Kwanini Watanzania wengi wanaenda Uganda (Makerere University) Kusoma?

Kiufupi Tanzania hakuna elimu Bali kunamakapi ya elimu.Ndiyo maana watu wanaokaa mipakani kama kule tarime na Tanga wengi wao wanasoma Kenya kuanzia shule ya msingi.Hivyo Hivyo na watu wa bukoba husoma Uganda kuanzia shule ya msingi na chuo.Hata watu wenye pesa au hata viongozi wetu huwezi kumwona mwanae anahangaika na vi vyuo uchwara vya hapa nyumbani.Mfumo wetu wa elimu ni wa hovyo hasa kwenye lugha ya kufundishia inawafanya wtz wawe nyuma Kila kitu.
 
duuuh kwaiyo Tatizo ni kiswahili au tatizo ni Quality ya elimu?
 
jipige konzi kwa maamuzi ya kijuha
kusoma tz ni vile watu hawana pesa. wenye pesa wanapeleka nje.
elimu imesihasishwa na kuchezewa. quality control ni sifuri.
 
Kiswahili kuwa lugha ya kufundishia ni chanzo kikubwa cha ubovu wa elimu. Vyuoni bila lecturer kuelezea tena jambo kwa kiswahili wanaoelewa huwa wachache. Binafsi kiingereza changu kilikuja kunyooka sana nilipoanza kutokatoka nje ya TZ.
 
Ahahh sijajua vizuri kuhusu hilo
Ilikuwepo Wizara ya Elimu ya Juu,Sayansi na Teknolojia na Mzee Mkapa amewahi kuwa Waziri kwenye hiyo Wizara,yenyewe ilikuwa niasimamia Elimu ya Juu tu. Sasa wanasiasa wetu wakaivunja hiyo wizara na kuibebesha mzigo mzito Wizara ya Elimu
 
Ilikuwepo Wizara ya Elimu ya Juu,Sayansi na Teknolojia na Mzee Mkapa amewahi kuwa Waziri kwenye hiyo Wizara,yenyewe ilikuwa niasimamia Elimu ya Juu tu. Sasa wanasiasa wetu wakaivunja hiyo wizara na kuibebesha mzigo mzito Wizara ya Elimu
πŸ‘
 
Bongo unakuta chuo kinachukua best student afundishe first year wajao. Unategemea tuwe na University za maana kweli.

Kimsingi chuo kikuu kinatakiwa wakufunzi wawe PhD holders ila bongo sasa ni huzuni kubwa.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…