Kwanini waliojaribu kutafutia suluhu ya mgogoro wa Israel na Palestina waliuawa?

Kwanini waliojaribu kutafutia suluhu ya mgogoro wa Israel na Palestina waliuawa?

Mpinzire

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2013
Posts
7,503
Reaction score
13,463
Kisa cha kwanza.
May 20, 1948 UN ilimteua Count Folke Bernadotte kuwa mpatanishi mkuu katika mgogoro wa Israel na Palestina.
1728373916021.png

Mapendekezo ya Count Folke Bernadotte
1. Kurejesha wakimbizi wa Kipalestina: wakimbizi wa Kipalestina waruhusiwe kurejea kwenye makazi yao au kulipwa fidia kwa mali zao zilizopotea.
2. Kurekebisha mipaka.
3. Kuiweka Yerusalemu chini ya udhibiti wa kimataifa.

Bernadotte aliuawa Sept 17, 1948 mjini Jerusalem na kundi la kiyahudi la Lehi ambalo lilikuwa linapinga mapendekezo yake.
Kundi la wanamgambo la Lehi lilikuwa linaongozwa na Yitzhak Shamir na Yitzhak Shamir alikuwa moja ya viongozi watatu waliopanga mauji ya Bernadotte.
1728373966183.png
Yitzhak Shamir mwaka 1973 alijiunga na chama cha mrengo wa kulia cha Likud na hatimae mwaka 1983 akawa Waziri Mkuu wa Israel.

Kisa cha Pili
Oslo Accords 1993
Aliyekuwa PM wa Israel Yitzhak Rabin na kiongozi wa Palestina na chama cha PLO Yasser Arafat walianzisha mazungumzo ya siri nchini Norway juu ya amani ya mataifa yao. na hatimae 1993 Oslo 1 ilisainiwa nchini Martekani na hatimae Oslo II ikasainiwa 1995 Taba - Egypt.
1728374523592.png

Oslo ilikuwa na mapendekezo kadhaa lakini haya matatu hayawakuwafulahisha Waisrael.
1. Kurejesha maeneo yaliyokaliwa:- Vikosi vya Israel kutoka ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharbi.
2. Kutambua PLO: Hii iliwakasirisha baadhi ya Waisraeli ambao waliona PLO kama kundi la kigaidi.
3. Haki ya kurejea kwa wakimbizi wa Kipalestina.

Oct 1994 Tuzo ya Nobel ya amani inatolewa kwa viongozi watatu.
1728376476710.png

Nov 4, 1995 mjini Tel- Aviv Waziri Mkuu wa Israel Yitzhak Rabin anauawa kwa kupigwa risasi na kijana Yigal Amir myahudi na mfuasi wa mrengo wa kulia aliepinga makubaliano ya Oslo.

Baada ya kuawa kwa Rabin na kijana wa kiyahudi, aliyekuwa Waziri wa mamo ya nje Shimon Peres ambaye pia alikuwa mmoja wa washindi wa tuzo ya Nobel anachaguliwa na chama cha Labour kumalizia mda wa Rabin mpaka uchaguzi mkuu wa 1996 ambapo Benjamon Netanyahu anakuja kuchukua Uwaziri Mkuu.
1728376991396.png

Benjamin Netanyahu ni mwanasiasa wa mrengo wa kulia wenye misimamo mikali na ni Waziri Mkuu wa Israel kwasasa kupitia chama cha Likud.

Chama cha Likud: Ni chama cha kisiasa cha mrengo wa kulia nchini Israel kilichoanzishwa mwaka 1973. Likud kinaunga mkono sera za soko huria, usalama wa taifa, na mara nyingi kimekuwa na msimamo mkali kuhusu masuala ya ardhi na makubaliano ya amani na Wapalestina.Chama hiki kimeongozwa na viongozi maarufu kama Menachem Begin, Yitzhak Shamir, Ariel Sharon, na Benjamin Netanyahu.

Chama cha Labour
ni chama cha siasa za mrengo wa kushoto nchini Israel, Kimekuwa kikijulikana kwa sera zake za kijamii na kiuchumi zinazolenga usawa na haki za kijamii. Labour kimekuwa kikihimiza mazungumzo ya amani na Wapalestina kama Oslo Accords I na II.

Chama hiki kimeongozwa na viongozi maarufu kama David Ben-Gurion, Golda Meir, Yitzhak Rabin, na Shimon Peres. Labour kimekuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za Israel, ingawa umaarufu wake umepungua kwasasa.

