Kwanini wakoloni wameamua kutembelea makoloni yao kwa mpigo

Kinacho tokea Niger, Mali nk. Wanajihami yasije chukuliwa na Put In.
 
Ni muhimu sana dogo. Yanaingiza hela nyingi sana huko yaliko. Kumbe hujui antiquities.

Unadhani hela zinazoingia huko na nyie mtaingiza mkipewa hayo mamijusi na mafuvu 😅

Mbuga na milimi iliyopo haiperform hata nusu ya potential yake ndo mijusi na mafuvu yawape hela, wamatumbi bana 😂😂
 
Kuna mambo yanaendelea katika ulimwengu wa roho na sio kwa bahati mbaya haya mambo yanatokea.
 
Hizi ziara zipo mkakati zaidi hasa kuzima ushawishi wa China huku Africa.
 
Wanawasi tusiamke kama Bukinafaso with their brilliant leader ..hawajui huku mzungu anathaminiwa kuliko kitu chochote kile
 
Si mfaransa kayakorofisha makoloni yake hawataki hata kumuona.

Sasa jamaa hawa na kwa yanayoendelea duniani hivi sasa lazima kila mmoja aelewe mapema washirika na maadui zake. (allies and foes) ni kina nani.
 
Wamejifunza kupitia mapinduzi yanayotokea nchi za Afrika magharibi, raia wameonesha wazi wamechoka na hawataki mahusiano yasiyo na tija na mkoloni Ufaransa
 
Badala wajadili mambo ya msingi wanaomba kurudishiwa mafuvu na mijusi. Smh
Hicho kitu cha ajabu eti,mafuvu,mara watuombe msameha, kwa ajili ya ukoloni [emoji24][emoji24][emoji24] kind like stupidity
 
Viongozi wanaotawala nchi za Afrika, ukiacha SouthAfrica, hawana akili, ni wezi, wajinga,waongo, IQ, ndogo,
Tuanzie hapa, kwetu,tuna rais, hajawahi kusoma degree, lakini yupo bize kuzurura kutqfuta PHD za heshima!
Ana chama chenye vijana wengi wasomi, watu wenye heshima na upeo mkubwa wa ki uongozi, kitaifa na kimataifa,lakini kateua jizi, uaji,jitu lenye kashfa,kibao, lililodoji hata vyeti vya elimu, kuwa kiongozi,mkubwa kwenye chama!
Kama hio hqitoshi, serikali inatayarisha sherehe kusherehwkea kuanzishwa kwa mkoa! Singida!Sasa nchi inamikoa 26+, utafanya hizo birthday ngapi!??
So fucking stupid!
 
Unajua mi nahisi sijui utumwa unarudi maana ilianza hivi hivi walitangulia Waarabu kufanya biashara baadae wakaja wajerumani ..
Sasa hibi wameanza DPW-Waarabu kuwasafishia njia watabe waje watubebe kama mchele ..
 
Rais wa Ujerumani ni Mkuu wa nchi asiyena mamlaka ya Kidola wala kiserikali.

Chancellor ndiye Mkuu wa Serikali na Amiri Jeshi Mkuu
Yes Sir ,Under the 1949 constitution (Basic Law) Germany has a parliamentary system of government in which the chancellor (similar to a prime minister or minister-president in other parliamentary democracies) is the head of government.
 
Mkuu kwani waliondoka lini? Nauliza hivyo kwa sababu!

1. Lugha rasmi tunayo tumia kwenye mawasiliano muhimu ya ndani na kimataifa ni ya Kwao.

2. Mifumo ya uendeshaji serikali, Bunge na mahakama tunayotumia ni ya kwao

3. Tunaabudu kwa kutumia dini na vitabu vya imani zao.

4. Tunakopa fedha ya maendeleo yetu kutoka kwao.

5. Mifumo ya elimu na ajira ni ya kwao.

6. Mifumo ya uchumi, maendeleo na miundombinu tunayotumia ni ya kwao.

5. Fedha tunazotumia kuagiza vitu mbali mbali kimataifa ni ya kwao

7. Mifumo ya siasa, kidemokrasia na mitindo ya maisha ni ya kwao.

8. Teknolojia ya viwanda, usafirishaji, afya, makaazi na habari ni ya kwao.

9. Silaha, taratibu na mifumo ya usalama na ulinzi wa taifa ni ya kwao

10. Starehe, sanaa na muziki tunayoimba na kuburudishana ni ya kwao.

Mkuu hapo unasemaje wanarudi wakati hawakuondoka?
 
Vijana wa usalama ni ngumu mno kufikiri kama ulivyowaza mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…