Kwanini wanasiasa wengi wa Afrika wanatofautiana kimaono na wanaowaongoza/wananchi?

Kwanini wanasiasa wengi wa Afrika wanatofautiana kimaono na wanaowaongoza/wananchi?

Heart Wood.

JF-Expert Member
Joined
Nov 16, 2014
Posts
982
Reaction score
1,179
Wakuu,

Mie sipendi tubishane sana. Wala si kwamba naleta mambo ya ujuaji kiviiile.

Ukiachana na watu wachache wenye kusifia kila jambo, kama unataka kuamini we ulizia watu 10 hapo mtaani kwenu ni kwa kiwango gani wanaridhika na uongozi wa viongozi wao. Kisha waulize wao wangependa viongozi wao wafanye mambo gani haswa? Bila shaka majibu utakayopata yatakushangaza. Yaani ni kama mbigu na ardhi.

Mfano mzuri: Japo wanasiasa wengi wa Africa hukimbilia kusema vijana wanatumiwa na mashirika ya nje kila vijana wanapopaza sauti zao, ila jaribu kujiuliza ni kwanini Ruto aliamua kufutilia mbali ule mswada baada ya maandamano na si yeye mwenyewe kujua kuwa ule mswada haukufaa hata vijana walipopaza sauti zao kabla ya maandamano?

Mfano mwingine tukisalia hapohapo Kenya, vijana wanadai baadhi ya Mawaziri waliorudishwa ( ambao walikuwepo hapo kabla)hawafai na walitaka mawaziri wapungue kwa idadi ila kupunguza matumizi ya anasa, ila Ruto ameshupaza shingo na kuendelea kufanya atakavyo. Japo nampongeza kwa machache aliyofanya.

Huku mitaani kwetu ukitembelea vijiweni utasikia watu wa kawaida wana maono makubwa sana kuhusu nchi yao na vile wangependa ienende, ila uhalisia ni tofauti kabisa na kinachofanyika.

Watu wana malalamiko kuhusu:

Ufisadi
Rushwa
Kujuana (connection)
Uhaba wa ajira uliopitiliza
Matumizi ya anasa ya pesa za umma
Huduma za elimu, afya za kusuasua n.k

We jiulize tu, hivi kwanini sekta binafsi zinahuduma bora kuliko sekta za umma kwenye elimu, afya n.k? Je, ni kweli Serikali haina fedha za kuwezesha huduma bora kama wafanyavyo Private sectors?

Sasa swali langu, hivi ni kwanini viongozi huwa hawana uwezo wa kutenda kama Wananchi wanavyopenda?

,Inamana kiti cha uongozi ukishakikalia unakuwa unaona tofauti kabisa na waonavyo unaowaongoza au inakuwaje Wakuu?

Mie ningekuwa Kiongozi Mkubwa:

1) Ningekuwa nafanya mpango wa kukusanya maoni na hoja za wananchi nao waongoza angalau kila baada ya mwezi mmoja
2) Baada ya kukusanya maoni na matakwa yao, ningekuwa nafanya analysis juu ya mawazo hayo na kuitisha mjadala wa kitaifa ambako tungejadili suala moja baada ya lingine, yaani hoja kwa hoja.
3) Kisha ningekuwa natoa mrejesho juu ya maoni ya wananchi na nini Seerikali itafanya/ inachofanya..

Haha ha haaa. Huenda haya ni mawazo fyatu lakini mwenyewe sina uhakika ya niwazacho.
 
Sababu ni kwamba Afrika hakuna viongozi, kuna wachumia tumbo (wapora mali). In Africa there are no leaders but looters.

Ndiyo maana hawafuati misingi ya uongozi wa kuwasikiliza wanaowaongoza.
 
Sababu ni kwamba hakuna viongozi, kuna wachumia tumbo (wapora mali). In Africa there are no leaders but looters.
Sasa hawa viongozi si ni jamaa na ndugu zetu? Kwanini watufanyie hivyo lakini? Kwani wametoka wapi wao? Si hapahapa kwetu?
 
Ndio tunapata ile tafsiri, Akili ndogo inaongoza akili kubwa.
Lakini Mkuu ukumbuke viongozi wakubwa wamezungukwa na Think tanks wengi. Inakuwaje wasiwe na ufahamu wa mambo ya muhimu? Huku mitaani hata watu ambao hawajanda sana shule ukiwasikia wanavyoelezea kuhusu nchi yao utashangaa sana. Mfano masuala ya rushwa, connection, n.k.
 