Unamuona nani kikwazo cha amani Mashariki ya Kati?
 
Unamuona nani kikwazo cha amani Mashariki ya Kati?
Umeegemea upande mmoja zaidi, kwa hapo, kwa kutegemea simulizi yako pekee(kujibu kulingana na simulizi yako), ni mwendawazimu pekee atakajibu tofauti na wewe unavyotarajia.

Ingekua vyema ungebalance mzani halafu ukauliza hilo swali lako la mwishoni hapo ..
 
Umeegemea upande mmoja zaidi, kwa hapo, kwa kutegemea simulizi yako pekee(kujibu kulingana na simulizi yako), ni mwendawazimu pekee atakajibu tofauti na wewe unavyotarajia.

Ingekua vyema ungebalance mzani halafu ukauliza hilo swali lako la mwishoni hapo ..
Ameambatanisha anqchokisema na evidence...... assassinations zte zilizofanywa kwa yyte aliyetaka kuweka mambo sawa aliliwa kichwa....unataka mzani gani zaidi....kwmba waliokataa mapendekezo ya amani walikuwa wavaa kobaz au waliowaua hao watoa mapendekezo ya amani walikuwa wavaa kobaz....unataka mzani upo yaqni
 
Pale hapatakuwa na suluhisho la kudumu
 
Umeegemea upande mmoja zaidi, kwa hapo, kwa kutegemea simulizi yako pekee(kujibu kulingana na simulizi yako), ni mwendawazimu pekee atakajibu tofauti na wewe unavyotarajia.

Ingekua vyema ungebalance mzani halafu ukauliza hilo swali lako la mwishoni hapo ..
Nambie wewe unamjua nani aliuawa na upande mwingine ambae alijaribu kusuruhisha mgogoro huu?
 
Nambie wewe unamjua nani aliuawa na upande mwingine ambae alijaribu kusuruhisha mgogoro huu?
Wote washari na hawataki amani, sio suala la nchi moja, walikubaliana kutuliia huyo unaesema anataka amani hata miezi 6 haikupita, Oct 7 akamlipua mwenzie.
 
Wote washari na hawataki amani, sio suala la nchi moja, walikubaliana kutuliia huyo unaesema anataka amani hata miezi 6 haikupita, Oct 7 akamlipua mwenzie.
Kwaiyo kikwazo ni yule ambae anapokonywa ardhi!
 
Utatulia wakati mapendekezo ya UN hayafuatwi na ule upande wa wanaojiona Wana nguvu??....kwhyo kule UN walivyosema Hawa taifa teule wanakalia maeneo ya watu kwa nguvu...wale wte wanawasingizia Hawa jamaa...kwmba wanawaonea wivu Hawa jamaa.....kadri muda unavyozidi kusogea hata Yale mataifa yaliyokuwa yanawaunga mkono baadhi wameshaanza kukaa mbali nao maana washaona Hawa jamaa ni nuksi na hawana akili sawasawa
Wote washari na hawataki amani, sio suala la nchi moja, walikubaliana kutuliia huyo unaesema anataka amani hata miezi 6 haikupita, Oct 7 akamlipua mwenzie
 
Utatulia wakati mapendekezo ya UN hayafuatwi na ule upande wa wanaojiona Wana nguvu??....kwhyo kule UN walivyosema Hawa taifa teule wanakalia maeneo ya watu kwa nguvu...wale wte wanawasingizia Hawa jamaa...kwmba wanawaonea wivu Hawa jamaa.....kadri muda unavyozidi kusogea hata Yale mataifa yaliyokuwa yanawaunga mkono baadhi wameshaanza kukaa mbali nao maana washaona Hawa jamaa ni nuksi na hawana akili sawasawa
Kabisa.
 
Kisa cha kwanza.
May 20, 1948 UN ilimteua Count Folke Bernadotte kuwa mpatanishi mkuu katika mgogoro wa Israel na Palestina.
View attachment 3118561
Mapendekezo ya Count Folke Bernadotte
1. Kurejesha wakimbizi wa Kipalestina: wakimbizi wa Kipalestina waruhusiwe kurejea kwenye makazi yao au kulipwa fidia kwa mali zao zilizopotea.
2. Kurekebisha mipaka.
3. Kuiweka Yerusalemu chini ya udhibiti wa kimataifa.

