Kwanini wanaume wasasa wamekalia malalamiko na kusahau nafasi na majukumu yao kama vichwa vya familia?

Kwanini wanaume wasasa wamekalia malalamiko na kusahau nafasi na majukumu yao kama vichwa vya familia?

Wanaume wa sasa mna matatizo gani haswa maana sielewi tatizo lenu ni kwamba hamtaki mabadiliko au akili zimeelemea kwenye mfumo dume au ni nini hasa?Hamna lilo la kheri kwenu,wanaume hamuishi malalamiko mnaongea hata kuwazidi wanawake, maana najua mwanamke ni itikadi yake kupenda kuongea.

Wanaume nyinyi wa karne hii mnataka mtu kama bibi zetu(kitabia na anavyojiweka) na wakati huohuo mnataka mwanamke aliyeelimika,mpenda maendeleo,mchapa kazi n.k ili musaidiane majukumu.
Mnasahau kama bibi zetu jukumu lake kubwa lilikuwa kujenga familia.Kama mwanamke anaingiza kipato kama ww au ikiwezekana kukuzidi wewe mwanaume usitegemee upewe treatment na mwaka 47 lazima mfumo mzima wa maisha ubadilike!
Hii ni 2021 inabidi mubadilike muendane na wakati uliopo waungwana!

Ninachojiuliza hasa ni kwamba mna hofu mkiwa na mwanamke aliyeelimika atawapa changamoto nyingi kwasababu amepambazuka akili na ana upeo wa kufikiri tofauti na ambaye hana elimu?na hamtoweza kumwambia lolote tu akubali bila kutaka kujua kwanini?
Je hilo litapunguza heshima kwenu au litaondoa uanaume wenu?

Tusisahau pia wanawake haohao wachapakazi ndo wanaozaa na kujenga familia kumaanisha wanabeba mzigo mzito kuliko hata wa mwaka 47!

Tuchukulie women empowerment ni kitu chenye manufaa kwa mwanamke na mwanaume na tuache kukandamiza wanawake kwasababu wamepata sauti na kuerevuka!

Tafadhali nahitaji michango ya watu mnaojielewa.Ahsanteni na karibuni!
Sema tu shida yako ni uwe unachungulia wallet yangu kila saa. Ova
 
dah nimecheka sana
naona umegusa maslahi yetu ndo maana umeshambuliwa sana
umetumia muda mwingi kutetea hoja badala ya kujenga hoja hiyo ina maanaisha hoja zako zina mapungufu
 
Nadhani huu uzi unawakera hasa wanaume ninaowaongelea!

Mwanamke huyohuyo anayekuwa na majukumu 50/50 anabeba ujauzito huku anafanya kazi na ahudumie mumewe na familia na mazagazaga yote yanayokuja anayabeba unataka kuniambia hivo havina maana?

Hio tafsiri ya kwenye usawa kwenye sex umeitolea wapi mkuu?usiende out of topic na kuanza kuleta dhihaka!
aisee bora ufuge ng'ombe kuliko kuwa na wewe
yaani hadi kubeba mimba unaona unaonewa
50/50 bado unasema unamuhudumia mume
hivi unaelewa unachoandika
moja ya madhara ya demokrasia ni haya
unaandika pumba kisha unatetea mashudu
 
Wanaume nyinyi wa karne hii mnataka mtu kama bibi zetu(kitabia na anavyojiweka) na wakati huohuo mnataka mwanamke aliyeelimika,mpenda maendeleo,mchapa kazi n.k ili musaidiane majukumu.
Ngoja nitoke na hii nukta.

Mwanamke aliye elimika ana sifa gani,naomba uwasemee hao wadau.

Hao wanaume wa karne hii wanamuelezea vipi mwanamke mchapa kazi na mpenda maendeleo ?

Ninasema mimi Zurri ya kuwa :
Katika kitu ambacho huwa nawashangaa vijana wenzangu wa kiume ni wao kujilinganisha na watoto wa kike,wanaishi na haya mawazo ya kura veto na makongamano kwamba kusaidiana katika majukumu. Hivi tangu lini mwanamke akafanana sawa kimajukumu na sisi ? Kwanza tu kimaumbile hatufanani.

