Kwanini waraka wa kisheria unaomkataza mwajiri kuingiza makato ya vyama viwili vya wafanyakazi kwa mpigo bila ridhaa ya mtumishi,hauheshimiwi?

Kwanini waraka wa kisheria unaomkataza mwajiri kuingiza makato ya vyama viwili vya wafanyakazi kwa mpigo bila ridhaa ya mtumishi,hauheshimiwi?

JET SALLI

JF-Expert Member
Joined
Dec 1, 2014
Posts
2,392
Reaction score
1,578
Ndugu zangu nimejiuliza maswali kadha wa kadha kuhusu suala la MWAJIRI kupitia ofisi ya Afisa utumishi kuingiza makato ktk mshahara wa mtumishi kwa vyama viwili tofauti vya wafanyakazi ktk mshahara wa mtumishi,nimefuatilia suala la Sumbawanga ,vilevile bado nafuatilia na mikoa,pamoja na wilaya nyingine ili kujua ukubwa wa tatizo hili,na ninaona suala hili la kutokuheshimu kanuni na sheria linatokea sana kwa upande wa WALIMU,Mwezi uliopita niliandika humu kuhusu suala la Mkurugenzi wa MANISPAA ya Sumbawanga,pamoja na Afisa utumishi wake walivyoingiza makato ya vyama viwili ktk mishahara ya walimu bila ridhaa yao na tunajua waraka ambao ndio sheria yenyewe inakataza kabisa tabia hii.Mtumishi ananya kazi Mwezi mzima na analipwa ujira wake hv mtu wa pili anaetamani pesa ambayo Mwalimu huyu kaitolea jasho Mwezi mzima na hivyo anajisikia kuikwapua bila ridhaa ya mwenye pesa ile ni nani.Na ni kweli kabisa CWT wamekua wakifanya kampeni chafu dhidi ya chama mwenza CHAKUHAWATA,Na hii inaonyesha kwa namna gani uwezo wa kufikiri ni mdogo kwa viongozi wa CWT kwa ngazi zote kuanzia kwenye matawi mpaka taifa.Hv kweli unaweza ukatamani kutokupoteza wanachama halafu ukaendelea na ujinga wa zamani usijirekebishe na hivyo ukaendelea kuwa punguwani tu,hii haiingii akili kama kweli CWT ina viongozi wenye akili timamu kabisa lzm Kuna shida.Itoshe kujifunza yafuatayo,ndani ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania vipo vyama vingi vya wafanyakazi kwa uchache nitaje baadhi na taasisi zake.Kwa mfano

a)wafanyakazi wa Serikali kuu vyama vyao ni THT,TEWUTA,RAAWU,
b)Taasisi za fedha vyama vyao ni TUICO na FIBUCA
c)Wafanyakazi wa migodini vyama vyao ni NUMET na TAMICO.
d)Na ndugu zetu waelimishaji wa Taifa ambao ni walimu vyama vyao ni CWT na CHAKUHAWATA.

Watumishi wote wa Serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania wanajiunga na chama chenye unafuu kwao na sio chama kinachofikiria kuvuna fedha bila ridhaa ya mtumishi husika.

Naendelea kutoa WITO kwa serikali sikivu ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania chini ya mama shupavu asiyependa watu waonewe na kuteseka SAMIA SULUHU HASSAN Kuhakikisha kwamba kanuni na sheria za kiutumishi zinaeshimika ndani ya nchi hii kwa kuzingatia sheria ya Ajira na mahusiano kazini namba 6 ya mwaka 2004 na mm kila nikitafakari sielewi kwanini Kwenye sekta ya UALIMU SHERIA HII HAIHESHIMIKI je wakurugenzi,Maafisa Utumishi na wanasheria ktk MANISPAA na wilaya zetu kama inavyotokea kule SUMBAWANGA MANISPAA je wameshindwa kutafsiri sheria na kama wameshindwa kutafsiri sheria iliyo wazi nn kifanyike kwa watu kama hawa wenye kuonyesha uwezo mdogo,wakati Serikali ina hazina ya Rasilimali watu tena wasomi wabobevu haipaswi kuwa na watendaji mfano wa Mkurugenzi wa MANISPAA ya SUMBAWANGA na Afisa utumishi wake kwa mambo wanyowatendea walimu ndani ya MANISPAA ya Sumbawanga.
 