Bernadotte aliuawa Sept 17, 1948 mjini Jerusalem na kundi la kiyahudi la Lehi ambalo lilikuwa linapinga mapendekezo yake.
Kundi la wanamgambo la Lehi lilikuwa linaongozwa na Yitzhak Shamir na Yitzhak Shamir alikuwa moja ya viongozi watatu waliopanga mauji ya Bernadotte.
View attachment 3118562Yitzhak Shamir mwaka 1973 alijiunga na chama cha mrengo wa kulia cha Likud na hatimae mwaka 1983 akawa Waziri Mkuu wa Israel.

Kisa cha Pili
Oslo Accords 1993
Aliyekuwa PM wa Israel Yitzhak Rabin na kiongozi wa Palestina na chama cha PLO Yasser Arafat walianzisha mazungumzo ya siri nchini Norway juu ya amani ya mataifa yao. na hatimae 1993 Oslo 1 ilisainiwa nchini Martekani na hatimae Oslo II ikasainiwa 1995 Taba - Egypt.
View attachment 3118572
Oslo ilikuwa na mapendekezo kadhaa lakini haya matatu hayawakuwafulahisha Waisrael.
1. Kurejesha maeneo yaliyokaliwa:- Vikosi vya Israel kutoka ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharbi.
2. Kutambua PLO: Hii iliwakasirisha baadhi ya Waisraeli ambao waliona PLO kama kundi la kigaidi.
3. Haki ya kurejea kwa wakimbizi wa Kipalestina.

Oct 1994 Tuzo ya Nobel ya amani inatolewa kwa viongozi watatu.
View attachment 3118620
Nov 4, 1995 mjini Tel- Aviv Waziri Mkuu wa Israel Yitzhak Rabin anauawa kwa kupigwa risasi na kijana Yigal Amir myahudi na mfuasi wa mrengo wa kulia aliepinga makubaliano ya Oslo.

Baada ya kuawa kwa Rabin na kijana wa kiyahudi, aliyekuwa Waziri wa mamo ya nje Shimon Peres ambaye pia alikuwa mmoja wa washindi wa tuzo ya Nobel anachaguliwa na chama cha Labour kumalizia mda wa Rabin mpaka uchaguzi mkuu wa 1996 ambapo Benjamon Netanyahu anakuja kuchukua Uwaziri Mkuu.
View attachment 3118626
Benjamin Netanyahu ni mwanasiasa wa mrengo wa kulia wenye misimamo mikali na ni Waziri Mkuu wa Israel kwasasa kupitia chama cha Likud.

Chama cha Likud: Ni chama cha kisiasa cha mrengo wa kulia nchini Israel kilichoanzishwa mwaka 1973. Likud kinaunga mkono sera za soko huria, usalama wa taifa, na mara nyingi kimekuwa na msimamo mkali kuhusu masuala ya ardhi na makubaliano ya amani na Wapalestina.Chama hiki kimeongozwa na viongozi maarufu kama Menachem Begin, Yitzhak Shamir, Ariel Sharon, na Benjamin Netanyahu.

Chama cha Labour
ni chama cha siasa za mrengo wa kushoto nchini Israel, Kimekuwa kikijulikana kwa sera zake za kijamii na kiuchumi zinazolenga usawa na haki za kijamii. Labour kimekuwa kikihimiza mazungumzo ya amani na Wapalestina kama Oslo Accords I na II.

Chama hiki kimeongozwa na viongozi maarufu kama David Ben-Gurion, Golda Meir, Yitzhak Rabin, na Shimon Peres. Labour kimekuwa na ushawishi mkubwa katika siasa za Israel, ingawa umaarufu wake umepungua kwasasa.

Unamuona nani kikwazo cha amani Mashariki ya Kati?

Umesahau kuhusu upande wa pili.. mgogoro huo ni two way trafick.. upande wa palestina kuna watu wanafaidika nao.. Yasser arafat aliuawa.. nenda youtube utakuta aljazera wana documentray inaelezea had kesi aliofungua mkewe na kupelekea mwili wake kufukuliwa kufanyiwa vipimo ikagundulika ulikuwa na sumu..

