Kwanini Watanzania wanahofia kupita Zimbabwe katika safari za Afrika Kusini?

Kwanini Watanzania wanahofia kupita Zimbabwe katika safari za Afrika Kusini?

1. Lengo kuu la safari ni kununua gari
2. Lengo la ziada ni kutalii, yaani, kuangalia nchi na miji ya wenzetu. Ndiyo maana ninatamani kupita nchi nyingi na maeneo mengi kadiri iwezekanavyo, kama usalama na bajeti itaruhusu. Ikishindikana kwa sababu mojawapo kati ya hizo mbili, nitafanya litakalowezekana.

Safari ya kwenda South Africa itaanzia Mwanza kwa ndege kupitia Dar Es Salaam hadi Johannesburg. Kutoka Johannesburg nitaenda hadi Pretoria kwa gari la abiria ambapo nitalala siku moja au mbili kwa ajili ya "kulichunguza" jiji. Kisha nitarejesha tena Johannesburg.

Gari natarajia kuchukulia Johannesburg au Durban. Itategemeana na nitakachokikuta maeneo tajwa.

Bila kujali kama gari nitachukulia Johannesburg au Durban, kufika Cape Town ni lazima. Safari kama hizo ni kwa wengi wetu, kwa hiyo nafasi ipatikanapo ni vizuri kuitumia vizuri. Safari ya "kuitafiti" South Africa itakahitimishwa Cape Town. Baada ya hapo, nitakuwa tayari kwa safari ya kurejea Mwanza.

Mpaka sasa, uwezekano uliopo ni kupita NAMIBIA na ZAMBIA, kwa kuzingatia ushauri wa wazoefu wengi.

Japo nimepanga kufika PRETORIA, JOHANNESBURG, DURBAN na CAPE TOWN, si SHERIA. Naweza kufanya adjustment kwa kupunguza au kuongeza miji nitakayofika. Lakini natamani zaidi kuongeza.

Ikitokea nitalazmika kupunguza, basi kipaumbele ni kufika DURBAN na CAPE TOWN. Bila kutia miguu yangu hayo majiji mawili, sitahesabu nimefika South Africa.
Je, unakwenda kununua gari ambalo ni mpya kabisa (brand new) kutoka kiwandani au gari ambalo tayari limetumika (used) ?
Kama unaenda kununua gari used nakushauri tena kwamba ufanye utafiti wako wa kina kuhusu suala hili la manunuzi ya gari kwa sababu kwa mujibu wa Sheria za nchi ya Afrika ya Kusini, ni kosa kisheria kwa mtu yoyote yule ambaye ni raia wa nchi za kigeni na ambaye Hana Viza halali ya kumruhusu kuishi nchini humo kununua gari lililotumika (mtumba) na kisha kuondoka nalo na kwenda (kulisafirisha) nje ya nchi hiyo. Jambo hili haliruhusiwi kisheria, labda kama Sheria hizo zimebadilishwa miaka hii. Biashara ya kuuza magari ya mtumba nje ya nchi hiyo ya South Africa imepigwa marufuku kabisa kisheria, labda kama utaenda kununua gari mpya kutoka kiwandani, hiyo inaruhusiwa.
 
Basi fanya Cape Town- Durban-Msumbiji, au Cape Town-Durban-Estwatini-Msumbiji, then from Msumbiji unaenda Malawi au Zimbabwe na kuendelea kama hapa chini route za Msumbiji au Zimbabwe

Cape Town-Namibia- Botswana (Ngoma)- Zambia- Tanzania (Tunduma)
Cape Town-Namibia- Zambia (Katima Mulilo)- Tanzania (Tunduma)
Cape Town- Botswana(Francis Town) - Zambia-Tanzania (Tunduma)
Cape Town- Botswana (Francis Town)- Zambia-Malawi-Tanzania (Kyela)
Cape Town-Msumbiji - Zimbabwe- Malawi-Tanzania (Kyela)
Cape Town- Zimbabwe (Beit Bridge) - Zambia-Tanzania (Tunduma)
Cape Town-Namibia-Botswana(Ngoma) -Zambia-Malawi-Tanzania (Kyela)
Cape Town-Namibia-Angola-Kongo-Burundi-Tanzania (Kigoma)
Cape Town-Namibia-Angola-Zambia-Tanzania (Tunduma)
Cape Town-Namibia-Angola-Kongo (Lubumbashi) -Zambia-Tanzania (Tunduma)
Msumbiji kukoje kiusalama?
 
