Yoda
JF-Expert Member
- Jul 22, 2018
- 48,475
- 70,102
Umaskini ukikutana na itikadi za msimamo mkali ni kama kiberiti kilichowashwa karibu na petrol.
Kama tatizo lingekuwa Waislamu kwani Dubai wengi wao ni wa dini gani na msuguano kama huo umeuona?
Qatar napo kuna Wahindi wengi msuguano kama huo umeuona?
Kuwait kuna Wahindi wengi msuguano wa namna hiyo umeusikia?
Kote huko Wahindi wana nyumba zao za ibada.
Kuna kipindi ilikuwa ni mwezi wa Ramadhani futari iliandaliwa kabla ya kuswali magharibi ili baada ya swala watu wale. Kwa ghafla kundi la nyani likavamia na kula futari. Kumaliza swala nyani wanakula futari.
Viongozi wakasema tusiwafukuze! Wakaenda temple ya karibu kuwaambia kuna suala limetokea kwenye nyumba yetu ya ibada tunaomba mtusaidie kuli tatua. Walipofika wakakuta nyani wanakula futari, walifurahi sana! Wakalipia gharama ya chakula chote kwa ujumla. Sikujua ina maanisha nini! Kuuliza nikaambiwa ile temple nyani ni mungu wao! Tungeliwakimbiza laiti wangelituona ingelikuwa mtafaruku mkubwa! Wahindu wana miungu mingi! Kuwa makini na kila kiumbe ukiwa kwenye jamii yao hususani India.
Kwa Waislam kuna dhehebu linaloitwa Salafi. Salafi nao wamegawanyika; kuna wa moto kiasi na wa moto kabisa. Hawa chao ni sahihi cha kwako si sahihi, ukimfuata upo sahihi usipomfuata umepotea. Hawa ndoa zao wanafungishana wao tu! Wengine wanafika mbali kabisa asie Muislam kwao wanamuona amekuja bahati mbaya duniani. Fahamu pia; mpaka Waislamu dheheb la Sunni kwa upande wa Salafi wanawaona Sunni wamepotea hivyo utapewa majina mabaya kweli.
Sasa Muhidu mwenye dini nyingi na miungu mingi wawe ndani ya jamii moja na Salafi unategemea nini? Chuki itakuwepo baina yao na uhasama mkubwa!