Mwanamke kiasili ni wakukaa nyumbani na kulea watoto,asubiri aletewe huu ndiyo usawa na wale waote wanao enda kinyume na hii kanuni habari wanayo,wanaugulia maumivu kimya kimya.

Nipo ....
 
aisee bora ufuge ng'ombe kuliko kuwa na wewe
yaani hadi kubeba mimba unaona unaonewa
50/50 bado unasema unamuhudumia mume
hivi unaelewa unachoandika
moja ya madhara ya demokrasia ni haya
unaandika pumba kisha unatetea mashudu
Tangu dunia inaumbwa sijapata kuona wanawake wajinga kama hawa wa kuanzia karne ya 19 mpaka hii 21. Sababu huu upofu wa haki sawa na harakati zao ndipo ulianza. Wanawake wa zama hizi wana sifa ya mshumaa,wenyewe unaungua na kuisha ukiwanufaisha watu kwa kauli mbiu ya haki sawa.

Wanajidhuru wenyewe huku wakifurahika,huwa nawaambia hakuna nazi iliyo shinda jiwe,wanajidhuru wenyewe huku wakichekelea.
 
Mwanaume aliambiwa atakula kwa jasho.
Mwanamke, utazaa kwa uchungu.

Siku hizi wanawake wanakula kwa jasho na bado wanazaa kwa uchungu wakati wanaume achilia mbali kutokuzaa, hata ile kula kwa jasho inawashinda.
SABABU NI ZIPI KIONGOZI?
 
Samahani nadhani itabidi tueleweshane 50/50 ndo inagawanywa vipi kwa uelewa wangu mimi ni kwamba mnasaidiana majukumu ukichangia ya kifedha nusu kwa nusu yaani ww mfano unalipa pango nusu na mwenzio analipa nusu hio ndio 50/50 ninayoongelea mimi na mabaki mtajadiliana yanatumika vp aidha kama mnaweka akiba au kila mtu anaweka zake mfukoni n.k!
50/50 kwenye hela dada zangu nyinyi ni wagumu mnoooooo,wanawake wenye moyo wakugawa 50/50 kipato chao ktk kumi hawazidi watatu.Halafu hela yenu ni chungu huambatana na masimango na ndio maana ktk maisha yangu sitokuja kuipigia bajeti hela ya mke wangu.

Ndio maana sometimes mwanaume anaamua kumuachisha kazi mke wake sababu haoni huo msaada wa kazi yake.
 
Wanaume hkuna anaelalamika but mwanaum alyekamilika lzma awe juu ya mwanaum kimaamuz kma c hvyo lzm ugomv uwepo tu bcoz hta muumba alitaka hvo
 
Naona wewe bado ni mgeni sana na ulimwengu wa mahusiano sababu umeandika kwa namna ya mtu ambaye hana experience yoyote juu ya maswala ya ndoa.

Nitakuuliza maswali kadhaa na ukiweza kuyajibu pengine tunaweza kuwa katika mlengo mzuri kujadili hii mada yako uliyoleta!

1. Una umri gani?! Nakuuliza umri ili nijue nazungumza na mtu ambaye amepita umbali gani katika utu uzima.

2. Unayajua mahitaji ya mwanaume anayotaka kutimiziwa na mwanamke?! Usiniambie mambo ambayo umesikia, nipe wewe personally unachojua na kama haujui (for the sake of honesty and goodwill) sema sijui nielimishe ila usije na hoja mitandaoni unazookota huko kuhusu wavulana ukiita ni wanaume.

3. Nani role model wako katika haya maisha kama mtoto wakike?! Tafadhali kama katika list ya role models au role model wako hawapo katika ndoa usihangaike kujibu hili swali sababu hatutakuwa na cha kujadili kama role model wako mwenyewe ni kipofu kama wewe.

4. Ni nani aliyekuambia wanaume wanataka mwanamke mjinga au anaepelekwa kama bendera?! So kwa assumption yako ni kuwa tunawatafutia watoto wetu mama ndezi?! (una mengi ya kujifunza kuhusu tofauti ya mke bora na mwanamke wa kawaida wa kisasa)

5. Kama assumption yako ni kuwa wanaume wanalalamika (of which sina uhakika kama huwa unaelewa kinachokemewa au kupigwa kelele na hao unaoita wanaume), je umeshawahi jitathimini wewe kama binti mdogo unaeuingia utu uzima mzito kwa kasi, umejitafakari juu ya uwezo wako na mapungufu yako kwa marejeo ya uhalisia wa namna mwanamke anatakiwa kuwa, yaani kwa mfano wakisema mke bora anatakiwa kuwa na vigezo 50, wewe una vingapi na je unaweza viainisha hapa tuone namna ulivyobora?!