Je, unakwenda kununua gari ambalo ni mpya kabisa (brand new) kutoka kiwandani au gari ambalo tayari limetumika (used) ?
Kama unaenda kununua gari used nakushauri tena kwamba ufanye utafiti wako wa kina kuhusu suala hili la manunuzi ya gari kwa sababu kwa mujibu wa Sheria za nchi ya Afrika ya Kusini, ni kosa kisheria kwa mtu yoyote yule ambaye ni raia wa nchi za kigeni na ambaye Hana Viza halali ya kumruhusu kuishi nchini humo kununua gari lililotumika tayari na kisha kuondoja nalo kwenda (kulisafirisha) kwenda nje ya nchi hiyo. Jambo hili haliruhusiwi kisheria, labda kama Sheria hizo zimebadilishwa miaka hii. Biashara ya kuuza magari ya mtumba nje ya nchi hiyo ya South Africa imepigwa marufuku kabisa kisheria, labda kama utaenda kununua gari mpya kutoka kiwandani, hiyo inaruhusiwa.
La mtumba mkuu! Kuna Shuhuda za wadau wengi wanaodai waliyachukulia huko South Africa.
 
La mtumba mkuu! Kuna Shuhuda za wadau wengi wanaodai waliyachukulia huko South Africa.
Okay sawa.

Lakini unapaswa kuwatafiti kwa undani zaidi hao Watu kuhusiana na suala hili. Usije ukaingia kwenye Mgogoro wa kisheria dhidi ya Serikali za huko uendako. Wenzetu kwenye nchi zao kuna utawala wa Sheria, nobody is above the law.
Uwaulize, Je, wakati waliponunua hayo magari ya mtumba huko South Africa, walikuwa na Viza ya kuishi huko au walienda tu mara Moja Kama wageni wengine wa kimataifa wenye kibali cha muda mfupi tu cha kuwepo huko??
Pia, ufuatilie na ujiridhishe juu ya uhalali wa manunuzi ya magari yao waliyonayo kwani South Africa ndiyo nchi inayoongoza kwa uhalifu hapa barani Afrika, ikiwamo na uhalifu wa kughushi katika biashara ya kuuza au kununua magari.
 
Okay sawa.

Lakini unapaswa kuwatafiti kwa undani zaidi hao Watu kuhusiana na suala hili. Usije ukaingia kwenye Mgogoro wa kisheria dhidi ya Serikali za huko uendako. Wenzetu kwenye nchi zao kuna utawala wa Sheria, nobody is above the law.
Uwaulize, Je, wakati waliponunua hayo magari ya mtumba huko South Africa, walikuwa na Viza ya kuishi huko au walienda tu mara Moja Kama wageni wengine wa kimataifa wenye kibali cha muda mfupi tu cha kuwepo huko??
Pia, ufuatilie na ujiridhishe juu ya uhalali wa manunuzi ya magari yao waliyonayo kwani South Africa ndiyo nchi inayoongoza kwa uhalifu hapa barani Afrika, ikiwamo na uhalifu wa kughushi katika biashara ya kuuza au kununua magari.
🙏🙏🙏
 
Sijawahi kufika kwenye hizo nchi, lakini naamini nitafanya hivyo muda si mrefu.Lakini kwa stori za hapa JF, wengi wa wadau wanashauri kutokupita Zimbabwe kwa safari za kwenda Afrika Kusini.

Natamani, katika safari yangu, niende kwa ndege, lakini wakati wa kurudi, nitumie usafiri wa usafiri wa gari binafsi. Lengo ni ili kufaidi mandhari ya Mataifa mbalimbali, hasa Namibia, Botswana, Zimbabwe, Zambia, na Malawi, kama hakutakuweko na kizuizi cha kupita huko.

Kama ninazo nyaraka zote zinazohitajika, ikiwa ni pamoja na za kununulia gari South Africa, bado kutakuwepo na ulazima wa kukwepa kupita Zimbabwe?

Kama itawezekana kutumia route itakayoniwezesha kupitia nchi zote hizo, ni mambo gani ya kuzingatia ili kuepuka usumbufu usio wa lazima?
Zimbabwe,
1. Barabara mbovu zaidi,
2. Rushwa, polisi/Trafiki,
3. Utekaji barabarani.
 
Kitu kikubwa hakikisha unaingia kihalali, naamini hili litakuwa maana unaenda kwa ndege.

Cha pili, hakikisha una documents zote za gari na mauziano ya gari na zipatikane kwenye mamlaka husika ulipe ushuru wao wote. Ukicheza hapa inakula kwako.
La mtumba mkuu! Kuna Shuhuda za wadau wengi wanaodai waliyachukulia huko South Africa.
Katika safari yako Ondoa Zimbabwe kabisa.

Pia Msumbiji kwa sasa sidhani kama bi sehemu sahihi kwasababu za vurugu za baada ya uchaguzi.

Itapendeza hii route ya
1. Botsawana Zambia TZ, au
2. BoT Zam Malawi Tz
3. Namibia Zambia, Tz
4. Namibia Zambia Malaw Tz.

NB. Barabara ya Lusaka Tanzania haikuwa nzuri sana, sijui kwa sasa. Ndio maana inakuwa vizuri ukiingia Zambia unachepukia Malawi barabara ni nzuri hadi Kyela
 
Okay sawa.

