Kila mwandishi anajipendekeza ile apate uteuzi. Habari siku hizi ziko kwenye social media tu
 
Kwa kifupi tasnia ya uandishi wa habari bongo ni jipu

Ukiacha uhuru wa vyombo vya habari pia
(1)Hatuna waandishi wa habari wanaojua kuhoji wanapokuwa kwenye interviews na viongozi wanaowaalika kwenye media zao au wanapokuwa kwenye press conference na viongozi

(2)Hatuna waandishi wa habari wanaoweza kufanya habari za kiuchunguzi kwa uweledi

(3)Hatuna waandishi wa habari waliobobea kwenye masuala kama ya uchumi, biashara, siasa, diplomasia. Hii inafanya habari zao ziwe nyepesi sana.

Kwa mfano vipindi vya asubuhi kwenye media nyingi wanasema eti wanafanya uchambuzi wa habari zilizo kwenye magazeti sioni uchambuzi mule ni kelele tupu.

Na Kitenge ndo kaleta huu ujinga alipokuwa Wasafi saivi kila media wameiga ndo upuuzi unaofanywa. Nilichogundua waandishi wengi kichwani weupe hawana madini, hawasomi na hawafanyi utafiti

(4)Hatuna waandishi wanaoweza kufuatilia mambo kwa kina hadi mwisho wengi wanaenda kwa trending. Muda si mrefu hatutaona wala kusikia habari za sakata la makinikia
 
Kwa hiyo uongozi huo wa Chadema, umemuomba Rais Samia, aunde Tume ya Majaji, kuchunguza Mauaji hayo.

Nimesikiliza na kuona kwenye runinga mimi mwenyewe.

Viongozi wa CDM "hawakumuomba" rais, bali "walimuelekeza".
Binafsi walinishangaza sana. Maana, maana inaonekana CDM hawajui mamlaka ya rais. Unaweza kutoa maelekezo kwa mamlaka ambayo umeiteua. Hiyo ndiyo unaisimamia na hata kuipa nidhamu. Lkn huwezi kutoa maelekezo kwa mamlaka ambayo iko juu yako. Tena juu sana.
 
Kwa kifupi tasnia ya uandishi wa habari bongo ni jipu

Ukiacha uhuru wa vyombo vy habari pia
(1)Hatuna waandishi wa habari wanaojua kuhoji wanapokuwa kwenye interviews na viongozi wanaowaalika kwenye media zao au wanapokuwa kwenye press conference na viongozi

(2)Hatuna waandishi wa habari wanaoweza kufanya habari za kiuchunguzi kwa uweledi

(3)Hatuna waandishi wa habari waliobobea kwenye masuala kama ya uchumi, biashara, siasa, diplomasia. Hii inafanya habari zao ziwe nyepesi sana.

Kwa mfano vipindi vya asubuhi kwenye media nyingi wanasema eti wanafanya uchambuzi wa habari zilizo kwenye magazeti sioni uchambuzi mule ni kelele tupu.

Na Kitenge ndo kaleta huu ujinga alipokuwa Wasafi saivi kila media wameiga ndo upuuzi unaofanywa. Nilichogundua waandishi wengi kichwani weupe hawana madini, hawasomi na hawafanyi utafiti

(4)Hatuna waandishi wanaoweza kufuatilia mambo kwa kina hadi mwisho wengi wanaenda kwa trending. Muda si mrefu hatutaona wala kusikia habari za sakata la makinikia

Nadhani changamoto inaanzia kwenye ubora wa wanafunzi wanaojiunga kwenye hiyo fani ya uandishi wa habari.
Zamani kidogo, kulikuwa na waandishi wenye uwezo mkubwa kitaaluma. Wanafunzi wengi waliojiunga walikuwa B and above. Kuna kipindi hapo katikati, waandishi wengi hawakuwa na msingi madhubuti wa kwenye taaluma ukilinganisha na fani zingine. Fani zingine kama uhandisi, udaktari, sheria nk. Sasa shida ni msingi, tukiboresha entry point to journalism, matokeo tutayaona.
 
Nadhani changamoto inaanzia kwenye ubora wa wanafunzi wanaojiunga kwenye hiyo fani ya uandishi wa habari.
Zamani kidogo, kulikuwa na waandishi wenye uwezo mkubwa kitaaluma. Wanafunzi wengi waliojiunga walikuwa B and above. Kuna kipindi hapo katikati, waandishi wengi hawakuwa na msingi madhubuti wa kwenye taaluma ukilinganisha na fani zingine. Fani zingine kama uhandisi, udaktari, sheria nk. Sasa shida ni msingi, tukiboresha entry point to journalism, matokeo tutayaona.
Ni kweli
 
Nimekuwa nikifuatilia waandishi wa habari wa nchi hii, nikagundua kuwa zile habari muhimu sana, zenye maslahi mapana kwa Taifa hili hawaziandiki na badala yake, wao Kila siku ni kuandika "mapambio" ya kusifu na kuabudu viongozi walioko madarakani!
Tatizo la Waandishi wetu, ama kwa makusudi ama kwa kutojua, wanadhani Serikali na Taifa ni kitu moja!! Bora basi hayo yangekuwa yanafanywa na Uhuru, Habari Leo, na Daily News lakini hata magazeti binafsi, wao nao ni watu wa ku-advocate serikali zaidi kuliko taifa!!