Wapo wachache wenye lengo baya kwa Rais Samia na itakuwa vema kama watashughulikiwa.ili kesho wasianze kusema Mama huyu asiyependa watu kuonewa kashindwa kazi.Wapuuzi wachache wasiotaka kubadilika ni vzr wakapumzishwa.huwezi kuwa Mkurugenzi au Afisa utumishi alafu huwezi kutafsiri mambo ya Msingi na bado ukaendelea kupenda nafasi uliyonayo.Naamini Rais Samia ana watu wake wa karibu wanaopita humu jamii forum taarifa hizi zifike kwa Rais wa nchi hii ili ajue ni akina nani wanamuangusha.
 
Walimu hawa ndio wanaolikomboa Taifa na huwezi kuzungumzia maendeleo ya Tanzania ukamwacha mwalimu Serikali wasaidieni walimu kule Sumbawanga ili makato wanayokatwa ya vyama viwili yatazamwe vzr,tunapaswa kutambua kwamba huu ni unyonyaji,Serikali lifuatilieni hili haraka iwezekanavyo na waliokiuka sheria wachukuliwe hatua haraka.
 
Tunasubiri tuone serikali itachukua hatua gani dhidi wazembe ndani ya ofisi za serikali kama pale Sumbawanga.
 
Watumishi eleweni kuwa sio lazima mfanyakazi awe mwanachama wa chama cha wafanyakazi, ni hiyari yake. Walimu wanadanganywabkuwa ni lazima wawe wanachama wa ama CWT au CHakamwatA (sina uhakika), jambo hilo sio kweli. Jitoeni uanachama, vyama vya wafanyakazi havipo kwa maslahi ya wafanyakazi.

Umekatwa mshahara mara 2, peleka CMA malalamiko yako, mshtaki mwajiri na chama husika
 
Baadhi ya mikoa na wilaya Sasa waraka huo umeanza kuheshimiwa vzr,ila naona bado Sumbawanga walimu bado wanamlalamikia Mkurugenzi wao bwana MTALITINYA J. ambaye hata juzi ktk ziara ya waziri wetu mkuu MAJALIWA, Mkurugenzi huyu kavurunda miradi ya maendeleo hovyohovyo,matumizi ya pesa za serikali pale Sumbawanga inasikitisha sana Mkurugenzi hakika anatia Aibu chama cha mapinduzi CCM Sasa sijui kama serikali itaendelea kukaa na mtendaji wa kiwango cha chini kama huyu Mkurugenzi wa manispaa ya Sumbawanga.
 
Kwanini wanalazimisha watu kuwa wanachama wa hivyo vyama vya kipuuzi?? Kuna haja ya kupeleka kuangalia utaratibu wa kupeleka kesi mahakamani! Makato ya vyama vya wafanyakazi lazima yawe hiyali kwa 100%.
 
Ndugu zangu nimejiuliza maswali kadha wa kadha kuhusu suala la MWAJIRI kupitia ofisi ya Afisa utumishi kuingiza makato ktk mshahara wa mtumishi kwa vyama viwili tofauti vya wafanyakazi ktk mshahara wa mtumishi,nimefuatilia suala la Sumbawanga ,vilevile bado nafuatilia na mikoa,pamoja na wilaya nyingine ili kujua ukubwa wa tatizo hili,na ninaona suala hili la kutokuheshimu kanuni na sheria linatokea sana kwa upande wa WALIMU,Mwezi uliopita niliandika humu kuhusu suala la Mkurugenzi wa MANISPAA ya Sumbawanga,pamoja na Afisa utumishi wake walivyoingiza makato ya vyama viwili ktk mishahara ya walimu bila ridhaa yao na tunajua waraka ambao ndio sheria yenyewe inakataza kabisa tabia hii.Mtumishi ananya kazi Mwezi mzima na analipwa ujira wake hv mtu wa pili anaetamani pesa ambayo Mwalimu huyu kaitolea jasho Mwezi mzima na hivyo anajisikia kuikwapua bila ridhaa ya mwenye pesa ile ni nani.Na ni kweli kabisa CWT wamekua wakifanya kampeni chafu dhidi ya chama mwenza CHAKUHAWATA,Na hii inaonyesha kwa namna gani uwezo wa kufikiri ni mdogo kwa viongozi wa CWT kwa ngazi zote kuanzia kwenye matawi mpaka taifa.Hv kweli unaweza ukatamani kutokupoteza wanachama halafu ukaendelea na ujinga wa zamani usijirekebishe na hivyo ukaendelea kuwa punguwani tu,hii haiingii akili kama kweli CWT ina viongozi wenye akili timamu kabisa lzm Kuna shida.Itoshe kujifunza yafuatayo,ndani ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania vipo vyama vingi vya wafanyakazi kwa uchache nitaje baadhi na taasisi zake.Kwa mfano

