Kwanini wanaume wasasa wamekalia malalamiko na kusahau nafasi na majukumu yao kama vichwa vya familia?

Kwanini wanaume wasasa wamekalia malalamiko na kusahau nafasi na majukumu yao kama vichwa vya familia?

Hebu nikuulize tu swali?!

Unaweza kutuelimisha huu umati mambo yafuatayo;

1. Nini maana ya neno haki?!
2. Mwanamke ana haki zipi?! Tuandikie zote tafadhali tujifunze.
3. Ni haki zipi kati ya hizo ulizosema ambazo wanawake wananyimwa hapa Tanzania au duniani na ni mazingira yapi huwa wananyimwa.
maswali konki
 
Mleta mada ndoa ni kama niche,everybody should play his/her role. Nadhani wewe ni msomi tena mwanasayansi,sidhani kama kuna kitu kinaitwa 50/50 kwenye niches,the same to marriages,let the nature take it’s course and things will be easier for both of you.
 
Kamwe sikio haliwezi zidi kichwa..

Mwanaume kutimiza majukumu yake huwa inategemea upande wapili mke, mwanaume anahitaji msaidizi(mke) anaejitambua mwenye adabu, heshima na unyeyekevu kwa mume wake, mambo ya kumtunishia kifua mwanaume usitegemee familia kuwa na amani na kuyafanya majukumu yake vizuri

Huyu Uzi wake haueleweki.Afu wao wanadhanigi majukumu ni kuwapa hela tuu, wakiweza kuzishika zao watajiita masupa wumani hapoo, utasikia nalea mwenyewe mwanangu, mwisho tunaona ongezeko la watoto vituko mtaani! Nyambaf
 
Mkuu hawa walokuwa so active kwenye huu uzi.Wenye kutambua majukumu yao wanajieleza na wametulia.

Nikupe heshima yako kwanza!
Shikamoo babu @aspirin long time no see!
Sweetheart... hivi si unajua pa kunipata ukinimisi?

Au nikuelekeze?

Marahaba naihifadhi kwa muda....
 
" ..... hilo halina discussion..." yaani matumizi yako ya maneno yanaonyesha we ni mwanamke wa namna gani. Jamaa yetu ana kazi sana. Ila una option ya kutafta mwanaume unayetaka wewe awe unavyotaka maana kama ndoa yako unaona haina furaha nikuhakikishie tu kuna ndoa zina furaha saaaana .
Mimi sikuja kuongelea ndoa yangu ila jinsi ya kuboresha maisha ya wanandoa kwa kusaidiana.Wewe kama njia unayotumia inafanya kazi kwako then hakuna shida lakini huna mamlaka ya kuhukumu kuhusu ndoa yangu!
 
Maishani napenda Sana nikutane na wanawake sampuli hi ila siwapati ili niwafundishe kwa vitendo maana ya 50/50 .....ila naishia kupata wife material tu hivyo kujikuta nakua mpole tu.....I wish mtoa maada ungekuja maishani mwangu Kama miaka miwili hivi nikufundishe kitu
 
Maishani napenda Sana nikutane na wanawake sampuli hi ila siwapati ili niwafundishe kwa vitendo maana ya 50/50 .....ila naishia kupata wife material tu hivyo kujikuta nakua mpole tu.....I wish mtoa maada ungekuja maishani mwangu Kama miaka miwili hivi nikufundishe kitu
Ni vizuri kama ungetupa ufafanuzi ili na wengine wanufaike hasa vijana wa sasa!
 
Wanaume wa sasa mna matatizo gani haswa maana sielewi tatizo lenu ni kwamba hamtaki mabadiliko au akili zimeelemea kwenye mfumo dume au ni nini hasa?Hamna lilo la kheri kwenu,wanaume hamuishi malalamiko mnaongea hata kuwazidi wanawake, maana najua mwanamke ni itikadi yake kupenda kuongea.

Wanaume nyinyi wa karne hii mnataka mtu kama bibi zetu(kitabia na anavyojiweka) na wakati huohuo mnataka mwanamke aliyeelimika,mpenda maendeleo,mchapa kazi n.k ili musaidiane majukumu.

Mnasahau kama bibi zetu jukumu lake kubwa lilikuwa kujenga familia.Kama mwanamke anaingiza kipato kama ww au ikiwezekana kukuzidi wewe mwanaume usitegemee upewe treatment na mwaka 47 lazima mfumo mzima wa maisha ubadilike!
Hii ni 2021 inabidi mubadilike muendane na wakati uliopo waungwana!

Ninachojiuliza hasa ni kwamba mna hofu mkiwa na mwanamke aliyeelimika atawapa changamoto nyingi kwasababu amepambazuka akili na ana upeo wa kufikiri tofauti na ambaye hana elimu?na hamtoweza kumwambia lolote tu akubali bila kutaka kujua kwanini?
Je hilo litapunguza heshima kwenu au litaondoa uanaume wenu?