But kwa upande mwingine, now am sick na watu wanaojitambulisha kama Waandishi wa Habari!! Hii ni taalamu inayohitaji watu wenye uelewa mpana kuliko watu wanaoenda huko kwa sababu tu walishindwa kuchaguliwa kusoma LL.B na kozi pendwa zingine!!
 
Nimekuwa nikifuatilia waandishi wa habari wa nchi hii, nikagundua kuwa zile habari muhimu sana, zenye maslahi mapana kwa Taifa hili hawaziandiki na badala yake, wao Kila siku ni kuandika "mapambio" ya kusifu na kuabudu viongozi walioko madarakani!

Waandishi wa habari wa nchi yetu, wamejijengea tabia ya kuwa hata kama ni "minor issue" ilimradi lmefanywa na watawala wetu wa CCM, basi watai-report kwa ukubwa Sana, wakati "big issues" kama hizo za kuuawa kwa raia zenye utata, wakizifukia!

waandishi wa habari Wana dhamana kubwa Sana ya kutuhahabarisha sisi wananchi kuhusu matukio mbalimbali yanayotokea hapa nchini.

Nikitoa mfano ni wa habari hii ilivyotokea majuzi ya Mauaji ya watuhumiwa watatu wa Mauaji wa ujambazi, yaliyotokea huko Serengeti, Mkoani Mara, ambapo uongozi wa Chadema, umetilia shaka Mauaji hayo, baada ya taarifa ya RPC wa Mara, kuwa watuhumiwa hao wa ujambazi, waliuawa, baada ya kurushiana risasi na askari.

Hata hivyo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Chadema, kwa waandishi wa habari, ni kuwa taarifa hiyo inatia shaka Sana, kutokana na "circumstancial evidence" ya Mauaji hayo yalivyotokea.

Tufahamu pia wajibu namba moja wa Jeshi letu la Polisi, ni kutulinda sisi raia pamoja na mali zetu.

Kwa hiyo uongozi huo wa Chadema, umemuomba Rais Samia, aunde Tume ya Majaji, kuchunguza Mauaji hayo.

Uundwaji wa Tume hiyo ya Majaji, kwa tukio lenye utata, haitokuwa jambo geni, kwa kuwa kama mkumbukavyo, wakati wa utawala wa awamu ya nne, ya Jakaya Kikwete, aliunda Tume ya aina hiyo, baada ya Mauaji ya watu, ambao Polisi wetu walitoa taarifa kuwa waliwaua "majambazi" hao wakati wakijibizana risasi.

Hata hivyo baada ya Tume hiyo kutoa ripoti yake, ikaeleza kuwa hao waliotajwa na Jeshi letu la Polisi, kuwa walikuwa majambazi, hawakuwa majambazi, bali walikuwa wafanyibiashara halali wa madini, toka Ifakara!

Ili kuujua ukweli wa Mauaji yanayoendelea nchini kwetu, siku hadi siku, kwa madai ya Polisi, kuwa wameuawa baada ya kujibizana kwa risasi, inabidi Rais Samia, aunde Tume hiyo ya Majaji, Ili kuondoa utata huu, kwa kuwa kwa mfumo wetu wa utawala, mhimili pekee unaoweza kutoa hukumu ya kifo ni mhimili wa Mahakama baada ya kupokea ushahidi.

Kwa maana hiyo, kwa mujibu wa sheria zetu, hakuna mtu mwingine yeyote aliyepewa mamlaka hiyo ya kuua raia bila kwanza kupata ushahidi usiokuwa na shaka.

Kuendelea kuruhusu mtindo huu wa Polisi kujichukulia sheria mkononi, Taifa hili tunaliingiza kwenye hatari kubwa, kwa kuwa leo yamewakuta hao raia wa Serengeti, nani anayejua who is next, may be it can be you or me.

Mungu ibariki Tanzania
Nimesoma hoja yako. Kwanza umeiwasilisha vizuri na kwa lugha ya heshima! Ila nami nakumbusha kitu kibaitwa Responsible Journalism. Mwandishi wa habari siyo tu anawajibika kuuza habari bali pia kulinda maslahi ya nchi. Kwa mfano, masuala ya usalama; ukiripoti bila FACTS tu kisa fulani kasema utawajibika kwa mujibu wa sheria.