Lakini unapaswa kuwatafiti kwa undani zaidi hao Watu kuhusiana na suala hili. Usije ukaingia kwenye Mgogoro wa kisheria dhidi ya Serikali za huko uendako. Wenzetu kwenye nchi zao kuna utawala wa Sheria, nobody is above the law.
Uwaulize, Je, wakati waliponunua hayo magari ya mtumba huko South Africa, walikuwa na Viza ya kuishi huko au walienda tu mara Moja Kama wageni wengine wa kimataifa wenye kibali cha muda mfupi tu cha kuwepo huko??
Pia, ufuatilie na ujiridhishe juu ya uhalali wa manunuzi ya magari yao waliyonayo kwani South Africa ndiyo nchi inayoongoza kwa uhalifu hapa barani Afrika, ikiwamo na uhalifu wa kughushi katika biashara ya kuuza au kununua magari.
Ulishawah kuvuka border toka uzaliwe. Punguza ujuaji kwenye mambo usiyoyafahamu. Unataka Sheria, Sheria bila kutaja kifungu?. Humu kuna kina Isanga family wanakera Magari toka SA kila siku wewe upo kwa shemeji yako Buza kwa Rulenge unaongea habari za SA
 
Kitu kikubwa hakikisha unaingia kihalali, naamini hili litakuwa maana unaenda kwa ndege.

Cha pili, hakikisha una documents zote za gari na mauziano ya gari na zipatikane kwenye mamlaka husika ulipe ushuru wao wote. Ukicheza hapa inakula kwako.

Katika safari yako Ondoa Zimbabwe kabisa.

Pia Msumbiji kwa sasa sidhani kama bi sehemu sahihi kwasababu za vurugu za baada ya uchaguzi.

Itapendeza hii route ya
1. Botsawana Zambia TZ, au
2. BoT Zam Malawi Tz
3. Namibia Zambia, Tz
4. Namibia Zambia Malaw Tz.

NB. Barabara ya Lusaka Tanzania haikuwa nzuri sana, sijui kwa sasa. Ndio maana inakuwa vizuri ukiingia Zambia unachepukia Malawi barabara ni nzuri hadi Kyela
Sasa hivi kimebaki kipande kidogo tu kutoka Mpika kuitafuta Isoka nadhani ndio bara bara mbovu ila inatengenezwa ukifika Chinsali ni mkeka mkubwa na mpana mpaka Nakonde..
 
Sawa, lakini napenda sana utalii! Nitafurahi endapo nitaweza kupita nchi zote nilizozitaja.

Kama kungekuwa na USALAMA CONGO DRC, ningeijumuisha nayo pia. Kwamba ningepita NAMIBIA, BOTSWANA, ZIMBABWE, ZAMBIA, MALAWI, CONGO DRC, RWANDA, BURUNDI, UGANDA, KENYA, kisha naingia home kwangu MWANZA.
Congo labda uende Kasumbalesa then Rudi Ndola-Kapiri Mposhi-Nakonde/Tunduma
 
Ulishawah kuvuka border toka uzaliwe. Punguza ujuaji kwenye mambo usiyoyafahamu. Unataka Sheria, Sheria bila kutaja kifungu?. Humu kuna kina Isanga family wanakera Magari toka SA kila siku wewe upo kwa shemeji yako Buza kwa Rulenge unaongea habari za SA
Ulishawah kuvuka border toka uzaliwe. Punguza ujuaji kwenye mambo usiyoyafahamu. Unataka Sheria, Sheria bila kutaja kifungu?. Humu kuna kina Isanga family wanakera Magari toka SA kila siku wewe upo kwa shemeji yako Buza kwa Rulenge unaongea habari za SA

Nafikiri wewe bado unaishi katika Mazingira ya ulimwengu wa kufikirika.

Kwa mujibu wa Sheria za Afrika Kusini, hairuhusiwi KUFANYA biashara ya kununua magari ambayo tayari yameshatumika nchini humo (used cars) na kisha kuyasafirisha kwenda nje ya nchi hiyo kwa mtindo wa kufanya biashara ya Kimataifa ya magari yaliyokwisha tumika. Biashara ya namna hiyo inaruhusiwa kwa magari mapya tu (brand new cars).
 
Zimbabwe ni shida sana! Sikushauri upite huko.
Mimi nilipita last year January, Nilitoka SA kununua gari, aisee police wa pale mpakani Victoria Falls walinisumbua sana mpaka nilijuta.
Kinachokera zaidi ni kuwa nilikuwa na nyaraka zote halali but walikuwa wanatafuta kila sababu za kunichomoa hela.
nilijiuliza sana hivi hawa Ndo Nyerere alipambana wapate uhuru halafu wanatufanyia hivi watanzania?
 
Back
Top Bottom