Kwanza Usalafi ni mmoja tu. Na kuugawanya kama wanavyofanya baadhi ya watu hasa wasomi wa Kimagharibi kwenye mapote mfano "Quietist Salafism" au "Salafi Jihadist" ni makosa.
Na hutakuta Salafi eti anasema nje ya Masheikh uliowataja wewe hakuna Dini. Hapo utakuwa unamaanisha kuwa hao "Masalafi" unaowazungumza hawachukui kutoka kwa Imaam Ibn Kathir, Ibn Qudama, al-Khatib al-Baghdadi, Ibn Asakir, Ibn al-Jawzi, Ibn Rajab al-Hambali, Adh-Dhahabi, Imaam Ibn Hajar al-Asqalaani, Imaam Suyuuti, Imaam Mahmud Shukri al-Alusi, Imaam Shawkaani, Imaam Ibn Jarir at-Tabari, Imaam Ibn Khuzaimah, Imaam at-Tahawi, Ibn Abil-Izz al-Hanafi, Imaam Ibn Hazm, Qadhi 'Iyad na wengine weeeengi mno (Allah awarehemu wote) na awahifadhi walio hai.
Pia, Isis na wengine mfano wao sio Masalafi, bali ni Makhawaarij (sijakisoma hicho kitabu cha "Refuting Isis" bado).
Na hao Isis na mfano wao, hawawakubali kabisa baadhi ya Wanachuoni uliowataja. Hawamkubali Shaykh Ibn Uthaymeen, Ibn Baaz, Albani (Allah awarehemu)wala Al-Fawzaan(Allah amhifadhi). Itakuwa huwajui vizuri hao.
Kuna tofauti kati ya Makhawaarij na Masalafi. Bahati nzuri Masalafi wenyewe hujipambanua kwa watu wao ni nani na Da'awah yao wanaifafanua.
Na mwisho kabisa, Masalafi kusema watu fulani ni Watu wa Bida'a wanafanya hivyo kwa dhulma? Na je watu wanaofanya shirki wakiambiwa kuwa wanafanya shirki wanaonewa? Ni makosa kusema hivyo? Mtu akifanya shirki hasa kiukweli na shirki yake ikakemewa ni makosa? Na kuhusu kuwatoa watu katika Uislam, katika watu wanaochunga mipaka, misingi na masharti mno katika kukufurisha, Masalafi wanaongoza. Ni waadilifu mno katika hili. Hutoona wakimkufurisha mtu maalum bila ya kufuata masharti ya Kishari'ah. Ajabu ni kwamba baadhi ya wanaowasingizia Masalafi kuwa wanawatoa watu katika Uislam (bila ya haki) nao hufanya hivyo hivyo, tena kwa ujinga au matamanio tu.
Nakukumbusha ndugu yangu post #10 ya uzi huu ulipomjibu mtu aliyesema kuhusu wanaojilipua, japo aliandika kuwakejeli Waislam, wewe ukasema "Huyo si Muislam!" Huko nako si kumtoa mtu katika Uislam? Ama mimi sijaelewa?
Ni hayo tu. Allah atuongoze sisi na wewe ndugu yangu
Hammaz Katika njia iliyonyooka.
Na Allah anajua zaidi.