Hata ikiwa mahakamani au bungeni ambako kuna kinga, bado Responsible Journalism inaweza kukuongoza uiache habari kama inaweza athiri maslahi ya nchi. Sasa chama cha siasa kutuhumu tu polisi bila FACTS sioni kosa la waandishi kuitupa story. Watu waeleze FACTS na hii nikuwa scientific tu kwa kutafuta evidence ambao ni ukweli wa mambo , siyo maneno ya mitaani ktk jambo nyeti. #Tukemee ujambazi.🙏🙏🙏
 
Waandishi wa habari wanawakilisha jamii yao kwa upana. Jamii ya bongo kwa jitahada za watawala na akili za raia wengi imejikita mno katika Simba na Yanga, comedy zisozotumia akili sana za kina Mandonga, Pierre, Shika n.k
 
Nimesoma hoja yako. Kwanza umeiwasilisha vizuri na kwa lugha ya hsshma. Ila nami nakumbusha kitu kibaitwa Responsible Journalism. Mwandishi wa habari siyo tu anawajibika kuuza habari bali pia kulinda maslahi ya nchi. Kwa mfano, masuala ya usalama; ukiripoti bila FACTS tu kisa fulani kasema utawajibika kwa mujibu wa sheria.

Hata ikiwa mahakamani au bungeni ambako kuna kinga, bado Responsible Journalism inaweza kukuongoza uiache habari kama inaweza athiri maslahi ya nchi. Sasa chama cha siasa kutuhumu tu polisi bila FACTS sioni kosa la waandishi kuitupa story. Watu waeleze FACTS na hii nikuwa scientific tu kwa kutafuta ukweli, siyo maneno ya mitaani ktk jambo nyeti. #Tukemee ujambazi.🙏🙏🙏
semtawa
Sasa nikuulize swali wewe ulieleta hoja hii, hivi kuna madhara gani, kwa mwandishi wa habari kuripoti kuwa kiongozi wa Chadema amemtaka Rais Samia aunde Tume ya Majaji kuchunguza Mauaji ya utata ya kupigwa risasi watuhumiwa wa ujambazi?
 
Nimesoma hoja yako. Kwanza umeiwasilisha vizuri na kwa lugha ya heshima! Ila nami nakumbusha kitu kibaitwa Responsible Journalism. Mwandishi wa habari siyo tu anawajibika kuuza habari bali pia kulinda maslahi ya nchi. Kwa mfano, masuala ya usalama; ukiripoti bila FACTS tu kisa fulani kasema utawajibika kwa mujibu wa sheria.

Hata ikiwa mahakamani au bungeni ambako kuna kinga, bado Responsible Journalism inaweza kukuongoza uiache habari kama inaweza athiri maslahi ya nchi. Sasa chama cha siasa kutuhumu tu polisi bila FACTS sioni kosa la waandishi kuitupa story. Watu waeleze FACTS na hii nikuwa scientific tu kwa kutafuta evidence ambao ni ukweli wa mambo , siyo maneno ya mitaani ktk jambo nyeti. #Tukemee ujambazi.🙏🙏🙏
Mkuu semtawa, thanks for this, waelimishe madogo humu kuhusu kitu kinachoitwa responsible journalism, media tukiitwa press conference, haturipoti kama kasuku, tunatumia objectivity kuamua turipoti nini kwa kutanguliza mbele maslahi ya Taifa.
P
 
Nimesikiliza na kuona kwenye runinga mimi mwenyewe.

Viongozi wa CDM "hawakumuomba" rais, bali "walimuelekeza".
Binafsi walinishangaza sana. Maana, maana inaonekana CDM hawajui mamlaka ya rais. Unaweza kutoa maelekezo kwa mamlaka ambayo umeiteua. Hiyo ndiyo unaisimamia na hata kuipa nidhamu. Lkn huwezi kutoa maelekezo kwa mamlaka ambayo iko juu yako. Tena juu sana.

Kwa taarifa yako rais ni muajiriwa wa wananchi na sio boss wa wananchi. Kwa bahati mbaya kwa katiba ya nchi hii na vimelea vya ujamaa vilivyopo, rais amegeuka mungu mtu hawezi kuhojiwa. Kwenye nchi za wenzetu kiongozi anaagizwa na anaweza kuhojiwa hadi kuondolewa madarakani ikibidi. Huku rais ndio anaamua nani awe kiongozi, hata viti kama ubunge na udiwani ambao huchaguliwa na wananchi kikatiba, siku hizi yeye ndio anaamua nani akalie kiti, kisa cha yote haya ni chawa wa aina yenu mnaomtukuza rais.
 
Back
Top Bottom