Cha ajabu arafat alikuwa na ulinzi mkali sana katika watu wake ,chakula chake kilikuwa kinaonjwa na watu wa tatu.. ila aliwekewa sumu.. ajabu la pili mkewe aliekuwa akiishi ufaransa alifungua kesi palestina akitaka uchunguz wa kifo cha mumewe akapigwa ban na viongoz wa palestina akiwemo Abbas.. ilibidi afungue kesi mahakama ya kimataifa france kuishinikiza palestina ikubali.. ndio mwili ukafukuliwa na uchunguz ukafanyika. Matokeo ikajulikana una sumu.. ain ya sumu ni ambayo Israel wanapenda kuitumia.. inaua taratibu ila humaliz wiki kadhaa

Swali je hiyo sumu ulifikaje kwenye Mwili wa yasser araft.. na kumbuka kipindi hicho ndio Islamic brotherhood wanaanza kuota mizizi ndan ya palestina na wao na upande wa Arafat walikuwa hawaelewan sababu ideology zao tofauti. Arafat anataka suluhu ya two state. islamic brotherhood a.k.a Hamas wanataka single islamic state na jews wote wawe eliminated

Kuna consipiracy inayoelea kuwa arafat aliwekewa sumu na mamluki wa Kipalestina aliopewa na upande israel ambao na wao una itikadi kali .. ndio hao kina nyau.

Kwa hiyi utaona pande zote mbili kuna wahafidhina ambao wana misimamo ya kigaidi na mbaya zaidi sasa hv wote wako at the helm "ndio utawala" huku israel kina nyau na wenzie kule palestina hamas lebanon wako hizbo. Yemen wako houthi.. iran yeye anatake advantage ya kisiasa anataka advantage ya ukolon mamboleo awe ana foot print zake .. aweke puppet govt middle east. Maana sasa hivi hii ndio game Plan dunian. Kuwa na proxy govt

So pande zote mbili kuna makundi yanadhoofisha amani hapo middle east
 
Umesahau kuhusu upande wa pili.. mgogoro huo ni two way trafick.. upande wa palestina kuna watu wanafaidika nao.. Yasser arafat aliuawa.. nenda youtube utakuta aljazera wana documentray inaelezea had kesi aliofungua mkewe na kupelekea mwili wake kufukuliwa kufanyiwa vipimo ikagundulika ulikuwa na sumu..

Cha ajabu arafat alikuwa na ulinzi mkali sana katika watu wake ,chakula chake kilikuwa kinaonjwa na watu wa tatu.. ila aliwekewa sumu.. ajabu la pili mkewe aliekuwa akiishi ufaransa alifungua kesi palestina akitaka uchunguz wa kifo cha mumewe akapigwa ban na viongoz wa palestina akiwemo Abbas.. ilibidi afungue kesi mahakama ya kimataifa france kuishinikiza palestina ikubali.. ndio mwili ukafukuliwa na uchunguz ukafanyika. Matokeo ikajulikana una sumu.. ain ya sumu ni ambayo Israel wanapenda kuitumia.. inaua taratibu ila humaliz wiki kadhaa

Swali je hiyo sumu ulifikaje kwenye Mwili wa yasser araft.. na kumbuka kipindi hicho ndio Islamic brotherhood wanaanza kuota mizizi ndan ya palestina na wao na upande wa Arafat walikuwa hawaelewan sababu ideology zao tofauti. Arafat anataka suluhu ya two state. islamic brotherhood a.k.a Hamas wanataka single islamic state na jews wote wawe eliminated

Kuna consipiracy inayoelea kuwa arafat aliwekewa sumu na mamluki wa Kipalestina aliopewa na upande israel ambao na wao una itikadi kali .. ndio hao kina nyau.

Kwa hiyi utaona pande zote mbili kuna wahafidhina ambao wana misimamo ya kigaidi na mbaya zaidi sasa hv wote wako at the helm "ndio utawala" huku israel kina nyau na wenzie kule palestina hamas lebanon wako hizbo. Yemen wako houthi.. iran yeye anatake advantage ya kisiasa anataka advantage ya ukolon mamboleo awe ana foot print zake .. aweke puppet govt middle east. Maana sasa hivi hii ndio game Plan dunian. Kuwa na proxy govt

So pande zote mbili kuna makundi yanadhoofisha amani hapo middle east
Hakuna ushahidi wa moja kwa moja kuwa Yassir Arafat aliuawa kwani ata timu ya uchunguzi ilipishana katika taarifa waliyotoa japo kweli wote walikiri kua mwili wa Yassir ulikuwa na kiwango cha Sumu ya mionzi, timu iliyoundwa kuchunguza mwili ilikuwa ya mataifa ma3 Ufaransa, Switzerland pamoja na Russia ila Switzerland ndiyo walitia shakha juu ya Sumu kuwa ndiyo chanzo cha kifo huku Ufaransa na Russia wakikiri kuwa kweli mwili ulikuwa na Sumu ila Sumu wao walisema sumu hiyo haikuwa katika kiwango cha kusababisha kifo hiko.
 
Back
Top Bottom