Mabadiliko huwa yanaletwa na watu wachache hii ni dunia nzima.

Hata katika familia unaweza kuzaa watoto 10 Ila mmoja ndo akaleta mabadiliko.

So in Africa wale thinkers (Visionary) huwa hawapendi siasa na huwa hawapendi uongo so sio rahisi uawakute wanapambania vyeo vya kisiasa.

Hivyo jambo la msingi na muhimu ni kuwatunza (Thinkers) na kuwa well treated.

Fewers can bring changes to the Masses but masses can fail to bring changes to the fewers .

Hii perspective ipo katika black family mama analea watoto 09 Ila watoto tisa wanashindwa kumuhudumia mama mmoja that is hell.
 
Lakini Mkuu ukumbuke viongozi wakubwa wamezungukwa na Think tanks wengi. Inakuwaje wasiwe na ufahamu wa mambo ya muhimu? Huku mitaani hata watu ambao hawajanda sana shule ukiwasikia wanavyoelezea kuhusu nchi yao utashangaa sana. Mfano masuala ya rushwa, connection, n.k...
Hawapewi room ya kushauri, serikalini kumejaa majungu na wasaka fursa kuliko watendaji
 
Mabadiliko huwa yanaletwa na watu wachache hii ni dunia nzima.

Hata katika familia unaweza kuzaa watoto 10 Ila mmoja ndo akaleta mabadiliko.

So in Africa wale thinkers (Visionary) huwa hawapendi siasa na huwa hawapendi uongo so sio rahisi uawakute wanapambania vyeo vya kisiasa.

Hivyo jambo la msingi na muhimu ni kuwatunza (Thinkers) na kuwa well treated.

Fewers can bring changes to the Masses but masses can fail to bring changes to the fewers .

Hii perspective ipo katika black family mama analea watoto 09 Ila watoto tisa wanashindwa kumuhudumia mama mmoja that is hell.
Hawasikilizwi wala hawatumiwi wanaotumiwa ni makada na chawa
 
Mitizamo ya wanasiasa na wananchi ni ya aina Moja, nipate cheo nipige pesa nikae pembeni. Hao wanasiasa ni miongoni mwetu wametoka kwenye jamii zetu.
Jamii positive inazaa wanasiasa positive ende vaisi vesa izi tru
 
Mitizamo ya wanasiasa na wananchi ni ya aina Moja, nipate cheo nipige pesa nikae pembeni. Hao wanasiasa ni miongoni mwetu wametoka kwenye jamii zetu.
Jamii positive inazaa wanasiasa positive ende vaisi vesa izi tru
Kwahiyo kumbe shida ipo kwenye DNA zetu? Kwahiyo tuache kulalamika au sio? Maana kila atakayepata nafasi anawaza kupiga na kuvunia tumboni kwake..
 
Kwahiyo kumbe shida ipo kwenye DNA zetu? Kwahiyo tuache kulalamika au sio? Maana kila atakayepata nafasi anawaza kupiga na kuvunia tumboni kwake..
Ndio kaka.... Angalia Sasa muda wa uchaguzi mtu anatumia pesa kupata uongozi.. Hauoni kama Kuna shida Hapa Kwa wanajamii. Hivi jamii positive inaweza kupata kiongozi Kwa msaada wa rushwa.?
 
Ndio kaka.... Angalia Sasa muda wa uchaguzi mtu anatumia pesa kupata uongozi.. Hauoni kama Kuna shida Hapa Kwa wanajamii. Hivi jamii positive inaweza kupata kiongozi Kwa msaada wa rushwa.?
Unashaurije Mkuu. Tusishupaze shingo zetu kuwashambulia walioko kwenye nafasi maana Miafrika ndilivyo tulivyo au tujitahidi kupaza sauti za kutaka mabadiliko kwenye jamii?
 
Unashaurije Mkuu. Tusishupaze shingo zetu kuwashambulia walioko kwenye nafasi maana Miafrika ndilivyo tulivyo au tujitahidi kupaza sauti za kutaka mabadiliko kwenye jamii?
Ndio kaka. Tubadirishe kwanza mitazamo ya jamii, hasa hili la kuona kwamba kupata uongozi ndio nafasi ya kujinufaisha badala ya kulitumikia taifa. Jamii lazima ibadilike ingawa hili litachukua miaka mingi sana. Ila jamii ndio kiongozi na kiongozi ndio jamii. Kaka samaki huanza kuoza kichwani
 
Sababu ni moja tu:

Hao wenye maono wamekaa kijiweni. Wanasubiri kuteuliwa ama kuajiriwa. Kazi yao kubwa ni kuongea zaidi kuliko vitendo. Hivyo kulalama na kulaumu bila kuchoka. Afrika karibu yote ina asili ya watu wa aina hii.