Tusisahau pia wanawake haohao wachapakazi ndo wanaozaa na kujenga familia kumaanisha wanabeba mzigo mzito kuliko hata wa mwaka 47!

Tuchukulie women empowerment ni kitu chenye manufaa kwa mwanamke na mwanaume na tuache kukandamiza wanawake kwasababu wamepata sauti na kuerevuka!

Tafadhali nahitaji michango ya watu mnaojielewa.Ahsanteni na karibuni!
Naomba niwe tofauti kidogo na mtazamo wako ila nafurahi kuona kwamba unatambua kuwa tulivyoumbwa tunatofautiana nikiwa na maana wanaume wengi si wazungumzaji na hii ndivyo tulivyo ambapo ni kinyume kwa wanawake sasa hapa ndipo tatizo uanza mwanaume anavumilia na kukaa na jambo muda mrefu na kutokana na tabia za wanawake kuwa wepesi kuongea anapokuwa na mafanikio kidogo inakuwa tabu na sasa wamefika mbali pa kujaribu kutulinganisha kwamba sisi tuko sawa wanasahau kuwa unaweza pata madaraka yoyote yale duniani wakitaka lakini cheo kimoja ambacho ni mume kamwe hawawezi kukipata na ukilazimisha ndipo matatizo mengi yanapoanzia,Majukumu ya mume ni mengi sana na ndio maana akaitwa kichwa cha familia sasa wanawake utaka cheo icho hapo hakuna mwaume anayeweza kuvumilia na ndipo sasa mizozo mingi inapoanza na familia kusambaratika na hili neno mfume dume linawadanganya kwani kipindi mfumo dume ulikuwa unafanya kazi ndio familia nyingi zilidumu chukuilia mfano wa wazazi wetu leo hii tunapinga mfumo huo ndoa changa kabisa zinasambaratika, Tujitafakari tulipotoka na tujifunze kutoka kwa wazazi wetu waliheshimiana kwa kuwa wake zao walikuwa wanawaheshimu tofauti sana na sasa na jambo baya sana ambalo wanawake wa sasa wanalifanya ni hili la kuwazoesha watoto wao kwa familia zao na kuwatenganisha kabisa watoto na familia za waume zao hili nalo nimeona linawafanya wanaume wapunguze mapenzi kwa wake zao wewe kila upatapo nafasi unawapeleka watoto kwenu ebu fikiria siku moja mumeo akaitwa na wazazi wake halafu anakukuta wewe uko unawasaidia na watoto wako kwa babu yao inakuwa ni faraja kwake.
 
Wanawake wanadhani wanaume wanaogopa challenge kuhusu wanawake waliosoma ila ukweli wenyewe wanaume wanaogopa stress za wanawake waliosomA.

Kaa na wanaume waliooa wanawake waliosoma wengi wao wana msongo wa mawazo hawana furaha kwenye nyuso zao..

Elimu ya mwanamke haimsumbui sana mwanaume ila ujuaji ,dharau ulimbukeni wa mwanamke aliyesoma ndio tatizo kubwa.

Wengi wa waliooa wanawake waliosoma wanapitia unnecessary sterss,hawajivunii ile kuwa na mke km ambavyo wanaume wengine wanajivunia..

Kuna raha ya kuwa na mke lakini wengi wa waliooa wanawake wasomi hawawezi wakakwambia kwa marefu na mapana raha ya kuwa na mke sababu Hawaijui na hawajawahi ku experience hiyo raha ya kuoa.

Mwanaume anaoa ili kupata sex na kupunguza msongo wa mawazo.Maisha ya mwanaume ni stress tu..

Hapa sijazungumzia 25% ya wanawake waliosoma ambao wapo humble maana ukimpata huyo utaiona mbingu duniani.
 
Labda uniambie huko vijijini..ila mjini kama daslam babu tutakuwa tunadanganyana..Wanawake ni dependants sana kwa wanaume.
Mwanamke anayetaka kila kitu afanyiwe na mwanaume anajisifu anapambana🤣🤣🤣!!!

Mwanamke ambaye ana kaduka ka kuuza nguo au kaduka ka mapochi sinza anaesikilizia booster ya kodi itoke kwa danga maana biashara anayofanya ni show off tu ila huko mitandaoni na kwenye jamii anaonekana ni superwoman!

Hawa wanawake wanatuona sisi mafala eeh?🤣🤣🤣
 
Haki ambazo wanawake wanadai ndo zipi?
Za kutumia hela ya mwanaume by 100% na kumtegemea katika maisha yake ya kila siku kama mashine ya kumtatulia matatizo yake!

Ila pia wapewe access ya kutafuta hela zao wakitaka bila kubanwa kama jinsi wanaume wanavyotafuta ila hizo hela zao zisiguswe kwa namna yeyote ile maana ni zao!

Msingi wote wa mtoa mada upo hapa ila kazunguka zunguka tu bila mpango kwa kugeuzia lawama kwa wanaume ambao wameamua kujiengua kwenye huo unyonyaji kwa kuwapa jina kuwa ni walalamikaji!
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Back
Top Bottom