6. Hebu tukiacha tu mijadala na mabishano ya mtandaoni baina ya wavulana na wasichana. Wewe umejipanga vipi kuingia taasisi ndoa kwa muktadha wa mchango gani utatoa kwa mumeo mtarajiwa?! Je huyu mume atapata offer gani ya thamani kutoka kwako tukiacha kumpa mwili wako kwaajiri ya kugegedana, una kipi kipya ambacho upo taayari kutoa bila manung'uniko ya kisichana.

7. Je, ndoa kwako ni jambo takatifu na muhimu?! Kama ni ndio hebu tuambie umejiandaaje kuheshimu hilo agano na maandalizi yako kuliingia, na kama hapana, hebu tueleze ni kwann tena unajihusisha na majadiliano ya mahusiano ile hali ndoa kwako si jambo muhimu.

Jibu hayo kwanza then nikuhoji zaidi.
 
Kama wote tunaingiza kipato na kujiimarisha pamoja kuna tatizo ikiwa 50/50?
50/50 katika muktadha gani, maana sijaelewa point ya kuwa nusu kwa nusu. Kama mtu ana kipato kizuri why ahangaike na pesa ya mkewe.

Na kama mwanamke amepata kazi nzuri na kipato kikubwa kumshinda mume wake, why aanze kutaka kuomba kwa mumewe ampatie si asimamie tu gharama na kuendelea kuwa mke kwa mumewe?!

Mbona sisi wanaume tunalipa bili zote na hatuachi kuwa mume kwa wakd zetu?!

Nadhani mabinti wa kisasa mpo busy kuprove kuwa mnaweza kuwa kama wanaume kiasi kwamba mnajisahau kujifunza uanamke. Matokeo mnafika umri mkubwa na kujua hamuwezi kuwa wanaume sababu mliumbwa wanawake na pia hamuyawezi majukumu yenu ya kike sababu kutokea umri mdogo hadi mnakomaa jamii imewajaza ujinga kuwa ninyi na wanaume ni sawa, something which is biologically, scientifically, economically and politically impossible and not true.
 
Wewe ndio unatimiza majukumu yako yote au unamuongelea nani?

Unamaanisha mwanamke kudai haki sawa ndo kutunisha kifua? Kama mwanamke anafanya kazi kama mwanaume na kujenga familia juu kuna tatizo akidai haki zake?

Na je hawa ambao wanafanya kazi wanaoonekana na mapungufu na si wife material kwasababu wapo independent?
Hebu nikuulize tu swali?!

Unaweza kutuelimisha huu umati mambo yafuatayo;

1. Nini maana ya neno haki?!
2. Mwanamke ana haki zipi?! Tuandikie zote tafadhali tujifunze.
3. Ni haki zipi kati ya hizo ulizosema ambazo wanawake wananyimwa hapa Tanzania au duniani na ni mazingira yapi huwa wananyimwa.
 
SIJAKURUPUKA naona wewe ndio unajitoa fahamu!!Kwasababu unaepuka kujibu kila nilokuuliza!

Wapo kama unajizungumzia jizungumzie wewe usijumuishe wote!

Heshima sio tatizo mbona lakini je unastahiki hio heshima au uheshimiwe tu kwasababu mwanaume au umeoa?Heshima inatakiwa iwepo pande zote!
Naomba unipe ufafanuzi hapa.

Je, mwanaume anaheshimiwa sababu ya jinsia yake ya kiume, kama mwanadamu, kama mpenzi au kama nani hebu tupe ufafanuzi kulingana na upeo wako.
 
Unapomtaja MWANAUME unamzungumzia mtu anayejitambua na aliyekomaa kiakili.....

MVULANA ni kijana mwenye jinsia ya kiume ambaye bado hajakomaa kiakili na anayeongozwa na mihemko badala ya utashi wa akili yake.......