Na huu ndio msingi wa ujio wa Mtandao wa Wafuasi Binafsi wa Rais; ambapo inampa kila mmoja jukwaa walau kujitolea kwa ajili ya Taifa lake vile anavyoona ina msaada kwenye nchi.

Hili la kujitolea ni kwa niaba ya Rais wa nchi ambaye ndio kiongozi mkuu wa wananchi wote.
 
Wakuu,

Mie sipendi tubishane sana. Wala si kwamba naleta mambo ya ujuaji kiviiile.

Ukiachana na watu wachache wenye kusifia kila jambo, kama unataka kuamini we ulizia watu 10 hapo mtaani kwenu ni kwa kiwango gani wanaridhika na uongozi wa viongozi wao. Kisha waulize wao wangependa viongozi wao wafanye mambo gani haswa? Bila shaka majibu utakayopata yatakushangaza. Yaani ni kama mbigu na ardhi.

Mfano mzuri: Japo wanasiasa wengi wa Africa hukimbilia kusema vijana wanatumiwa na mashirika ya nje kila vijana wanapopaza sauti zao, ila jaribu kujiuliza ni kwanini Ruto aliamua kufutilia mbali ule mswada baada ya maandamano na si yeye mwenyewe kujua kuwa ule mswada haukufaa hata vijana walipopaza sauti zao kabla ya maandamano?

Mfano mwingine tukisalia hapohapo Kenya, vijana wanadai baadhi ya Mawaziri waliorudishwa ( ambao walikuwepo hapo kabla)hawafai na walitaka mawaziri wapungue kwa idadi ila kupunguza matumizi ya anasa, ila Ruto ameshupaza shingo na kuendelea kufanya atakavyo. Japo nampongeza kwa machache aliyofanya.

Huku mitaani kwetu ukitembelea vijiweni utasikia watu wa kawaida wana maono makubwa sana kuhusu nchi yao na vile wangependa ienende, ila uhalisia ni tofauti kabisa na kinachofanyika.

Watu wana malalamiko kuhusu:

Ufisadi
Rushwa
Kujuana (connection)
Uhaba wa ajira uliopitiliza
Matumizi ya anasa ya pesa za umma
Huduma za elimu, afya za kusuasua n.k

We jiulize tu, hivi kwanini sekta binafsi zinahuduma bora kuliko sekta za umma kwenye elimu, afya n.k? Je, ni kweli Serikali haina fedha za kuwezesha huduma bora kama wafanyavyo Private sectors?

Sasa swali langu, hivi ni kwanini viongozi huwa hawana uwezo wa kutenda kama Wananchi wanavyopenda?

,Inamana kiti cha uongozi ukishakikalia unakuwa unaona tofauti kabisa na waonavyo unaowaongoza au inakuwaje Wakuu?

Mie ningekuwa Kiongozi Mkubwa:

1) Ningekuwa nafanya mpango wa kukusanya maoni na hoja za wananchi nao waongoza angalau kila baada ya mwezi mmoja
2) Baada ya kukusanya maoni na matakwa yao, ningekuwa nafanya analysis juu ya mawazo hayo na kuitisha mjadala wa kitaifa ambako tungejadili suala moja baada ya lingine, yaani hoja kwa hoja.
3) Kisha ningekuwa natoa mrejesho juu ya maoni ya wananchi na nini Seerikali itafanya/ inachofanya..

Haha ha haaa. Huenda haya ni mawazo fyatu lakini mwenyewe sina uhakika ya niwazacho.
Noted
 
Wanasiasa ni wachumia tumbo
Unaweza kudhani hivyo kwa urahisi. Lakini chimbuko la hili ni kukosekana kwa uwajibikaji wa wananchi wenyewe kwa ajili ya Taifa lao.

Laiti wananchi wenyewe wangekuwa ni wawajibika wazuri wa Taifa lao kusingekuwepo kiongozi yeyote wa kisiasa ambaye angethubutu kulichezea Taifa hili kwa sababu anafahamu wazi nini atakachokipata kwa wananchi wapenda nchi yao.
 
Back
Top Bottom