a)wafanyakazi wa Serikali kuu vyama vyao ni THT,TEWUTA,RAAWU,
b)Taasisi za fedha vyama vyao ni TUICO na FIBUCA
c)Wafanyakazi wa migodini vyama vyao ni NUMET na TAMICO.
d)Na ndugu zetu waelimishaji wa Taifa ambao ni walimu vyama vyao ni CWT na CHAKUHAWATA.

Watumishi wote wa Serikali ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania wanajiunga na chama chenye unafuu kwao na sio chama kinachofikiria kuvuna fedha bila ridhaa ya mtumishi husika.

Naendelea kutoa WITO kwa serikali sikivu ya Jamuhuri ya muungano wa Tanzania chini ya mama shupavu asiyependa watu waonewe na kuteseka SAMIA SULUHU HASSAN Kuhakikisha kwamba kanuni na sheria za kiutumishi zinaeshimika ndani ya nchi hii kwa kuzingatia sheria ya Ajira na mahusiano kazini namba 6 ya mwaka 2004 na mm kila nikitafakari sielewi kwanini Kwenye sekta ya UALIMU SHERIA HII HAIHESHIMIKI je wakurugenzi,Maafisa Utumishi na wanasheria ktk MANISPAA na wilaya zetu kama inavyotokea kule SUMBAWANGA MANISPAA je wameshindwa kutafsiri sheria na kama wameshindwa kutafsiri sheria iliyo wazi nn kifanyike kwa watu kama hawa wenye kuonyesha uwezo mdogo,wakati Serikali ina hazina ya Rasilimali watu tena wasomi wabobevu haipaswi kuwa na watendaji mfano wa Mkurugenzi wa MANISPAA ya SUMBAWANGA na Afisa utumishi wake kwa mambo wanyowatendea walimu ndani ya MANISPAA ya Sumbawanga.
Yaani kuna Mtu ni mwanachama wa ACT halafu kapewa uanachama wa CCM kwa nguvu na kaambiwa aendelee hivyo hivyo?
 
Tatizo la walimu kutoheshimiwa uamuzi wao wa kujiondoa Cwt na kujiunga na chakuhawata huku wakiwa wamefuata hatua zote kama sheria ya ajira na mahusiano kazini inavyotaka sio kwamba ni tatizo kwa sumbawanga manispaa sumbawanga dc ndio hatusemi kule kuna miungu watu hawasikii wala hawaoni walimu wanapewa visingizio visivyo na kichwa wala miguu sijui Cwt wamewapa nini hadi sheria haziheshimiwi
 
Watumishi eleweni kuwa sio lazima mfanyakazi awe mwanachama wa chama cha wafanyakazi, ni hiyari yake. Walimu wanadanganywabkuwa ni lazima wawe wanachama wa ama CWT au CHakamwatA (sina uhakika), jambo hilo sio kweli. Jitoeni uanachama, vyama vya wafanyakazi havipo kwa maslahi ya wafanyakazi.

Umekatwa mshahara mara 2, peleka CMA malalamiko yako, mshtaki mwajiri na chama husika
Ni hiari Kujiunga na chama Cha wafanyakazi ila ni LAZIMA kukatwa mshahara kwenda kwa chama Cha wafanyakazi.

Loophole hiyo ipo kwenye Sheria ya Ajira na mahusiano kazini, 2004.
 
Ni hiari Kujiunga na chama Cha wafanyakazi ila ni LAZIMA kukatwa mshahara kwenda kwa chama Cha wafanyakazi.

