Kwanini Wakenya siyo wajanja kwenye hili?

Kwanini Wakenya siyo wajanja kwenye hili?

Naziomba hizo takeimu
Kwanza Soma hio form mbona wanahitaji jina la ukoo? Hakuna nchi dunia nzima isiojua wananchi wake kwa idadi ya makabila.
IMG-20190814-WA0004.jpeg
 
Tofautisha kati ya nchi kutangaza kila kabila kwa idadi yao na kujaza taarifa binafsi kwenye fomu huko guest House na maeneo mengine ambayo hayana uhusiano na kuhesabu watu

Tanzania haipingi watu kuwa na makabila yao au kujivunia kabila lako ndio maana tunayo tamasha maarufu linaitwa URITHI FESTIVAL linakutanisha makabila yote huku kukiwa na ngoma, vyakula, mavazi, mila na desturi za kila kabila nchini na tamasha hilo linaendesha na serikali,

Tanzania haitaki kuendekeza ukabila mpaka kwenye kuhesabu idadi kwamba kabila a wapo kadhaa kabila b wapo kadhaa (unafanya hivyo ili iweje? Kwani kuna huduma yoyote serikali inatoa kikabila kwamba lazima wajue idadi ya wanufaika?)
1846491_1537002547819.png
Wacha ujinga wewe..yani unajisifia kutaja kabila lako unapoingia guest...naskia hata kuna form zingine hko pia unajaza mpka kabila lako...

Kisha mnakuja kujisifu hapa[emoji1787]
 
Nimejibu ila sio lazima nijibu kwa kutumia maneno mnayolazimishia, ukiwa na nia utaelewa, fahamu kwamba dodoso la sensa huandaliwa kisayansi, lengo na madhumuni ya kila swali humo huwa kwa ajili ya takwimu zinazosaidia kisayansi. Kuna tasnia mbali mbali ambazo hutumia kanzidata ya sensa kwenye maboresho ya kijamii.
Ndio sababu umeulizwa, taja tasnia moja inayotumia idadi ya watu katika makabila ya nchi. Ukiona watu wanatafuta idadi ya watu kwa kila kabila au dini, ujue ni wabaguzi, hakuna data yoyote ya kisayansi inayohitaji kujua idadi wa watu kwa misingi ya ukabila au dini.

Sensa imeanzia nchi zilizoendelea, huwezi kukuta nchi yoyote iliyostaarabika inayouliza kabila au dini ya mtu katika zoezi la sensa, hii ipo katika nchi chache sana duniani, na msingi wake ni ubaguzi, sio zaidi ya hapo.
 
Ndio sababu umeulizwa, taja tasnia moja inayotumia idadi ya watu katika makabila ya nchi. Ukiona watu wanatafuta idadi ya watu kwa kila kabila au dini, ujue ni wabaguzi, hakuna data yoyote ya kisayansi inayohitaji kujua idadi wa watu kwa misingi ya ukabila au dini.

Sensa imeanzia nchi zilizoendelea, huwezi kukuta nchi yoyote iliyostaarabika inayouliza kabila au dini ya mtu katika zoezi la sensa, hii ipo katika nchi chache sana duniani, na msingi wake ni ubaguzi, sio zaidi ya hapo.

Marekani wanauliza 'race' ya mtu, Black, White, Hispanic etc.
 
Marekani wanauliza 'race' ya mtu, Black, White, Hispanic etc.
Na ndio sababu wanarekani ni wabaguzi sana. Nilikua Europe kwa miaka kadhaa, wazungu wa Europe wanasema wamarekani ni tajiri lakini hawajaendelea, moja ya sababu hi hiyo na kuamini dini.
 
Back
Top Bottom