Safari ya kutoka kwenye UVULANA kuelekea kwenye UANAUME hapo ndipo wanapojichuja kati ya wanaume na wavulana...........na hapo panapozuka mtafaruku kwa kuwa wavulana ni wengi kuliko wanaume.......
Ha ha ha ha ha ha bora umempa mwangaza nadhani mabinti wengi wanaongea out of insinuation na sio experience. Matatizo ya kusoma fikra taka za akina Joyce kiria mitandaoni na pia kukaa na mama zao ambao wengi wanachangamoto za maisha yao ya usichana na hawakuwahi pata psycho therapy popote kutibu trauma walizoishi katika experience zao na matokeo wanawatemea watoto wao wakike sumu za namna hii.

Study case Moshi, Mara, Arusha, Machame, etc.
 
Uzi huu unagusia sehemu tofauti rafiki....kwasababu vyote vinategemeana na kimoja kinasababishwa na kingine 50/50 haitokuwa applicable kama wanaume wanataka mfumo dume! Ili 50/50 ifanye kazi watu wenye fikra za mfumo dume inabidi wabadilike!

Swala la wazee kutotaka kupeleka watoto shule unamaanisha kwa jinsia zote mbili au jinsia mmoja?

Katika kongamano la nne la dunia la wanawake lililo fanyika septemba 15 1995 mlilofanya kule Beijing moja hasa ya lengo lake ni ku

empowering women and girls in economic growth and development.maana yake hapo wote hap tuwe na equal rights ktk job opportunities, properties, etc na aspects mbalimbali za maisha

Kwa hyo unataka 50/50 kwa jinsia zote mbili huku ukishangazwa na baadhi ya wanaume ambao mengi ya majukumu yao yanafanywa na wanawake zao sio wao ?


Wanawake bhana


Anyway hio 50/50 mnayoitaka itakua kinywani tu hapa mwendo ni mfumo dume ndo heshima itakuwepo tu sisi ndio watafutaji sisi ndio ma provider sisi ndio viongozi ndio maana kwenye jamii mwanaume kutosimamia haya majukumu utaonekana wa ajabu especially na wanawake na ni kweli unakuwa ni waa ajabu sana


So ukishangazwa na kwa nini baadhi yenu mnafanya majukumu makubwa hapo tayari tuseme usha support mfumo wa siku zote wa zamani " mfumo dume" sema upo kwenye "denial"
 
Wanaume wa sasa mna matatizo gani haswa maana sielewi tatizo lenu ni kwamba hamtaki mabadiliko au akili zimeelemea kwenye mfumo dume au ni nini hasa?Hamna lilo la kheri kwenu,wanaume hamuishi malalamiko mnaongea hata kuwazidi wanawake, maana najua mwanamke ni itikadi yake kupenda kuongea.

Wanaume nyinyi wa karne hii mnataka mtu kama bibi zetu(kitabia na anavyojiweka) na wakati huohuo mnataka mwanamke aliyeelimika,mpenda maendeleo,mchapa kazi n.k ili musaidiane majukumu.
Mnasahau kama bibi zetu jukumu lake kubwa lilikuwa kujenga familia.Kama mwanamke anaingiza kipato kama ww au ikiwezekana kukuzidi wewe mwanaume usitegemee upewe treatment na mwaka 47 lazima mfumo mzima wa maisha ubadilike!
Hii ni 2021 inabidi mubadilike muendane na wakati uliopo waungwana!

Ninachojiuliza hasa ni kwamba mna hofu mkiwa na mwanamke aliyeelimika atawapa changamoto nyingi kwasababu amepambazuka akili na ana upeo wa kufikiri tofauti na ambaye hana elimu?na hamtoweza kumwambia lolote tu akubali bila kutaka kujua kwanini?
Je hilo litapunguza heshima kwenu au litaondoa uanaume wenu?

Tusisahau pia wanawake haohao wachapakazi ndo wanaozaa na kujenga familia kumaanisha wanabeba mzigo mzito kuliko hata wa mwaka 47!

Tuchukulie women empowerment ni kitu chenye manufaa kwa mwanamke na mwanaume na tuache kukandamiza wanawake kwasababu wamepata sauti na kuerevuka!

Tafadhali nahitaji michango ya watu mnaojielewa.Ahsanteni na karibuni!
"Siku utakayo muelewa mwanamke anataka nini, inaweza ikawa ndo siku yako ya mwisho"
 
Back
Top Bottom