Loophole hiyo ipo kwenye Sheria ya Ajira na mahusiano kazini.
Sio kweli mkuu, sheria uliyoitaja kifungu cha 9(1)(a) kinaeleza kuwa mfanyakazi anaweza kujiunga na chama cha wafanyakazi na akijiunga basi mwajiri atafanya makato kwenda chama hicho, asipojiunga hatakatwa makato yoyote. Isipokuwa pale tu, chama cha wafanyakazi kitapofanya majadiliano kwa niaba yake (collective bargaining), mfano, CWT kinapambana nyongeza ya mishahara ya walimu, serikali ikakubali na mshahara ukaongezwa, mabadiliko yanakuwa kwa walimu wote bila kujali ni wanachama wa CWT au la, hapo CWT watastahili kumkata huyo mwalimu asiye mwanachama wao kwa kuwa amenufaika kwa majadiliano waliyofanya wao. Kiwango watachomkata kinatakiwa kiwe sawa au kiwe kidogo kuliko wanachomkata mwalimu ambaye ni mwanachama. Na watamkata mara moja tu (mwezi mmoja tu) - kifungu cha 72 (3)(c) na 72(4).

Kinyume na hivyo mfanyakazi hatakatwa mshahara wake, mwajiri akikata anakuwa amefanya kosa. Kama kuna loophole inayolazimisha makato, share nasi tuifahamu mkuu
 
Sio kweli mkuu, sheria uliyoitaja kifungu cha 9(1)(a) kinaeleza kuwa mfanyakazi anaweza kujiunga na chama cha wafanyakazi na akijiunga basi mwajiri atafanya makato kwenda chama hicho, asipojiunga hatakatwa makato yoyote. Isipokuwa pale tu, chama cha wafanyakazi kitapofanya majadiliano kwa niaba yake (collective bargaining), mfano, CWT kinapambana nyongeza ya mishahara ya walimu, serikali ikakubali na mshahara ukaongezwa, mabadiliko yanakuwa kwa walimu wote bila kujali ni wanachama wa CWT au la, hapo CWT watastahili kumkata huyo mwalimu asiye mwanachama wao kwa kuwa amenufaika kwa majadiliano waliyofanya wao. Kiwango watachomkata kinatakiwa kiwe sawa au kiwe kidogo kuliko wanachomkata mwalimu ambaye ni mwanachama. Na watamkata mara moja tu (mwezi mmoja tu) - kifungu cha 72 (3)(c) na 72(4).

Kinyume na hivyo mfanyakazi hatakatwa mshahara wake, mwajiri akikata anakuwa amefanya kosa. Kama kuna loophole inayolazimisha makato, share nasi tuifahamu mkuu
Soma kifungu cha 72 (c) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya Mwaka 2004.
 
Soma kifungu cha 72 (c) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya Mwaka 2004.
Mkuu, hakuna kifungu hicho ulichotaja katika Sheria ya Ajira na Uhusiano kazini, lakini nafikiri ulitaka kusema 72(3)(c) ambapo tayari niliitaja katika comment ya awali, kuwa ni makato yanayofanyika pale tu chama cha wafanyakazi kinapofanya majadiliano kwa niaba ya wafanyakazi wote (yaani wanachama na wasio wanachama wao). Kifungu hicho hakitumiki kila siku, ni mara chache sana, na hiyo sio loophole
 
Mkuu, hakuna kifungu hicho ulichotaja katika Sheria ya Ajira na Uhusiano kazini, lakini nafikiri ulitaka kusema 72(3)(c) ambapo tayari niliitaja katika comment ya awali, kuwa ni makato yanayofanyika pale tu chama cha wafanyakazi kinapofanya majadiliano kwa niaba ya wafanyakazi wote (yaani wanachama na wasio wanachama wao). Kifungu hicho hakitumiki kila siku, ni mara chache sana, na hiyo sio loophole
Punguza theory Mkuu.

Uhalisia hauko hivyo.

Kwa taarifa yako Mwajiri ni mnufaika wa Makato hayo, na ndio huyo huyo anayeingiza Makato ya mtumishi kwenye mshahara.
 
Punguza theory Mkuu.

Uhalisia hauko hivyo.

Kwa taarifa yako Mwajiri ni mnufaika wa Makato hayo, na ndio huyo huyo anayeingiza Makato ya mtumishi kwenye mshahara.
Mkuu kwenye huu mjadala usiweke hisia. Weka vifungu kama sajo . Mwenzio anaandika kitachotakiwa kufanyika wewe unaandika kinachofanyika-ambacho ni kosa
 
Punguza theory Mkuu.

Uhalisia hauko hivyo.

Kwa taarifa yako Mwajiri ni mnufaika wa Makato hayo, na ndio huyo huyo anayeingiza Makato ya mtumishi kwenye mshahara.
Naona unageuza ligi na unataka ushindi, hutaki kujifunza. Hivyo unavyosema ni mambo yasiyo ya kisheria, ni utaratibu mbovu kwa watu wasiojua sheria imesemaje. Kwa kuwa ulisema kuna loophole kisheria, tumeitazama sheria yenyewe naona unahamisha goli na kuleta utartibu mbovu wa kimakosa uliouzoea. Wewe nikikwambia wapo watumishi wengi tu wasiokatwa mshahara wa vyama vya wafanyakazi kwa kuwa hawana vyama hivyo, bado unaweza usiamini.
 
Naona unageuza ligi na unataka ushindi, hutaki kujifunza. Hivyo unavyosema ni mambo yasiyo ya kisheria, ni utaratibu mbovu kwa watu wasiojua sheria imesemaje. Kwa kuwa ulisema kuna loophole kisheria, tumeitazama sheria yenyewe naona unahamisha goli na kuleta utartibu mbovu wa kimakosa uliouzoea. Wewe nikikwambia wapo watumishi wengi tu wasiokatwa mshahara wa vyama vya wafanyakazi kwa kuwa hawana vyama hivyo, bado unaweza usiamini.
Wewe jamaa una ubishi wa kichoko kinoma. Unajifanya unajua Sheria kuliko Sheria yenyewe na CMA.

=======

Walimu 347 Kigoma ruksa kujitoa CWT​

TUME ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), imekubali ombi la walimu 347 wa Manispaa ya Kigoma Ujiji kujitoa kutoka katika Chama cha Walimu Tanzania (CWT) ili kuanzisha chama kitakachotetea maslahi yao kutokana na madai kwamba chama hicho cha walimu hakikuwa na msaada kwao katika kutetea maslahi yao.

Akitoa uamuzi wa shauri hilo mjini Kigoma, mwamuzi wa shauri hilo, L.L Mwakyusa alisema baada ya mlolongo mzima wa uamuzi wa pande zinazohusika, Tume imeamua kuwa walalamikaji si wanachama wa CWT tena na kitabaki kuwa wakala kwa walalamikaji kwa kuwa ni chama pekee kinachotambuliwa na mwajiri.

Aidha, Mwakyusa alisema suala la makato kwa walimu hao linapaswa kuangaliwa upya kwa kuwa pande hizo zimeshaingia kwenye mgogoro na kwamba walimu hao hawatafaidi matunda halisi kama wanachama.

Pamoja na uamuzi wa kujitoa kwa walimu hao na kujiunga na chama kingine, alisema walimu hao wataendelea kukatwa ada ya uwakala ili kufaidi matunda ya masuala ya jumla kama walimu yatakayosimamiwa na CWT kwa mujibu wa kifungu cha 72 (c) cha Sheria ya Ajira na Uhusiano Kazini ya Mwaka 2004.

Akizungumzia hukumu hiyo, kiongozi wa kundi hilo la walimu, Kalimwabo Sabibi alisema pamoja na Tume hiyo kuridhia kujitoa CWT, wanakusudia kuanzisha chama kingine cha walimu kitakachosimamia maslahi yao.

Sabibi alisema kwa muda mrefu, walimu wamekuwa kama watoto yatima kutokana na CWT ambacho machoni kinaonekana kama kinasimamia maslahi yao, kudai hakifanyi chochote kwa ajili ya maslahi ya walimu.

Alisema walimu wamekuwa kwenye malumbano ya kudai maslahi yao kutoka kwa mwajiri badala ya chama hicho kuwa upande wao, wakati mwingine kimechangia kuwafanya wakose hata kile kidogo wanachodai.

Pamoja na hukumu hiyo, hata hivyo walimu hao wamesema hawajaridhishwa na uamuzi wa Tume kuruhusu kuendelea kukatwa kwa makato kutoka katika mishahara yao kwa ajili ya kuchangia CWT kwa kigezo cha ada ya uwakala wakati wao si wanachama wa chama hicho.
 
Back
Top Bottom